Monday, February 18, 2013

MASHAURIANO KUUNDWA KWA SERIKALI MPYA TUNISIA


 

Mashauriano kuhusu kuundwa kwa serikali mpya nchini Tunisia yanakusudiwa kuanza tena. Waziri mkuu Hamadi Jebali anataka kubuni utawala wa kiteknokrasia. Mfumo huu wa kiteknokrasia hujumuisha utawala unaongozwa na wahandisi, wanasayansi na wataalam wengine. Lakini hatua hiyo inapingwa na kiongozi wa chama chake cha Ennahda, Rached Ghannouchi. Bwana Jebali ametishia kujiuzulu iwapo uamuzi wake, anaotarajia kuwa suluhisho la kisiasa nchini humo, utaendelea kupingwa na Ennahda.

Mzozo wa kisiasa ulizuka baada ya kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa upinzani nchini humo, Chokri Belaid. Familia ya Bwana Belaid ilikilaumu chama hicho kwa kupanga mauaji yake. Chama hicho cha Kiislamu cha Ennahda kimegawanyika kati ya walio na msimamo wa kadri, wakiongozwa na waziri mkuu, na wale wenye itikadi kali, wanaoongozwa na Bwana Ganouchi.


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment