Tuesday, July 31, 2012

ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013


WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013 

MAELEKEZO MUHIMU

Waombaji waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu katika mwaka wa masomo 2012/13 wanatakiwa kuripoti katika vyuo walivyopangiwa tarehe 12/08/2012. Kwa wale watakaochelewa kupata barua za maelekezo (Joining instruction) kutoka vyuoni wanatakiwa waripoti vyuoni katika tarehe iliyopangwa bila kukosa. Wanafunzi wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:

 1.Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA kulingana na kozi husika.

 2. Ada kwa mwaka ni shilingi 200,000/=. (Muhula wa kwanza shilingi 100,000/= na muhula wa pili shilingi 100,000/=). 

3.Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika . 

4. Fedha za matumizi binafsi. 

Aidha, kila Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SI vinginevyo.

BOFYA HAPA KUANGALIA ORODHA YA MAJINA

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA MWAKA WA MASOMO 2012/2013


 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA  MWAKA WA MASOMO 
2012/2013


MAELEKEZO MUHIMU
Waombaji waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya Stashahada katika mwaka wa masomo 2012/13 wanatakiwa kuripoti katika vyuo walivyopangiwa tarehe 12/08/2012. 

Kwa wale watakaochelewa kupata barua za maelekezo (Joining instruction) kutoka vyuoni wanatakiwa waripoti vyuoni katika tarehe iliyopangwa bila kukosa.
Wanafunzi wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:
1.Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA kulingana na kozi husika.


2. Ada kwa mwaka ni shilingi 200,000/=.  (Muhula wa kwanza shilingi  100,000/=  na muhula wa pili shilingi 100,000/=).


3.Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika na


4. Fedha  kwa matumizi binafsi.


Aidha, kila Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na  SI vinginevyo.



MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Saturday, July 28, 2012

BIBI ANAYEFUGA MISUKULE ACHOMEWA NYUMBA


Nyumba ilichomwa moto na kuvunjwa vunjwa.
Nyumba ya bibi Irene iliyo teketezwa leo kwa moto kwa tuuma za uchawi. Bibi huyo ambaye  amekuwa akisadikiwa kuwa na tabia ya kuwachukuwa watoto wa majirani zake kwa nguvu ya giza ameumbuka leo baada ya mtoto mmoja aliye potea kwa muda mrefu kwao na kutajwa kuwa alishafariki dunia kisha leo kijana huyo ana kwa ana akakutana na ndugu yake.

Mshangao ulitawala kwa ndugu huyo ambaye kwa ujasili alianza kumuuliza unaishi wapi na kijana yule ndo akamwelekeza kua nipo kwa bibi mmoja anaitwa bibi Irene na tunaishi na wenzangu wengine ambao nilikutana nao pale kwa bibi wakiongezeka siku baada ya siku.

Bibi huyo ambaye anatajwa kuwa mkali katika vitendo vya ushirikina, kakutwa na hilizi kibao na mara baada ya kupata kichapo ambacho hata ivyo akikuonyesha kumdhuru kwa licha ya kupigwa na mawe, bakora na hata vitu vingine vigumu vya hatari hakutokwa na damu, kuvimba nundu wala kuonyesha makovu ya majeraha mwilini mwake, aliwambia wananchi kua watoto wengine wapo ndani na alipo ambiwa awatoe nje alifanya mandingo yake na walio toka ni bata na kuku.

Kwa sasa bibi huyo anashikiliwa na jeshi la police jijini Mwanza kwaajili ya usalama wake.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, July 26, 2012

MTOTO WA AJABU MWENYE VICHWA VIWILI AZALIWA TANZANIA



Mwanamke mmoja amejifungua mtoto mwenye vichwa viwili katika hospitali teule ya Wilaya ya Bunda, mkoani Mara.

Mganga Mkuu wa hospitali ya DDH Bunda, Dk. Willam Krekamoo, amemtaja mwanamke huyo kuwa ni Sarah Abenenego (16), mkazi wa mtaa wa Chiringe, mjini Bunda.


Dk. Krekamoo alisema mwanamke huyo alipokelewa hosptilini hapo usiku wa kuamkia jana akiwa anaumwa uchungu, na kwamba muda mfupi alijifungua mtoto wa kike akiwa na vichwa viwili, midomo miwili, macho manne na masikio manne.

Alisema mtoto huyo alizaliwa akiwa pia na mikono miwili na miguu miwili na kwamba baada ya muda mfupi alipoteza maisha.

Alisema uchunguzi unaonyesha kuwa ujauzito ulikuwa wa miezi saba na huo ulikuwa ni uzazi wake wa kwanza na kuongeza kuwa hali ya mwanamke huyo inaendelea vizuri.
 
 
via: NIPASHE
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Ukiona dalili hizi 20 kwa mkeo, bora umuache tu!


TUKO kwenye Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, niwape pole wale waliojaaliwa kufunga na niwasihi wale wenye uwezo huo wafanye hivyo ili kumfurahisha Mwenyezi Mungu aliyetuumba.
Lakini nitoe angalizo kwa wale wenzangu na mimi wasiofunga, wajitahidi kutowaharibia swaumu wenzao. Wewe msichana uliyezoea kuvaa kimitego hebu funga breki kipindi hiki ili kutowatia majaribuni wenzako.
Aidha, kama wewe una mpenzi wako ambaye ni Muislam na wewe ni Mkristo, iheshimu imani yake na ikiwezekana mpe sapoti ili aweze kuvuka kipindi hiki salama.
Ndugu zangu, mmoja wa wadau wakubwa wa safu hii aliyejitambulisha kwa jina la Jafari wa Arusha, ameuliza swali ambalo nimeona ni vyema nikamjibu kupitia hapa ili na wengine waweze kufaidika
.
Yeye alitaka kujua jinsi anavyoweza kumbaini mwanamke asiye na mapenzi ya dhati kwa mumewe. Katika kujibu hili nimeorodhesha dalili 20 ambazo ukiziona kwa mpenzi wako ni bora ukamuacha tu.
Moja, Ni mwepesi wa kuanika udhaifu wako kwa watu wengine, ni mgumu wa kukusifia mbele za wenzake badala yake haoni noma kukuponda.
Mbili, anakuwa mgumu sana kukutambulisha kwa rafiki zake na ndugu.
Tatu, haonyeshi kubana matumizi kwa ajili ya maendeleo, kwake ni kufuja mali na anapokosa kupewa fedha ni mwepesi kulalamika.
Nne, anaahirisha mara kwa mara kukutana na wewe tena bila kukueleza sababu za msingi. 
Tano, anapokuwa anatoa maelezo ya mwanaume anayempenda kwenye maisha yake, sifa zake zinakuwa si zile ulizonazo wewe.
Sita, si mtu wa kucheka kwa furaha, hata kama ukimchekesha haoneshi furaha ya moyoni, tena mara nyingine anakuwa mkimya.
Saba, anajaribu kukuunganisha na wanawake wengine, haoni vibaya anaposikia unamfukuzia hata rafike yake badala yake anaweza hata kukutia moyo. Kwa kifupi hana wivu na wewe.
Nane, haumii pale inapotokea amekukosea, ni mwepesi wa kujitenga, kutozungumza na wewe na mwingi wa kukusukumia makosa hata kama yeye ndiye aliyekukosea.
Tisa, hataki kuambatana na wewe katika matembezi na ikitokea anakuwa mtu wa masharti sana. Ni rahisi kukuambia utangulie, yeye anakuja au mnaweza kutoka pamoja lakini yeye akawa anatembea mbali na wewe.
Kumi, siku zote ni mtu wa kupokea tu na si wa kutoa. Analazimisha kukumbatia mali zako na zake pia. Hupenda kufanya mambo yake kwa siri lakini hulazimisha kujua mipango yako.
Kumi na moja, hakumis hata unapokuwa mbali naye, kwa kifupi hathamini uwepo wako na anakuchukulia kama mtu wa akiba kwake.
Kumi na mbili, hakupi moyo pale unaposhindwa katika mambo unayopanga. Hachukui huzuni yako kama yake, hakufariji na hakusaidii pale ulipokwama.
Kumi na tatu, anayeweza kuchochea hisia mbaya kwa watu ili jamii ikuone mbaya, unayestahili kudharauliwa. Anakuwa mstari wa mbele kukuchafua katika maeneo ambayo anastahili kukusafisha.
Kumi na nne, hakupi kipaumbele katika maamuzi, anajiona yeye ndiye wa kwanza na wewe ni mtu wa kufuatia.
Kumi na tano, muwapo faragha anafanya bora liende, hakufikishi pale ambapo ulitarajia. Kwa kifupi anakuwa hana msisimko na wewe.
Kumi na sita, hakuhudumii tendo la ndoa mpaka siku amependa yeye. Ni mwingi wa kutoa sababu za kuchoka, kusingizia ugonjwa.
Kumi na saba, hazungumzii maendeleo yenu, ni mtu anayependa kufikiria maendeleo binafsi na ikiwezekana kuuza vilivyopo ili atimize malengo yake.
Kumi na nane, hataki kuambiwa ukweli na inapotokea akaambiwa huwa mkali na kuja juu mithili ya moto wa kifuu.
Kumi na tisa, hata akukosee vipi ni mgumu wa kuomba samahani na ikitokea umekosea wewe, ni mgumu kukusamehe kiasi kwamba kosa la mwaka jana anaweza kulikumbushia leo.
Ishirini, haoni hatari kukuambia; ‘Kama vipi tuachane, kwani nini....? Wapo wanaume wengi na wananitaka’.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

WEMA SEPETU AFANANISHA MAPENZI YAKE NA DIAMOND KAMA YA CRISS BOWN NA RIHANA



MSANII anayeongoza kwa ku-make headlines kwenye vyombo vya habari kila kukicha Wema Sepetu, amedai kuwa mahusiano yake yeye na mpenzi wake Nasseb Abdul ‘Diamond’, ni kama ya nyota wa marekani Rihanna na Chris Brown, huku akiamini kuwa kila kitu wanachokifanya kinakuwa kinafanana.

Wiki iliyopita Rihanna na Chris Brown, walioneka kwa nyakati tofauti huko St. Tropez, France wakila bata na kujiachia, ambapo hiyo pia imetokea kwa Wema na Diamond ambapo nao walionekana pamoja pande za Kigoma, Diamond alipoenda kwenye ziara ya Kigoma all stars inayoshirikisha wasanii wanaotokea mkoa wa kigoma.

Wema akiongea na DarTalk alidai kuwa hakuna mtu anayeweza kumfanya ashindwe kula bata na mpenzi wake huo kwani anaamini kwa kufanya hivyo ndiyo njia moja wapo ya kuwakata vilimi wale wanaozungumza mabaya juu ya mapenzi yao.

Hata hivyo mwandishi wa habari hizi, alitaka kujua mipango yao ya baadaye juu ya mapenzi yao ambapo alidai kuwa juu ya hilo hawezi kuzungumzia kwani ni miezi kadhaa walikuwa katika matatizo hivyo bado wanakula bata na watakapofikia maamuzi ya kuvishana tena pete watafanya hivyo.

“Mapenzi yetu hayana matatizo kwani wanadamu kutofautiana hiyo ni hali ya kawaida, hivyo sioni kama kuna haja ya kuongea sana, na kitendo cha sisi kuonekana pamoja sehemu za bata kuna watu inawauma na sisi hatujali kwani kila mtu ana maisha yake,” alisema Wema.

Mbali na ishu hiyo pia, mwandishi alitaka kujua tena itakuwaje kwa upande wa Jokate, alijibu kwa upande wake hamuoni kama ni mtu wa maana kwani mapenzi yake hakuna wa kukatisha ingawa anaamini Jokate ni mtoto mdogo sana kwake.

 
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

MH: MKAPA AMEASA JAMII ZA KIAFRIKA ZIHAMASISHWE KUHUSU TOHARA YA HIARI KWA WANAUME.


Mhe. Benjamin Mkapa akiwasili hotelini tarehe 21 Julai 2012, kuhudhuria Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI linalofanyika Mjini Washington D.C. Kushoto ni Balozi wa Tanzania Marekani Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar. 
Mhe. Benjamin Mkapa akisalimiana na Dr. Ellen Mkondya-Senkoro, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS mara baada ya kuwasili hotelini tarehe 21 Julai 2012, kuhudhuria Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI linalofanyika Mjini Washington D.C.
Mhe. Benjamin Mkapa akipewa taarifa na Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar, Balozi wa Tanzania nchini Marekani mara baada ya kuwasili Washington D.C kuhudhuria Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI kuanzia Julai 22-28, 2012. Wengine kwenye picha ni Dr. Ellen Mkondya-Senkoro, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS na picha nyingine ni Ms. Eileen A. Swai, Msaidizi wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa. 
Mhe. Benjamin Mkapa akiwasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Washington Convention Centre Julai 23, 2012 kuhudhuria Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI linalofanyika Mjini Washington D.C. 
Ma-Champion wa HIV Free-Generation Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe. Benjamin Mkapa na Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joachim Chisano wakifuatilia mojawapo ya mikutano ya Kongamano la UKIMWI kwenye Ukumbi wa Mikutano wa mjini Washington. Pembeni ni Mhe. Mwanaidi SinareMaajar, Balozi wa Tanzania Marekani na Dr. Ellen Senkoro wa Taasisi ya Benjamin Mkapa.
Pichani Juu na Chini ni Ma-Champion wa HIV Free-Generation Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe. Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joachim Chisano na Rais Mstaafu wa Zambia Mhe. Kenneth Kaunda wakijiandaa kabla ya mjadala kuanza kwenye mojawapo ya mikutano ya Kongamano la UKIMWI kwenye Ukumbi wa Mikutano wa mjini Washington D.C. 
Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe. Benjamin Mkapa akihitimisha mjadala kuhusu Mpango wa Tohara ya Hiari kwa Wanaume ili kupunguza maambukizi ya UKIMWI kwenye mojawapo ya mikutano ya Kongamano la UKIMWI kwenye Ukumbi wa Mikutano wa mjini Washington D.C.
Washington DC;Mhe. Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewaasa viongozi wa Nchi za Kiafrika kuchukua hatua ya kuhamasisha jamii za kiafrika kuhusu mpango wa tohara ya hiari kwa wanaume (Voluntary Medical Male Circumcision for HIV Prevention) kama mojawapo ya njia ya kupunguza maambukizi ya UKIMWI barani Afrika.
Mheshimiwa Mkapa aliyasema hayo alipokuwa anahitimisha mojawapo ya mijadala ya pembeni (Satelite Session) iliyokuwa inaendelea wakati wa Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI linaloendelea Mjini Washington DC, Marekani ambapo watu takribani 22,000 wanahudhuria. Mjadala huo uliovutia mamia ya wajumbe hususan kutoka Afrika kuhusu tohara ya hiari kwa wanaume, uliendeshwa na Bi. Brenda Wilson kutoka Afrika  Kusini ulielezea tafiti za kisayansi kuhusu mpango huo kama njia ya kupunguza maambukizi ya UKIMWI.
Rais Mkapa alisema mpango huu ni muhimu kutekelezwa na viongozi wa nchi za Kiafrika kwani imethibitishwa na tafiti zilizofanyika kwa Waafrika kwamba unapunguza maambukizi kwa asilimia 60, ambapo alisema si jambo dogo katika harakati za kutokomeza UKIMWI. Aliongeza kuwa ni mpango uliopendekezwa na sisi Waafrika wenyewe na ni wa hiari na hivyo hakuna atakayeshurutishwa.
 “Umebuniwa na nchi za magharibi, lakini umetafitiwa na kuthibishwa na sisi Waafrika wenyewe, hivyo ni mpango wetu huu” alisisitiza Rais Mkapa huku akishangiliwa kwa makofi na wajumbe wa mjadala huo.
Ili kutekeleza mpango huu wa tohara ya hiari kwa mafanikio, Mhe. Mkapa alielekeza mambo matatu. Kwanza nchi za kiafrika inabidi zitengeneze sera na mikakati madhubuti ya jinsi ya kukabiliana na janga hili la UKIMWI. Pili mipango na mikakati hiyo imilikiwe na wananchi wa nchi husika ili wao wenyewe wathibitishe ushiriki wao na sio kuonekana kama shuruti .Na mwisho mipango na sera za kukabiliana na UKIMWI itekelezwe kwenye mazingira ya ukweli na uwazi ili jamii za kiafrika ziweze kutambua athari za janga hili la UKIMWI.  Pia serikali nazo zitenge fedha za kusaidia katika mapambano haya na si kutegemea fedha za wafadhili tu.
“Umefika wakati sasa dunia nzima ielekeze nguvu zake kwenye kutokomeza ugonjwa huu hatari ambao unaua maelfu ya watu kila siku” Alisema Mhe. Mkapa na kuongeza kuwa mataifa mbalimbali duniani hutoa misaada haraka sana mara majanga ya dharura yanapotokea,  kama vile mafuriko, ajali n.k. Lakini janga la UKIMWI ni kama dharura  inayoendelea na sasa ni wakati muafaka dunia nzima itazame janga la UKIMWI kama dharura na inayoendelea.
Naye Mwenyekiti mwenza wa Mpango wa Tohara ya Hiari wa PEPFAR Dkt. Emmanuel Njeuhmeli alithibitisha tafiti hizo kwa kutoa mfano wa Zimbabwe ambapo maambukizi ya UKIMWI yanakadiriwa kupungua kwa asilimia 45 ndani ya kipindi cha miaka mitano ya utekelezaji wa mpango huo.
Wengine walioongea katika mjadala huo ni Angelo Kaggwa (Uganda), Mhe. Dkt. Speciosa Wandira (Uganda), Bi. Henrica Okondo (Kenya), Chifu Jonathan Mumena (Zambia), Mhe. Oburu Oginga (Kenya), Mhe. Dkt. Christine Ondoa (Uganda), na Mhe. Blessing Chebundo (Zimbabwe). Mjadala huo pia ulihudhuriwa na marais wastaafu wanaojishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi  ( wajulikanao kama Champions for AIDS Free Generation)Mhe. Joachim Chisano, Rais Mstaafu wa Msumbiji na Mhe. Kenneth Kaunda, Rais Mstaafu wa Zambia
Mhe. Mkapa amehudhuria Kongamano hili kubwa la UKIMWI kwa mwaliko wa taasisi ya Champions for HIV-Free Generation inayoongozwa na Rais Mstaafu wa Botswana Mhe. Festus Moghae, ambapo Mhe. Mkapa ni mmoja wa Ma-Champion nane wa taasisi hiyo.
Kongamano la XIX la Kimataifa la UKIMWI limeanza Washington DC tarehe 22 Julai hadi 28 Julai 2012 ambapo watu mashuhuri na viongozi mbalimbali wa Marekani wamehudhuria akiwemo Rais wa Marekani Mhe. Barack Obama.  


Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania Marekani
Julai 25, 2012
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

WAZIRI WA UCHUKUZI DR. HARRISON MWAKYEMBE AZINDUA HUDUMA MPYA ZA SHIRIKA LA NDEGE LA QATAR KUTOKA KIA.


Picha ya pamoja mara baada ya Shirika la ndege la serikali ya Qatar (Qatar airways) leo kuzindua  huduma ya safari zake za anga kutoka Kilimanjaro kuelekea sehemu mbalimbali za dunia kila siku na kufanya huduma za safari za anga kufikia zaidi miji 118.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika hilo Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo la ndege la Qatar zawadi ya picha yenye kivuli cha Mlima Kilimanjaro .
Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo akimpa Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison zawadi  ya yenye nembo ya ndege ya shirika hilo la Qatar.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo na wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani),mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA.
Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo na wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani),mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA.
Kutoka kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat,Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki wakijadiliana jambo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh lakizungumza machache na pia kumkaribisha mgeni rasmi na wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo mapema leo iliofanyika kwenye uwanja wa KIA.
 Wakuu wa uzinduzi wakipga makofi kwa pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison akipiga makofi wakati kikundi cha ngoma za asili kikitumbuiza,shoto kwake ni Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat mara baada ya kuwasili na ndege ya shirika hilo aina ya Ndege namba QR546,shoto kwake ni  Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh akimpokea Mgeni rasmi,Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe mara baada ya kuwasili KIA tayari kwa uzinduzi 
Mgeni rasmi,Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe akishuka kwenye ndege ya Qatar kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa ameambatana na Mkewe pamoja na  Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki.
 Ndege ya Qatar ikiwasili kabla ya kuzinduliwa rasmi KIA.
 Ikifanyiwa shower kwa mbwembwe zote.
 Wageni waalikwa mbali mbali wakisubiri kushuhudia uzinduzi huo.
Pichani kulia ni Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mhe.Novatus Makunga akizungumza jambo  na Mhariri Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima,Bw.Absalom Kibanda.
Baadhi ya Wanahabari Waandamizi wakiwa kwenye uzinduzi huo mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
 
 
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Wednesday, July 25, 2012

NIGERIA U20 YAWASILI KUIKABILI NGORONGORO HEROES.



 
Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana U20 ya Nigeria (Flying Eagles).

Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ya Nigeria (Flying Eagles) inatarajia kuwasili nchini leo (Julai 25 mwaka huu) saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir ikiwa na msafara wa watu 30 wakiwemo wachezaji 18.
Flying Eagles itapambana na Ngorongoro Heroes katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili itakayofanyika Jumapili (Julai 29 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Mechi hiyo ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za 18 za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 zitakazochezwa mwakani nchini Algeria itachezeshwa na waamuzi kutoka Kenya wakati Kamishna ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Flying Eagles inayofundishwa na kocha John Obuh, jana (Julai 24 mwaka huu) ilicheza mechi ya kirafiki na Rwanda (Young Amavubi) kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Nigeria ililala bao 1-0.
Msafara wa timu hiyo unaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFF), Chris Green. Baadhi ya wachezaji walioko katika kikosi cha Flying Eagles ni Chidi Osuchukwu, Alhaji Gero, Shehu Abdullahi, Aminu Umar, Aliyu Mohamed, Uche Agbo, Jonah Usman, Harrison Egbune, Hassan Abubakar na Yahya Adamu.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C itakuwa sh. 5,000. Kiingilio kwa VIP A itakuwa sh. 10,000.

NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME
Nusu fainali zote mbili za kuwania Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) mwaka 2012 zinachezwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Azam na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) zitacheza nusu fainali ya kwanza kuanzia saa 8 kamili mchana, na kufuatiwa na nusu fainali ya pili kati ya Yanga na APR ya Rwanda itakayoanza saa 10 kamili jioni.

via. dewjiblog.com
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

SAJUKI APATA GONJWA BAYA LAMSHAMBULIA UTI WA MGONGO


 
Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
 
Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa na mkewe Wastara.

PAMOJA na kwamba afya ya staa wa filamu Bongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ inaendelea vizuri, imegundulika kuwa ana ugonjwa mwingine tofauti na ule uliompeleka India kufanyiwa upasuaji,
Hivi karibuni, Sajuki alirejea kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya matibabu ambapo alionekana kuwa na mabadiliko makubwa kiafya jambo lililowapa matumaini mashabiki wake.

HABARI MEZANI
Akizungumza na waandishi wetu, juzi, Jumapili nyumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam, mke wa Sajuki, Wastara Juma alisema mumewe amegundulika kuwa na tatizo lingine walipokuwa nchini India kwa matibabu.
Alisema, hawakutaka kuweka hali hiyo mapema kwa Watanzania kwa kuhofia kusababisha simanzi, lakini sasa wanalazimika kufanya hivyo ili kuwafanya wajue kinachoendelea kwa staa wao.
“Kwa kweli mume wangu bado anaumwa na amegundulika kuwa na tatizo lingine ila tunamshukuru Mungu anaendelea vizuri,” alisema Wastara kwa huzuni nyingi.

NI UGONJWA GANI?
Kwa mujibu wa Wastara, walipokuwa India (katika Hospitali ya Apollo), Sajuki alifanyiwa vipimo mbalimbali ili kubaini matatizo yanayomsumbua ambapo aligundulika kuwa na tatizo kwenye uti wa mgongo na ngozi ya mwili mzima.
“Ana tatizo kwenye mfupa wa uti wa mgongo, lakini pia anasumbuliwa na tatizo jingine kwenye ngozi. Baada ya madaktari kugundua magonjwa hayo walimuanzishia dawa ya kutibu mgongo na mazoezi kwa ajili ya kumuweka sawa.
“Hizo dawa alianza kuzitumia tulipokuja huku, ambapo pia anaendelea na mazoezi. Tatizo lingine ni hilo la ngozi, ambalo pia anaendelea kutumia dawa,” alisema.

KWA NINI MGONGO?
Akifafanua kuhusu ugonjwa unaoshambulia sehemu ya mfupa wa uti wa mgongo, Wastara alisema madaktari walisema, tatizo hilo linasababishwa na kukaa kwa muda mrefu.
“Jambo hilo tulikubaliana nalo, kwa sababu ni kweli Sajuki huwa anakaa muda mrefu kwenye kompyuta kwa ajili ya kazi zake, lakini pia huwa anaendesha gari kwa muda mrefu. Tunaamini ndiyo chanzo cha ugonjwa huo kama madaktari walivyosema,” alisema na kuongeza:
“Lakini baada ya kupata dawa na ushauri  sasa anaendelea vizuri,  kwa sababu pia anafuata masharti aliyopewa vizuri. Huwa nahakikisha anapata muda mrefu wa kupumzika, hakai muda mwingi na haendeshi sana gari.
“Wamemwambia mambo mengi, hata kuinainama kila mara pia wamekataza. Kimsingi mwenzangu anahitaji uangalizi wa karibu sana. Hata hivyo anaweza kuendelea na filamu ila kwa kuzingatia na scene (onesho) yenyewe, ila kwa sasa anapumzika kwanza ili afya yake itengemae.”

KLINIKI KILA WIKI
Akiendelea kuzungumzia afya ya mumewe, Wastara alisema huwa wanalazimika kwenda Kliniki ya kila wiki katika hospitali moja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuangaliwa maendeleo yake.
Aidha, alisema kila wiki tatu huwa wanatuma vipimo nchini India katika Hospitali ya Apollo aliyokuwa akitibiwa kwa lengo la kuchunguza maendeleo yake.

KUHUSU UGONJWA WA NGOZI
Wastara alisema, tatizo la ngozi alilonalo mumewe bado hajaanza kutumia dozi yake kwa sababu hawajapata fedha ya kutuma India ili waweze kutumiwa dawa zenyewe.
“Tupo kwenye mchakato wa kutafuta hizo fedha, lakini hali bado ni ngumu na anatakiwa kuanza dozi mapema kama madaktari walivyoshauri,” alisema na kuongeza:
“Mwezi Desemba (mwaka huu) anatakiwa kurudi tena ili aangaliwe tena maendeleo yake kwa ujumla. Yote hiyo ni gharama kubwa sana, lakini tunaamini Mungu atatusimamia.”

GHARAMA ZAMTOA CHOZI WASTARA
Alisema kwa namna mahitaji yalivyo mengi na yanayohitaji fedha, wapo kwenye wakati mgumu kuweza kuyakabili.
“Kiukweli bado tunahitaji msaada wa Watanzania wenzetu. Tunashukuru kwa wale waliojaliwa kutusaidia awali hadi kufanikisha safari yetu ya matibabu India lakini watakaoguswa wanaweza kuendelea kutusaidia.
“Mpaka sasa Sajuki hajaanza dozi ya ugonjwa wa ngozi na zipo nyingine anazotakiwa kuzitumia, lakini hazipatikani hapa...ni mpaka India.”

VIDUME VYAMTOKEA WASTARA
 Akizungumzia suala la usumbufu wa kimapenzi, Wastara alisema ni jambo la kawaida na ni kweli kuna baadhi ya wanaume wanatumia udhaifu wa ugonjwa wa mumewe kumshawishi kimapenzi.
“Kutongozwa ni jambo la kawaida kwa mwanamke, lakini mimi kama Wastara msimamo wangu ni kumheshimu mume wangu. Siwezi kushawishika kwa namna yoyote, kwanza hata hamu yenyewe sina.
“Ninachokiangalia kwa sasa ni afya ya mume wangu. Najua nina wajibu mkubwa wa kuhakikisha namhudumia mume wangu kwa mapenzi yote. Akili yangu haipo kwenye mapenzi kabisa, hali aliyonayo mume wangu inaniumiza sana.
“Kamwe sitamsaliti Sajuki wangu. Wema wake kwangu wakati nikiwa kwenye matatizo siwezi kuulipia kwa kumdhalilisha kwa kutoka na mwanaume mwingine eti kwa sababu anaumwa. Anayewaza kufanya hivyo, akajaribu kwingine, siyo kwangu.”

KALAMU YA MHARIRI
Kwa matatizo aliyonayo Sajuki ni wazi yeye na familia yake bado wanahitaji msaada wa hali na mali ili kuweza kukidhi mahitaji ya matibabu yanayomkabili kwa sasa.
Kama Mtanzania mwenzake, guswa na moyo wa utoaji na Mungu wa Mbinguni atakuongezea katika mifuko yako.
Ikiwa umeguswa, tafadhali tuma mchango wako kwenye akaunti namba 050000003047 yenye jina la Wastara Juma Issa iliyopo katika Benki ya Biashara ya Akiba (ACB) au tumia Tigopesa kwenda namba 0713 666113 yenye jina Wastara Juma.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Madiwani 22 CCM Misungwi wajiandikisha kuhamia CHADEMA


Madiwani 22 wa CCM wa wilaya ya Misungwi (mkoa wa Mwanza) wamejiorodhesha na kutishia kutaka kuhamia CHADEMA kutokana mgogoro uliopo kati yao na viongozi wa CCM wilaya, Tanzania daima leo limeripoti. Uamuzi huo unatokana na Kamati ya siasa ya Mkoa na wilaya kumshinikiza Mkiti wa Halmashauri hiyo Mr Benard Policarp kujivua gamba kutokana na tuhuma za ufisadi wa fedha umma.

Hata hivyo, madiwani 22 kati ya 36 hawakubaliani na kamati hizo za siasa kwa madai kuwa uchunguzi wa kina ufanyike kwanza, ndipo uamuzi wa kumshinikiza M/kiti wao ajiuzulu ufuate, kwa kuwa hakuna uthibitisho uliopatikana dhidi yake hadi sasa. kwa mujibu wa taarifa hizo, ambazo zimethibitishwa na baadhi ya madiwani hao, tayari wamekwishajiorodhesha na kata wanazotoka na wamedhamiria kuipeleka majina yao makao makuu ya CCM.

Leo (jana) madiwani hao walitaka kuandamana kudai mali zao walizokuwa wakichangia Chama hicho lakini walikwama baada ya magari ya FFU kuzagaa kwa lengo la kupambana nao.

Mmoja wa madiwani hao (gazeti laficha jina) alisema muda wo wote watahamia Chadema kuanzia sasa.

Chanzo cha mtifuano
Ripoti ya CAG ilionesha kuwa halmashauri hiyo ilikuwa na ripoti mbaya ikionesha ufisadi wa Bil 5. Waziri mkuu Pinda aliagiza mkurugenzi ashushwe ( + jirani wa sengerema) wote wameshushwa vyeo. 

Baada ya hapo viongozi wa CCM (wilaya + mkoa) kupitia kamati za siasa wakahamisha bifu kwa m/kiti wa Halmashauri hiyo bila ushahidi wo wote, hata hivyo madiwani 22 kati ya 36 wakaamua kumkingia kifua ikibidi kwa gharama ya kuhama naye kwenda CHADEMA kutetea haki yao mpaka uchunguzi wa kina ufanyike kwanza.

My take;
Kama bifu linaanza mapema namna hii, kura ya maoni ya ndani ya CCM 2015 itakuwaje? 
Pili, hivi Chadema isingekuwa na nguvu wangeweza kuwa na ujasiri huo walio nao sasa?
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

BREAKING NYUZIII::Rais wa Ghana John Attah Mills afariki



John Atta Mills
 Rais wa Ghana John Atta Mills amefariki ghafla wakati akipata matibabu. Taarifa kutoka afisi ya rais 
zinasema kuwa alifariki ghafla baada ya kupelekwa hospitali siku ya Jumatatu usiku. 

Msaidizi wake pia amethibitisha kufariki kwa kiongozi huyo.
Kifo cha rais wa taifa la pili duniani kwa ukuzaji wa cocoa kimekuja wakati alikuwa anajiandaa kupogania tena urais.
Rais Attah Mills ambaye husafiri mara kwa mara kwenda ng'ambo kwa matibabu alifariki muda mfupi baada y kupelekwa katika hospitali moja mjini Accra , Ghana.
Ni hivi majuzi tu rais huyo alisafiri hadi Marekani kwa kile kilichosemekana kwa ni uchunguzi wa kawaida wa afya yake.
Kwa muujibu wa katiba ya Ghana, Makamu wa Rais John Dramani Mahama anatarajiwa kushikilia hatamu za uongozi hadi uchaguzi wa urais utakapofanywa.
Ghana ilikuwa inatarajiwa kwenda katika uchaguzi mkuu mwezi Disemba mwaka huu ambapo John Attah Mills alikuwa ametangaza nia yake ya kutetea uadhifa wake.
Wakati wa uongozi wake, uchumi wa Ghana uliimarika na demokrasia kupanuka zaidi.
" Ni kwa masikitiko makuu na kwa moyo mzito... Tunatangaza kifo cha ghafla cha rais wa jamhuri ya Ghana " taarifa iliyotumiwa shirika la Reuters kutoka ofisi ya rais ilisema.
Tarifa hiyo ilisema kuwa Rais Mills mwenye umri wa miaka 68 alifariki saa chache tu baada ya kupelekwa hospitali.
Hata hivyo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Lakini msaidizi wake mmoja ambaye hakutaka kutajwa, alisema kuwa Rais John Attah Millis alisikika siku ya Jumatatu akilalamika kwa anaumwa.
Hali yake ilizorota na hatimae kufariki mapema siku ya Jumanne.
Mills , anajulikana kwa kuanzisha uchimbaji wa mafuta nchi Ghana.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, July 24, 2012

KESI YA LULU MICHAEL YAPIGWA KALENDA TENA HADI AGOSTI 20



KESI ya msanii wa fani ya filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu Lulu, imeahirishwa hadi Agosti 20 mwaka huu, kutokana na Jaji anayeisikiliza, DK Fauz Twaib, kuwa na majukumu mengine.Akiahirisha kesi hiyo jana, Msajili wa Wilaya wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Amir Msumi, alisema Jaji DkTwaibu, anakabiliwa na majukumu mengine.

“Jaji Twaib ni Mwenyekiti wa Baraza la Kodi na pia ni Mwalimu wa Sheria katika Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hivyo kwa sasa anatekeleza majukumu mengine katika nafasi hizo.Kwa hiyo kesi hiyo inaahirishwa hadi Agosti 20, mwaka huu,” alisema Msumi.

Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake, Steven Kanumba, yanayodaiwa kufanyika April 7 mwaka huu nyumbani kwa marehemu Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.
Kabla ya kesi hiyo ya msingi haijaanza kusikilizwa, tayari imeshafikia ngazi ya Mahakama ya Rufani, baada ya kuibuka kwa utata wa umri wa mshtakiwa huyo.

Utata huo uliiobuka baada ya mawakili wanaomtetea msanii huyo, kuomba kesi isikilizwe katika Mahakama ya Watoto kwa madai kuwa mteja wao bado ni mtoto kwa kuwa ana umri wa miaka 17 na si 18 kama, inavyoonyesha katika hati ya mashtaka.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Baba amfumania Mama akizini na mwanaye; Awaua wote


Mkazi wa Kijiji cha Ng’hoboko, Stephano Mihulu (60) anadaiwa kumfumania mkewe na akifanya mapenzi na mtoto wao wa kumzaa na kuwaua kwa kuwakata mapanga.

Kamanda wa Polisi mkoani Simiyu, Salum Msangi aliwataja waliouawa kuwa ni Kundi Sita (40) ambaye ni mke wa mtuhumiwa na Boyayi Stephano (27) ambaye ni mtoto wake.

Akizungumza jana, kamanda alisema Mihulu alimkuta mkewe akifanya tendo la ndoa na mtoto wake ndipo alipoghadhabika na kuwashambulia kwa kuwakata mapanga na kisha kuwachinja shingoni.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda, tukio hilo ni la saa 7 usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Ng’hoboko wilaya ya Meatu mkoani hapa.

Baada ya kufanya mauaji hayo, inadaiwa Mihulu alitembea kwa miguu umbali wa kilometa 18 kutoka kijiji cha Ng’hoboko hadi makao makuu ya wilaya ya Meatu mjini Mwanhuzi, kwenda kujisalimisha kwenye kituo cha polisi cha wilaya hiyo.

Kamanda alisema mtuhumiwa alikabidhi silaha ambazo ni panga na fimbo alivyotumia kufanya mauaji hayo.

Alisema Mihulu alitembea kwa miguu kuanzia saa 7 usiku hadi asubuhi kwenda kituo cha polisi kwa madai kuwa hakutaka kuwasumbua polisi na kwamba yeye ndiye mhusika wa mauaji hayo.

Katika tukio lingine la kifo, kijijini Ipililo tarafa ya Mwagala wilayani Maswa, mkazi wa kijiji hicho Lugate Lazaro (45) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga mtoto wake Yohana Lazaro (9) mwanafunzi wa shule ya msingi ya Ipililo B na kusababisha kifo chake.

Inadaiwa kuwa mtoto Yohana alipigwa na baba yake kwa kuchelewa kurejea nyumbani baada ya kutoka shule kutokana na michezo njiani na wanafunzi wenzake. Kutokana na kipigo hicho, hali ya mtoto huyo ilikuwa mbaya mpaka saa 10 alfajiri ya kuamkia jana alipofariki.

Polisi inaendelea na uchunguzi wa matukio hayo na mara baada ya uchunguzi kukamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani kusomewa mashitaka yanayowakabili.

via HabariLeo
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Sunday, July 22, 2012

HAWA NDIO WASANII WALIOSOMA NA KWENDA SHULE PAMOJA


Ommy dimpoz mzee wa nai nai na baadae amesoma na super producer Mensen Selkta akiwa amemtangulia kidato kimoko pale Mbezi High school
Mesen Selekta yeye ni producer kutoka de fetality records lakini pia ni msanii ambae keshatoa pini kama kushoto kulia, na nyamnyamu.
Jaffarai amesoma na Jay moe kuanzia darasa la pili mpka la saba katika shule ya msingi Makumbusho iliyoka kijitonyama Dar-es-salaam

Juma Mchopanga a.k.a Jay moe
Mangwea mzee wa freestyle amesoma shule moja na Mez B, Noorah na Daki Master katika secondary ya Mazengo iliyoka Dodoma 
Mez B
Daki master
Noorah
Bob jr ambae pini lake la Nichumu limekamata nafasi ya kwanza ndani ya Top20 za Clouds wiki hii, amesoma na producer Nah Real ambae ameshatengenez pini kama Pea ya Nikki wa pili na zinginezo katika shule ya msingi Olympio.
Mzee wa Ndehe mtini Feruz amesoma na jamaa wa Born Cruz waliowahi kutoa ngoma iliyofanya vizuri iayoitwa kaka poa(wanamuita kaka poa huyu jamaa, wanamuita mtoto wa watu huyu jamaa) katika shule ya sekondari ya Makongo
Ben paul amesoma na Baghdadi Azania Secondary, lakini Ben Paul akiwa A level na Baghdadi akiwa A level
Baghdadi
Msanii Suma Lee amesoma na Producer Duke kutoka M lab katiska shule ya sekondari Sahare iliyoko Tanga huku Suma akiwa mbele ya Duke ki madarasa
Mh Temba kutoka kiumeni amesoma shule na Solo Thang, Rich one, Chidi Benz, Soggy Doggy, marehem Kanumba na Dazz baba katika shule ya sekondary ya Jitegemee iliyoko Temeke, Dar es salaam
Sollo Thang
Chidi benz
Marehem Kanumba

djfetty.blogspot.com
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.