Friday, February 15, 2013

CHRIS MARTIN AWAGUSA WASWAHILI, KUMBE JAMAA ANAJUA KISWAHILI .


Chris Martin amedhihirisha kukolewa kwake na Afrika Mashariki na hii pengine ni kutokana na show zake kubwa ambazo amezipiga katika nchi za Uganda na Kenya kwa wakati tofauti na hii ni kutokana na mshkaji huyu kudhihirisha kuwa lugha 'hadhimu' ya Kiswahili haimpigi chenga.
Christopher Martin
Investigation ya www.sammisago.com imelithibitisha hili pia na kugundua kuwa ni kweli msanii huyu wa miondoko ya reggae ana-feel Kiswahili, na hiki ndicho tulicho kutana nacho kwenye twitter timeline yake...

                       
Kama bado huamini, #FACT iis.. Yeah, for real, Jamaa Kiswahili kinapanda kimtindo.

Mshkaji leo anatimiza miaka 26 tokea kuzaliwa kwake mwaka 1987, ni mkali mwenye hits kibao kutoka Jamaica, Chris Martin, Hits zake kama vile Cheaters Prayer na Paper Loving ndio zime-establish jina lake vizuri kabisa Afrika Mashariki, Happy Birthday to him na wewe ambaye pia leo unaadhimisha siku yako ya kuzaliwa.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment