Friday, November 30, 2012

MAAJABU YA DUNIA; ANGALIA PICHA JAMAA AKIFUFUKA DAKIKA CHACHE KABLA YA KUZIKWA




He woke up few minutes before his burial. When he came back from the beyond, even his closest relatives and the bravest in the village ran into the bush for safety.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, November 27, 2012

SIMBA WAMLILIA SHARO MILLIONEA - Alikuwa anataka kuwatungia wimbi



 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Mhe; Ismail Aden Rage, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa aliyekuwa msanii maarufu wa muziki na filamu, Hussein Ramadhani Mkiety, maarufu kwa jina la Sharo Milionea, kilichotokea jana usiku mkoani Tanga.
Kwa niaba ya klabu ya Simba na kwa niaba yake binafsi, Mwenyekiti anapenda kutuma salamu za pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu kutokana na msiba huu mkubwa sana si kwao pekee bali kwa taifa zima la Tanzania.
Sharo Milionea hakuwa msanii wa kawaida. Yeye ni miongoni mwa kizazi kipya cha vijana wa Kitanzania walioamua kutafuta maisha kwa kutumia vipaji walivyopewa na Mungu. Yeye alijitumbukiza zaidi katika uchekeshaji na baadaye akaonyesha uwezo mkubwa katika fani ya muziki.
Sharo alikuwa maarufu kiasi kwamba makampuni makubwa yalikuwa yameanza kumtumia kwenye matangazo yao ya kibiashara. Hii ilionyesha kwamba makampuni yalibaini faida itakayopatikana kwao kwa kumtumia msanii huyu ambaye bado alikuwa na heshima kubwa kwenye jamii kutokana na haiba yake na uwezo wake kwenye kazi alizokuwa akifanya.
Msiba huu umekuwa pigo kubwa kwa tasnia ya filamu ambayo bado inaomboleza vifo vya wasanii kama Steven Kanumba, Mlopelo na John Steven Maganga, waliofariki dunia mwaka huu pia.
"Ifahamike kwamba Sharo Milionea alikuwa miongoni mwa wasanii wa Kitanzania waliotuma maombi Simba ya kutaka kushiriki kwenye mchakato wa kutengeneza wimbo rasmi wa klabu ya Simba. Yeye alikuwa miongoni mwa wasanii waliokuwa wakiumizwa na ukweli kwamba klabu kama Simba inashindwa kufanya biashara ya kuuza nyimbo zake ilhali wanunuaji wapo," alisema Rage.
Kwa klabu ya Simba, namna pekee ya kumuenzi marehemu ni kufanyia kazi mambo ambayo alikuwa akitushauri kwenye eneo la biashara. Ni matumaini yetu kwamba iwapo tutafanya lile alilokuwa akitushauri, atakuwa mwenye amani huko alikotangulia mbele ya haki.
Rage amewaomba wasanii wa tasnia ya filamu na muziki kuwa watulivu na wenye subra kwenye kipindi hiki kigumu kwao. Kila kitu katika maisha ya wanadamu kinapangwa na Mwenyezi Mungu na ndiyo maana Waswahili wana msemo kuwa Kazi ya Mungu haina makosa.
Mola na ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Hussein Ramadhani Mkeity (Sharo Milionea).
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

ALIYEKUWA MSANII WA BONGO MOVIES, JOHN MAGANGA AAGWA :NAPE AWAKILISHA CCM


 



 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM,  Nape Nnauye akitoa salamu za Chama, kwenye msiba wa msanii, Joseph Maganga, Mwananyamala, Dar es Salaam leo.
Wasanii wa Bongo Movies wakibeba jeneza lenye mwili wa msanii mwenzao, John Maganga, wakati wa kuaga mwili huo, Mwananyamala, Dar es Salaam leo.
Msanii wa Bongo Movies,  Husna Maulidi 'Lishez', akitulizwa na wenzake, Babby Candy na Ketty wakati akilia kwa uchungu, wakati wa kuaga mwili wa Msanii wa Bongo Movies, marehemu  John Maganga leo.
Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi CCM, Nape Nnauye akiwa kwenye shughuli ya kuaga mwili wa msanii, John Maganga, Mwananyamala, jijini Dar es Salaam leo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpa pole Stephen Maganga, baba wa msanii John Maganga wakati wa kuaga mwili wa msanii huyo, Mwananyama, Dar es salaam leo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpa pole Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba (kulia).
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

TAARIFA KAMILIKUHUSU KIFO CHASHAROMILLIONEA.



Taarifa kuhusu kifo cha Msanii wa
maigizo na Mziki wa Bongo fleva
kufariki zimasamba nchi nzima
masaa machache yaliopita.
Kwa mujibu wa Sam Misago.Com ni
kwamba amepata uthibitisho
kutoka kwa diwani Makame Seif
ambaye ni rafiki yake wa karibu
sana wa Marehemu Hussen
Ramadhani Mkiete maarufu kama
Sharo Millionea amepata ajali mida
ya saa mbili eneo la maguzoni
Tanga na amefariki dunia papo
hapo. Polisi wametambua ni Sharo
Millionea kwa vitambulisho vyake
na picha moja ya passport aliokuwa
nayo mfukoni ambavyo kwa sasa
viko na polisi.
Diwani huyu amemfahamisha
mwandishi kuwa Sharo Millionea
ameumia vibaya sana kichwani,
kifuani na kwenye mikono. Pia
Mjomba wa marehemu
amethibitisha kuwa Sharo Millionea
atazikwa Tanga na asubuhi ya leo
ratiba ya msiba itatolewa. Ndugu
na marafiki wa Sharo wameanza
kwenda hospitalini baada tu ya
taarifa hizi kuwafikia. Familia ya
Sharo imeshafika Hospitali ya Teule
ya Tanga.
Tunamuombea Ndugu yetu SHARO
MILLIONEA Apumzike Kwa
Amani....


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

HIVI NDIVYO MWILI WA MAREHEMU SHARO MILIONEA ULIVYO BAADA YA KUPATA AJALI ** TUNAOMBA RADHI KWA PICHA UTAKAYOONA **



IVI NDIVYO MWILI WA MAREHEMU
SHARO MILIONEA ULIVYO BAADA YA
KUPATA AJALI ** TUNAOMBA RADHI
KWA PICHA UTAKAYOONA *


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

MSIKILIZE KAMANDA WA POLISI WA TANGA AKIONGEA KUHUSU KIFO CHA MSANII SHARO MILIONEA


Kuhusu kifo cha msanii /mwigizaji Sharo
Milionea , namkariri Kamanda wa Polisi
Tanga akisema “ leo majira ya saa mbili
usiku kwenye barabara ya Segera Muheza
mtu mmoja alietambulika kwa jina la
Hussein Ramadhani au Sharo Milionea
akiwa anaendesha gari namba T 478 BVR
Toyota Harrier akitokea Dar es salaam
kwenda Muheza alipofika eneo hilo gari
lake liliacha njia na kupinduka mara
kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili
wa marehemu umehifadhiwa kwenye
hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”
Kamanda amesema hakuna kona kali sana
wala ubovu wa barabara kwenye sehemu
aliyopata ajali Sharo Milionea , katikati ya
Segera na Muheza ambapo gari
imehifadhiwa mahali salama kwa sababu
haitembei. Kwenye gari alikua mwenyewe.

by G5 NEWS


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Monday, November 26, 2012

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZZ ZZ HIVI PUNDE: MSANII SHARO MILLIONEA AFARIKI DUNIA HIVI PUNDE



Msanii mahiri wa uchekeshaji
na mwanamuziki wa Bongo
Fleva Sharo Millionea amefariki
katika ajali ya gari huko Muheza
mkoani Tanga hivi punde.
R.I.P SHARO MILLIONEA:


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Saturday, November 17, 2012

WASANII HII SI YAKUACHA KUSOMA KWANI INAWAHUSU SANA




MAKALA NA   TRIM SALEEM (Trim Saleem)
Suala la usambazaji wa films za kitanzania ni moja ya vitu vinavyolalamikiwa sana kuwa limejaa upendeleo kwa wasanii wenye majina makubwa na wachanga kupuuzwa, vile vile hata hao wenye majina nao wananyonywa kama kawa licha ya 

kwamba uharamia nao unaonekana kuota mapembe bila juhudi thabiti za kuuteketeza ingawa upo duniani kote. ila inatakiwa wasanii kuungana na pia kuishinikiza serikali ili ijenge majumba ya cinema maana haya huwa ndiyo chanzo kikubwa cha mapato ya films na hata kuamuliwa kama film ni hit or flop kutokana na kuwa wazi zaidi hasa katika suala la uuzaji wa tiketi kuliko uuzaji wa dvd, vcd, net au tv broadcast ingawa vyote hivi ni vyanzo vikuu vya mapato ila majumba ya sinema ndo hutegemewa zaidi.

Hapa nchini kuna majumba machache ya sinema lakini ukiyaangalia sana ni kama hayapo Tanzania maana mara nyingi yanaonyesha films za hollywood na bollywood/ india ingawa pia watengenezaji wa films za kitanzania wanaonekana kukosa ufahamu au weledi wa kutumia majumba haya, ila ikiwa wasanii wataungana na kufanya harambee za kukusanya pesa kwa kuanzia hata na majumba 2 au 3 kwa msaada wa serikali na wao wenyewe hili linawezekana na ni moja ya njia ya kuwashikisha adabu baadhi ya wasambazaji waliojaa unyonyaji huku wakikosa ubunifu wa namna ya kutangaza films ambazo sio za kimapenzi ili ziuzike yaani wasambazaji hawa ni kama hawana nia ya dhati ili films zetu zifike mbali ila mapenzi tu ndio films! suala hili linawezekana ikiwa wasanii wataacha kufanya sherehe au party zisizo na kichwa wala miguu kila siku na kuchangishana pesa nyingi kwenye harusi halafu ndoa zenyewe nyingi hazidumu zikiwa na lengo la kujionyesha tu mbele za watu ,na ikumbukwe kuwa kuna wafanyabiashara wazalendo wengi tu ambao wanaweza kuwa interested na hata kuwekeza kwenye project kama hizi ikiwa wataona wasanii wenyewe wana maono ya mbali ili kufanikiwa, na ikiwa hili litatiliwa maanani basi hata ndani ya miaka 5 ijayo tayari njia nzuri itakuwa ishaanza kuonekana kuliko hali ilivyo sasa msambazaji ndio huamua kuwa film imeuza au haijauza hata kabla haijaingia sokoni wakati wa kuliamua hili ni wanunuzi au mashabiki wenyewe baada ya kuona film sokoni . 

Ukweli ni kuwa Tanzania ina nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri kuliko hata Nigeria maana Nigeria yenyewe imeanza muda kidogo ila kuna films nyingi ukiziangalia zina makosa kibao kama za kibongo na hii ndiyo sababu licha ya Nigeria kuzalisha utiriri wa films kibao kila siku lakini nyingi zinashindwa kushindana na chache kutoka south Afrika ambazo zinatamba mpaka nje ya bara la afrika wakati za Nigeria nyingi zimeishia barani afrika. Ikiwa tutaendelea kutegemea uuzaji wa dvd na vcd kama chanzo kikuu cha mapato wakati india na hollywood huwa chanzo kingine baada ya majumba ya cinema hatuwezi kuwa mabilionea kupitia films hata siku moja na amin usiamini majumba ya sinema yakijengwa wasambazaji watakuwa na nidhamu kwa maproducer na hata kuwashobokea ili wafanye biashara kuliko sasa, pia haya majumba machache yaliyopo yataacha kasumba zao na kugeukia films za kitanzania. ila hili litawezekani kwa asilimia kubwa huku tukiwa tunazidi kuziboresha films zetu ili huko kwenye cinemas tusije kuwachosha watu kama ilivyo sasa mtu hata nyumbani kwake film ya kibongo inamboa . suala la kuwa sisi ndo kwanza tumeanza lisiwe kigezo cha sisi kuchukuwa miaka kibao ili kufika mbali maana walioanza zamani mazingira yao yalikuwa magumu kuliko ulimwengu wa leo. pichani ni THEA 1 wa waigizaji wetu wachache wenye viipaji halisi ambavyo vinatakiwa ili kuifikisha tasnia hii anga za kimataifa
 
via:bongofilmdatabase.blogspot.com

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, November 6, 2012

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII ATEMBELEA BANDA LA TANZANIA KATIKA MAONYESHO YA UTALII YA WTM YANAYOFANYIKA JIJINI LONDON UINGEREZA



Waziri wa maliasili za Utalii Balozi Khamis Kagasheki akihojiwa na kituo cha Televisheni ya Taifa TBC mara baada ya kutembelea mabanda ya makampuni ya Tanzania yanayoshiriki katika maonyesho ya Utalii ya World Travel Market yanayoandaliwa na kufanyika katika eneo la Excell jijini London nchini Uingereza, yakishirikisha makampuni mbalimbali ya utalii kutoka pande zote za dunia, Mwaka huu Tanzania inawakilishwa na makampuni zaidi ya 55 yakiwa chini ya Bodi ya Utalii nchini Tanzania (TTB).
 
Waziri Balozi Kagasheki amesifushiriki wa makampuni ya Tanzania katika maonyesho hayo lakini amesisitiza kwamba makampuni hayo yaongeze juhudi za kutangaza utalii wa Tanzania mpaka kufikisha lengo la idadi ya watalii milioni moja kila mwaka, ameongeza kwamba kuna haja ya kuongeza vitanda zaidi nchini Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii watakaotembelea katika mbuga zetu na kufanya utalii kuka zaidi, Maonyesho hayo yatazinduliwa rasmi kesho.
Fullshangweblo iko jijini London nchini Uingereza ikikumuvuzishia matukio haya moja kwa moja kutoka katika maeneo ya Excell ambako ndiko maonyesho hayo yanafanyika.
 
PICHA NA FULLSHANGWEBLOG.COM
 
Waziri aliasili na Utalii wa Balozi Khamis Kagasheki akisalimiana na Issa Ahmed Othman Mshauri wa Rais masuala ya Utalii Zanzibar wakati alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho ya utalii ya (WTM) jijini London leo nchini Uingereza
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Leila Ansel Mkuu wa mauzo na masoko kampuni ya Tanzania Zara Adventures wakati alipotembelea katika banda hilo leo kwenye maonyesho ya utalii ya WTM nchini Uingereza.
Yvone Baldwin Afisa mauzo wa kampuni ya ndege ya Precision Air akimkabidhi zawadi Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mh. Peter Kallaghe mara baada ya kutembelea banda hilo leo akiongozana na Waziri wa Maliasili Balozi Khamis Kagasheki.
Waziri wa Maliasili Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Rashid Adam Meneja Masoko wa Tanzania Zara Adventures wakati alipotembelea maonyesho ya Utalii ya WTM katika banda la Tanzania leo jijini London, wa pili kutoka kushoto ni Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na katikati ni mama Balozi.
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Laura Meneja wa Maendeleo ya Biashara kampuni ya Laitolya Tours & Safari Ltd kushoto wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonyesho ya WTM leo, kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi.
Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi akiwahudumia watu mbalimbali waliotembelea katika banda la Tanzania leo katika maonyesho ya Utalii ya WTM jijini London Uingereza
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii ya Tanzania TTB Bw. Geofrey Meena akiwa katika picha ya pamoja na wakurugenzi wa African Environments Richard Beatty na Janice Beatty katika maonyesho hayo.
Leila Ansel Mkuu wa mauzo na masoko kampuni ya Tanzania Zara Adventures akizungumza na mmoja wa wageni waliotembelea katika banda la kampuni hiyo katikati ni Rashid Adam Meneja Masoko wa Tanzania Zara Adventures.
 
Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza akizungumza na mdau Juma Mabakila wakati akitembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho ya WTM
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii ya Tanzania TTB Bw. Geofrey Meena akiwasikiliza wageni mbalimbali waliofika katika banda la Tanzania katika maonyesho hayo leo.
Balozi Khamis Kagasheki Waziri wa Maliasili Utalii wa pili kutoka kulia akizungumza na Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi mara baada ya kutembelea Banda la Tanzania katika maonyesho ya Utalii ya WTM nchini Uingereza , kulia ni Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na katikati ni Mama Balozi.
Mmoja wa washiriki kutoka kampuni ya Africa Adventure akihojiwa na kituo cha televisheni cha TBC katika maonyesho ya Utalii ya WTM yanayofanyika jijini London nchini Uingereza.
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakati alipotembelea maonesho hayo kushoto ni Meneja wa Masoko wa Bodi ya Utalii nchini TTB.
Washiriki mbalimbali wakiwa katika banda la Tanzania wakipokea wageni mbalimbali wanaotemelea kwenye banda hilo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu utalii wa Tanzania.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

NYANGUMI YAWAJERUHI WATU WATATU



Nyangumi

Watu watatu wamejeruhiwa baada ya Nyangumi kuibuka ghafla na kurukia boti waliyokua wakisafiria huko Eastern Cape Afrika Kusini.

Boti ilikua inakwenda polepole ghafla Nyangumi akajitokeza toka chini ya maji na kurukia hiyo boti, waliojeruhiwa ambao baadae kidogo waliokolewa na kikosi cha uokoaji ni mzee wa miaka 41 na abiria wengine wenye umri wa miaka 25 na mwingine 35.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Friday, November 2, 2012

LOST FAMILY COMING SOON



 POSTERZ











MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.