Tuesday, July 31, 2012

ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013


WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013 

MAELEKEZO MUHIMU

Waombaji waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu katika mwaka wa masomo 2012/13 wanatakiwa kuripoti katika vyuo walivyopangiwa tarehe 12/08/2012. Kwa wale watakaochelewa kupata barua za maelekezo (Joining instruction) kutoka vyuoni wanatakiwa waripoti vyuoni katika tarehe iliyopangwa bila kukosa. Wanafunzi wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:

 1.Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA kulingana na kozi husika.

 2. Ada kwa mwaka ni shilingi 200,000/=. (Muhula wa kwanza shilingi 100,000/= na muhula wa pili shilingi 100,000/=). 

3.Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika . 

4. Fedha za matumizi binafsi. 

Aidha, kila Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SI vinginevyo.

BOFYA HAPA KUANGALIA ORODHA YA MAJINA

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment