Thursday, October 27, 2016

MATOKEO DARASA LA SABA 2016


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, October 20, 2016

Diamond Platnumz ft Rayvanny Salome ( Traditional Official Music video)


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Wednesday, September 7, 2016

MAFUTA YASHUKA BEI


Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji na Mafuta (Ewura), imetangaza kushuka bei ya mafuta ya aina zote kwa jumla na rejareja.


Bei hizo mpya ya mafuta zimeshuka katika mikoa yote isipokuwa Mkoa wa Tanga, hasa kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa.



Taarifa ya Ewura jana ilisema bei hizo zimeshuka ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, mwaka huu.



Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi, alisema katika toleo hilo, bei ya rejareja kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa imepungua kwa viwango tofauti.



Alisema kwa petroli imeshuka kwa Sh 65, dizeli Sh 63 na mafuta ya taa Sh 86.



“Bei ya jumla imepungua ambako kwa petroli ni Sh 65.31, dizeli Sh 63.39 na mafuta ya taa Sh 85.93,” alisema.



Ngamlagosi alisema kushuka kwa bei ya petroli katika soko la dunia na kupungua kwa gharama za usafarishaji/uletaji wa mafuta hayo nchini, ndizo sababu kuu zilizochangia kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la ndani nchini.



“Bei ya jumla na rejareja kwa petroli na dizeli katika Mkoa wa Tanga imeongezeka kidogo ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, 2016.



“Katika toleo hili, bei ya rejareja kwa petroli na dizeli imeongezeka kwa viwango ambavyo petroli ni Sh 50 na dizeli Sh 19. Kwa kulinganisha na matoleo haya mawili, bei ya jumla imeongezeka.



“Petroli Sh 49.61 kwa lita sawa na asilimia 2.80 na dizeli Sh 18.57 kwa lita sawa na asilimia 1.1.



“Ongezeko hili la bei limechangiwa kwa kiasi kikubwa na kupokea mafuta mapya (petroli na dizeli) ndani ya Agosti 2016, ambayo yalitarajiwa kupokewa Julai 2016 na pia kutokupokea mafuta mapya kutoka katika meli ya MT. Nevaska Lady ndani ya Agosti mwaka huu,” alisema Ngamlagosi.



Hata hivyo, alisema mamlaka hiyo inawakumbusha wananchi kwamba bei kikomo ya mafuta kwa eneo husika, pia inapatikana kupitia simu zao za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kufuata maelekezo.



Alisema huduma hiyo hutolewa bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi nchini.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

JPM atoa siku saba kwa wadaiwa sugu NHC


Siku chache baada ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) litoe nje vitu vya mmiliki wa Mbowe Hotels Limited, Freeman Mbowe kwa kile kilichoelezwa kushindwa kulipa kodi ya pango iliyofikia Sh bilioni 1.172 , Rais Dk. John Magufuli amempongeza Mkurugenzi wa Shirika hilo, Nehemia Mchechu kwa hatua hiyo.

Pamoja na hali hiyo ametoa siku saba kufukuzwa kwa wapangaji wote wa NHC watakaoshindwa kulipa kodi ya pango, zikiwemo wizara, taasisi za Serikali, watu binafsi na watumishi wa umma.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika mkutano wake na waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota, Rais Dk. Magufuli, alisema hatua zinazochukuliwa na Mchechu zitasaidia upatikanaji wa fedha za kuwekeza kwenye miradi mipya.


“Nakupongeza kwa hatua unazoendelea kuchukua. Wale wapangaji wote ni lazima walipe madeni yao, nimetoa maagizo leo (jana) wapangaji wote wa Serikali, Wizara ya Ujenzi, wizara gani kule ndani ya siku saba lazima wawe wameshalipa madeni yao,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:


“Wasipolipa endelea kuwatoa nje kama ulivyomtoa yule jamaa (Mbowe),” alisema na kusababisha watu kushangilia huku wakiangua vicheko.


“Endelea hivyo hivyo usiogope kumtoa nje mtu yeyote. Awe amepangishwa ni wa CCM mtoe nje, awe ni wa Ukawa mtoe nje, awe mtumishi wa Serikali mtoe nje, awe mtumishi huyo ni waziri mtoe nje, awe ni Rais mtoe nje,” alisema Rais Magufuli.


Alisema anashangaa kuona watumishi wa Serikali wakishindwa kulipa madeni ya kodi za pango wakati kila siku wanaomba safari za nje huku wakilipana posho.


“Ukipanga na ukashindwa kulipa kodi jiandae kuondoka. Nataka uendelee kuwatoa na nakueleza kweli Nehemia sitanii ‘take it from me and I am very serious’ (nisikilize mimi sifanyi mzaha) ” alisisitiza.


Alisema madeni hayo yangekusanywa yangelisaidia shirika hilo kuwekeza katika maeneo kama la Magomeni Kota ambalo limekaa kwa muda mrefu bila kuendelezwa.


“Inawezekana ungekuwa na hizo fedha ungeshajenga katika eneo hili kuliko kuanza kumtafuta mwekezaji kwa ujanjaujanja. Haiwezekani eneo kama hili (Magomeni Kota) la ekari 33 unazitoa hivi hivi na ni mali ya Serikali,


“Afadhali umtoe mke wako umpe mzaramo mtani wangu akae naye,” alisema Rais Magufuli huku wananchi wakiangua kicheko.

Alimsisitizia Mchechu kuharakisha kuzitoa wizara zinazodaiwa kwenye majengo yake ili ziharakishe kwenda kujenga Dodoma yaliko makao makuu ya nchi.


Awali Rais Magufuli, alisema alibaini ukweli kuhusu eneo hilo kwamba lilitaka kuuzwa kwa mwekezaji kinyemela na kuwaacha bila kitu wakazi hao.


VIA Mtanzania
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Darasa la saba waanza mitihani leo



WATAHINIWA 795,761 wanatarajia kufanya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) unaofanyika leo na kesho nchini kote.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk Charles Msonde alisema wanafunzi 372,883 ambao ni sawa na asilimia 46.86 ni wavulana na wasichana ni 422,878 ambao ni asilimia 53.14.


Mwaka 2015 watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 775,729 huku 763,602 ndio waliofanya mtihani huo na wanafunzi 518,034 walifaulu.


Dk Msonde alisema watahiniwa 765,097 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili na watahiniwa 30,664 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiingereza ambayo wamekuwa wakiitumia katika kujifunzia. Masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa.


Alisema watahiniwa wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani ni 95 wakiwemo wavulana 57 na wasichana 38 wakati wale wenye uoni hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 810 ambao kati yao wavulana ni 402 na wasichana ni 408.


“Maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika kiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, fomu maalum za kujibia mtihani na nyaraka zote muhimu katika halmashauri na manispaa zote nchini,” alisema Dk Msonde.


Aidha, Dk Msonde alitoa mwito kwa kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha taratibu za mitihani ya Taifa zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mazingira ya vituo vya mitihani yanakuwa salama, tulivu na kuzuia mianya ya udanganyifu.


“Wasimamizi wanatakiwa kusimamia kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu. Nawaaasa kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani Baraza litachukua hatua kali kwa yeyote yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya Taifa,” alieleza.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Ujenzi nyumba za Magomeni Kota kukamilika mwakani


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 06 Septemba, 2016 amewatembelea Wakazi wa Magomeni Kota Jijini Dar es Salaam ambao nyumba walizokuwa wakiishi katika eneo hilo zilivunjwa mwaka 2012 kwa makubaliano ya kujengwa nyumba za kisasa na kuwaahidi kuwa Serikali itaanza kujenga nyumba hizo katika kipindi cha Miezi miwili kuanzia sasa.


Rais Magufuli amesema ujenzi wa nyumba hizo utakamilika katika kipindi cha mwaka mmoja na baada ya hapo Wakazi wote 644 walioondolewa kupisha ujenzi wa nyumba za kisasa watapatiwa nyumba za kuishi na kwamba wataishi katika nyumba hizo kwa muda wa miaka mitano bila kulipa pango na baada ya muda huo kuisha wataandaliwa utaratibu wa kila mmoja kuuziwa nyumba anayoishi.


"Nakwenda kutoa pesa Mwezi huu, ili Mkandarasi atakayeteuliwa aanze kujenga nyumba za wakazi wote 644, wakati wanapojenga hayo majengo ya wakazi 644, ujenzi utaendelea pia katika maeneo mengine, ili kusudi kama yanajengwa maduka makubwa (Shopping Malls) au zinajengwa nyumba zingine za wananchi wanaohangaika nao tuwalete hapa.


"Nataka katika miji yetu ya Tanzania tuanze kupambana na makazi ya wananchi, tuwe tunajenga nyumba ili hata hawa masikini wa Tanzania waweze kufaidi kukaa kwenye ghorofa" Amesema Rais Magufuli.


Aidha, Dkt. Magufuli ameelezea kusikitishwa kwake na namna tatizo la wakazi wa Magomeni Kota lilivyoshughulikiwa na amewaahidi kuwa Serikali yake itahakikisha wananchi hao hawasumbuliwi tena.


Pamoja na hatua alizochukua kwa wakazi wa Magomeni Kota ambao nyaraka zimeonesha walikuwa wakiishi katika Nyumba za Shirika la Nyumba (NHC), Rais Magufuli ameagiza maeneo yote katika mikoa 20 hapa nchini yenye nyumba za kuishi za NHC kama lilivyo eneo hilo yatwaliwe na Serikali na kwamba Serikali itatoa maelekezo ya namna yatakavyotumika ama kuendelezwa.


Pamoja na kumpongeza kwa kazi nzuri anazofanya, Rais Magufuli amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Shirika na Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Neemia Mchechu Kyando kuwaondoa wapangaji ambao ni wadaiwa sugu wa pango zikiwemo Taasisi za Serikali ambazo amezipa siku saba kuwa zimelipa madeni yao.


"Wale wapangaji wote lazima walipe madeni yao, nimetoa maagizo leo, wapangaji wote wa Serikali, Wizara ya Ujenzi, Wizara gani kule... ndani ya siku saba lazima wawe wameshalipa madeni yao wasipolipa endelea kuwatoa nje.


"Endelea hivyo hivyo usiogope kumtoa nje mtu yeyote, awe amepangishwa ni wa CCM mtoe nje, awe wa UKAWA mtoe nje, awe Serikali mtoe nje, awe Waziri Mtoe nje, mpangaji huyo awe ni Rais mtoe nje, ni lazima upate pesa zitakazowezesha kuendesha Shirika la Nyumba la Taifa" Amesisistiza Rais Magufuli.


Wakati huo huo, Rais Magufuli amekagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa kwa chuo hicho alipokwenda kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho tarehe 02 Juni, 2016.


Jumla ya majengo 20 yenye ghorofa nne kila moja yanajengwa katika eneo hilo la mashariki mwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na yatakapokamilika tarehe 31 Desemba, 2016 yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanachuo 3,840 kati ya wanachuo 7,000 wanaolazimika kupanga vyumba vya kuishi mitaani kutokana na kukosa nafasi katika mabweni ya chuo yaliyopo.


Akizungumza na wafanyakazi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na Vijana walioajiriwa katika kazi za ujenzi wa majengo hayo Rais Magufuli amepongeza moyo wa uzalendo waliouonesha kwa kufanya kazi usiku na mchana na amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TBA Elius Mwakalinga kuendelea kuwatumia vijana hao katika miradi mingine ambayo Serikali itaitekeleza kwa kutumia TBA.

TBA ikitumia wataalamu na Vijana wa Kitanzania itatumia Shilingi Bilioni 10 kukamilisha ujenzi huo ikilinganishwa na endapo ingetumia Wakandarasi ambao walitaka kulipwa kati ya Shilingi Bilioni 50 na Bilioni 100.


Rais Magufuli ameutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuacha kuingia mikataba mingine na wafanyabiashara wanaotumia maeneo ya chuo hicho kujenga majengo ya kibiashara na badala yake amesema Serikali itaendelea kutafuta namna ya kulimaliza tatizo la mabweni kwa wanafunzi wa chuo hicho na vyuo vingine hapa nchini. 

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Friday, September 2, 2016

ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI (SECOND SELECTION) KWA MWAKA 2016


TAARIFA KWA UMMA


OR-TAMISEMI inatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya Pili (Second Selection) kwa mwaka 2016. Jumla ya wanafunzi 3,918 wakiwemo wasichana 2,413 na wavulana 1,505 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na wanafunzi ambao hawakuripoti awamu ya kwanza. 

Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 1,864 wakiwemo wasichana 1,099 na wavulana 765 sawa na asilimia 47.58 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 2,054 wakiwemo wasichana 1,314 na wavulana 740 sawa na asilimia 52.42 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara. 

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2015 wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili atakuwa amepoteza nafasi hii. 

Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2016 inapatikana kwenye tovuti ya OR-TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz

Imetolewa na Katibu Mkuu,
OR-TAMISEMI

Tumia link hii kupata matokeo :
>> Waliochaguliwa kidato cha tano awamu ya pili 2016


Link ya Matokeo ya awali : >> Waliochaguliwa kidato cha tano na vyuo vya ufundi 2016

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, August 16, 2016

Jibu la Mwimbaji Emmanuel Mbasha kuhusu kurudiana na Flora Mbasha



Kama utakuwa unakumbuka mnamo September 21,2015 moja ya stori kubwa iliyogusa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania ni ishu ya Hukumu ya Kesi ya Mwimbaji wa Gospel Tanzania, Emmanuel Mbasha ambapo alikuwa anakabiliwa na Keshi ya kumbaka shemeji yake na kesi imekuwa Mahakamani tangu 2014.

Wengi tunafahamu kwamba mwimbaji huyo aliachiwa huru baada ya Mahakama kumkuta hana hatia kwenye Kesi hiyo, sasa leo kajibu swali kuhusu kurudiana na mkewe Flora Mbasha na kuyaongea haya>>

‘Mimi kurudiana na Flora Mbasha ni ngumu kwasababu yeye ndio aliniacha mimi na yeye ndio aliandaa mazingira yake ya kuniacha mimi mpaka ikafika wakati Familia yangu, viongozi mbalimbali wa Dini wakawa wanamshauri lakini akutaka kurudiana na mimi kwahiyo naweza sema ni ngumu kurudiana na Flora’




MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

WANAFUNZI SHULE YA MSINGI MASANZA 1192 WASOMEA JUANI


Na, Shushu Joel,BUSEGA


Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Masanza katika Kijiji cha Mitindu Kata ya Kiloleli, Wilaya ya Busega, Mkoani Simiyu, wanalazimika kusomea kwenye mti kutokana na upungufu wa madarasa.

Aidha upungufu huo wa madarasa unawalazimu wanafunzi wengine kusomea juani katika madarasa mawili ambayo hayajapauliwa licha kufikia hatua hiyo miaka miwili iliyopita.

Shule hiyo ilianzishwa tangu mwaka 2006 lakini mpaka sasa haina hata nyumba moja ya walimu.

Wanafunzi wa shule ya msingi masanza wakiwa darasani

Akizungumza na NIPASHE mwalimu mkuu wa shule hiyo Vedasto Chibuga  amesema kutokana na uwepo wa changamoto hizo kunapelekea idadi kubwa ya wanafunzi kusomea kwenye darasa la vyumba viwili ambalo halijaezekwa, huku wengine wakisomea chini miti.
 
Chibuga aliongeza kuwa wanaosomea kwenye darasa hilo ni wanafunzi wa awali,darasa la sita na darasa la tatu, lakini ikifika majira ya saa tano asubuhi hulazimika kuthitisha vipindi kutokana na jua kali na kwenda kuwachanganya na wananfunzi madarasa mengine.

“Sera ya elimu inasema kuwa kila chumba wasome wanafunzi 45 lakini hapa kwangu mkondo mmoja wanasoma wanafunzi wasiopungua 100  kutokana na changamoto hizo za uhaba wa vyumba vya madara”.

Aidha Chibuka alisema kuwa serikali ndio ya kulaumiwa kwani wananchi wao walitimiza wajibu wao wa kuchangishana kwa ajili ya ujenzi wa boma hilo tangu mwaka 2013.

Kwa muji mwalimu mkuu huyo, hali inawafanya walimu kukata tamaa hali inayopelekea wanafunzi kutofanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa kutokana na mazingira magumu ya kufundishia.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi katika shule hiyo, Mikwanga Yona, alisema kuwa ni aibu kwa serikali kushindwa kupaua jengo hilo lililojengwa kwa nguvu za wananchi, na kwamba hali hiyo inaweza kufanya wananchi kukata tamaa kuchangia maendeleo katika maeneo yao kwa kukatishwa tamaa na serikali kwa kushindwa kuunga mkono jitihada zao.
Wanafunzi wakiwa darasani na mwalimu wao akiwafundisha

Ofisa Elimu Kata ya Kiloleli John Mayunga amethibitisha kuwepo kwa hali hiyo, na kwamba jambo hilo wamelifikisha katika kikao cha maendeleo ya kata ambacho mwenyekiti wake huwa diwani wa kata husika, na kuongeza kuwa pengine serikali inalifanyia hivyo kwa kuwa walishaliwasilisha katika ngazi ya halmashauri.


>>>>>>>>>>MWISHO>>>>>>
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Monday, August 15, 2016

Video ya Original Komedi alivyoingia ukumbini kwenye Harusi ya Masanja


Ni August 14, 2016 ambapo mchekeshaji kutoka kwenye kundi la Original Komedi, Emmanuel Mgaya aka Msanja Mkandamizaji aliziandika headlines baada ya kufunga ndoa na mchumba wake Monica katika kanisa la Mito ya Baraka Dar es Salaam.

Miongoni mwa walitoa burudani kwenye sherehe hiyo wakiwemo wachekeshaji wenzake kutoka kundi la Original Komedi, tazama video uone jinsi walivyoingia ukumbini.



Download


Download
Download
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

DOWNLOAD AUDIO JEFF UNTOUCHABLE FT. COYO_MC_S MAIH SACHO_BEKA TITTLE_C SIR MADINI -- EVERY DAY



Jeff-untouchable-ft-coyo-mc-s-maih-sacho-beka-tittle-c-sir-madini-every-day

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Friday, August 12, 2016

DULLY SYKES FT HARMONIZE - INDE (OFFICIAL VIDEO )




MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, August 11, 2016

Download Audio:II Barnaba-Lover-Boy MP3



Barnaba-Lover-Boy-King-Sele-Blog

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, August 9, 2016

Chege Ft. Diamond - Waache Waoane (BEAT) Instrumental



chege-ft-diamond-waache-waoane-beat-instrumental

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

DOWNLOAD AUDIO: G.FREE ----- MAPENZI MATAM TAM mp3



G.free-mapenzi-matam-tam

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Download Audio: Ruby- Je utanipenda? (Cover)


Download-audio-ruby-je-utanipenda-cover
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, August 4, 2016

Chege Feat. Diamond Platnumz | Waache Waoane | Official Video


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Download Chege Ft. Diamond Platnumz - Waache Waoane ( Official Audio)



https://my.notjustok.com/track/117005/chege-ft-diamond-platnumz-waache-waoane

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Monday, August 1, 2016

Diamond Platnumz ft P'square KIDOGO (Official Video)




MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Sunday, July 31, 2016

DOWNLOAD WANANDOTO KALA JEREMIAH ft MIRIAM CHIRWA (official video)




MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, July 28, 2016

Joh Makini ft Chidinma - Perfect Combo Official Music Video




MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, July 26, 2016

DOWNLOAD AUDIO KALA JEREMIAH ft MIRIAM CHIRWA WANANDOTO



https://my.notjustok.com/track/117035/kala-jeremiah-ft-miriam-chirwa-wanandoto

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Friday, July 15, 2016

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA(ACSEE) NA UALIMU (DSEE NA GATCE) 2016 YAMETANGAZWA


THE NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA 

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA 

 MATOKEO YA KIDATO CHA SITA(ACSEE) NA UALIMU (DSEE NA GATCE) 2016.


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, July 7, 2016

JPM ateua wakurugenzi halmashauri za majiji, wilaya


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo July 07 2016 amefanya uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji 5, Manispaa 21, Miji 22 na Wilaya (DC) 137 za Tanzania Bara.
Uteuzi huo umetangazwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe ambapo kati ya wakurugenzi wote 185 walioteuliwa, 65 wameteuliwa kutoka orodha ya wakurugenzi wa zamani na 120 ni wakurugenzi wapya.
Orodha ya wakurugenzi walioteuliwa kulingana na mikoa yao ni kama ifuatavyo;

ARUSHA
⦁ Arusha Jiji – Athumani Juma Kihamia

⦁ Arusha DC – Dkt. Wilson Mahera Charles

⦁ Karatu DC – Banda Kamwande Sonoko

⦁ Longido DC – Jumaa Mohamed Mhiwapijei

⦁ Meru DC – Kazeri Christopher Japhet

⦁ Monduli DC – Stephen Anderson Ulaya

⦁ Ngorongoro DC – Raphael John Siumbu


DAR ES SALAAM
⦁ Dar es salaam Jiji – Siporah Jonathan Liana

⦁ Kinondoni Manispaa – Aron Titus Kagurumjuli

⦁ Temeke Manispaa – Nassibu Bakari Mmbaga

⦁ Ilala Manispaa – Msongela Nitu Palela

⦁ Kigamboni Manispaa – Stephen Edward Katemba

⦁ Ubungo Manispaa – Kayombo Lipesi John


DODOMA
⦁ Dodoma Manispaa – Dkt. Leonard M. Masale

⦁ Kondoa DC – Kibasa Falesy Mohamed

⦁ Kondoa Mji – Khalifa Kondo Mponda

⦁ Mpwapwa DC – Mohamed Ahamed Maje

⦁ Kongwa DC – Mhandisi Ngusa Laurent Izengo

⦁ Chemba DC – Semistatus Hussein Mashimba

⦁ Chamwino DC – Athuman Hamis Masasi

⦁ Bahi DC – Rachel Marcel Chuwa


GEITA
⦁ Bukombe DC – Dionis Maternus Nyinga

⦁ Chato DC – Mhandisi Joel Bahahari

⦁ Geita DC – Ally Abdallah Kidwaka

⦁ Geita Mji – Modest J. Apolinaly

⦁ Mbogwe DC – Mahwago Elias Kayandabila

⦁ Nyang’wale DC – Carlos K. Gwamagobe


IRINGA
⦁ Iringa Manispaa – William Donald Mafwele

⦁ Mafinga Mji – Saada S. Mwaruka

⦁ Mufindi DC – Riziki Salas Shemdoe

⦁ Iringa DC – Robert Mgendi Magunya

⦁ Kilolo DC – Aloyce Kwezi


KAGERA
⦁ Biharamulo DC – Wende Israel Ng’ahala

⦁ Bukoba DC – Abdulaaziz Jaad Hussein

⦁ Bukoba Manispaa – Makonda Kelvin Stephen

⦁ Karagwe DC – Godwin Moses Kitonka

⦁ Kyerwa DC – Shedrack M. Mhagama

⦁ Missenyi DC – Limbe Berbad Maurice

⦁ Muleba DC – Emmanuel Shelembi Luponya

⦁ Ngara DC – Aidan John Bahama


KATAVI
⦁ Mlele DC – Alex Revocatus Kagunze
⦁ Mpimbwe DC – Erasto Nehemia Kiwale

⦁ Mpanda DC – Ngalinda Hawamu Ahmada

⦁ Mpanda Manispaa – Michael Francis Nzyungu

⦁ Nsimbo DC – Joachim Jimmy Nchunda


KIGOMA
⦁ Buhigwe DC – Anosta Lazaro Nyamoga

⦁ Kakonko DC – Lusubilo Joel Mwakabibi

⦁ Kasulu DC – Godfrey Msongwe Masekenya

⦁ Kasulu Mji – Fatina Hussein Laay

⦁ Kigoma Ujiji – Manispaa – Judethadeus Joseph Mboya

⦁ Kigoma DC – Hanji Yusuf Godigodi

⦁ Kibondo DC – Shelembi Felician Manolo

⦁ Uvinza DC – Weja Lutobola Ng’olo


KILIMANJARO
⦁ Manispaa ya Moshi – Michael Nelson Mwandezi

⦁ Hai DC – Yohana Elia Sintoo

⦁ Siha DC – Valerian Mwargwe Juwal

⦁ Same DC – Shija Anaclaire

⦁ Mwanga DC – Golden A. Mgonzo

⦁ Rombo DC – Magreth Longino John

⦁ Moshi DC – Emalieza Sekwao Chilemeji


LINDI
⦁ Kilwa DC – Bugingo I. N. Zabron

⦁ Lindi DC – Samwel Warioba Gunzar

⦁ Lindi Manispaa – Jomaary Mrisho Satura

⦁ Liwale DC – Justine Joseph Monko

⦁ Nachingwea DC – Bakari Mohamed Bakari

⦁ Ruangwa DC – Andrea Godfrey Chezue


MANYARA
⦁ Babati Mji – Fortunatus Hilario Fwema

⦁ Hanang DC – Bryceson Paul Kibasa

⦁ Mbulu DC – Festi Fungameza Fwema

⦁ Mbulu Mji – Anna Philip Mbogo

⦁ Simanjiro DC – Yefred Edson Myezi

⦁ Kiteto DC – Tamim Kambona

⦁ Babati DC – Hamis Iddi Malinga


MARA
⦁ Manispaa ya Musoma – Fidelica Gabriel Myovela

⦁ Bunda DC – Amos Jeremiah Kusaja

⦁ Bunda Mji – Janeth Peter Mayanja

⦁ Butiama DC – Solomon Kamlule Ngiliule

⦁ Musoma DC – Flora Rajab Yongolo

⦁ Serengeti DC – Juma Hamsini Seph

⦁ Rorya DC – Charles Kitanuru Chacha

⦁ Tarime DC – Apoo Castro Tindwa

⦁ Tarime Mji – Hidaya Adam Usanga


MBEYA
⦁ Busokelo DC – Eston Paul Ngilangwa

⦁ Chunya DC – Sofia Kumbuli

⦁ Kyela DC – Mussa Joseph Mgata

⦁ Mbarali DC – Kivuma Hamis Msangi

⦁ Mbeya DC – Ameichiory Biyengo Josephat

⦁ Mbeya Jiji – Zacharia Nachoa Ntandu

⦁ Rungwe DC – Loema Isaya Peter


SONGWE
⦁ Momba DC – Adrian Jovin Jungu

⦁ Tunduma Mji – Valery Alberth Kwemba

⦁ Mbozi DC – Edna Amulike Mwaigomole

⦁ Ileje DC – Haji Mussa Mnasi

⦁ Songwe DC – Elias Philemon Nawela


MOROGORO
⦁ Gairo DC – Agnes Martin Mkandya

⦁ Kilombero DC – Dennis Lazaro Londo

⦁ Ifakara Mji – Francis Kumba Ndulane

⦁ Kilosa DC – Kessy Juma Mkambala

⦁ Morogoro DC – Sudi Mussa Mpili

⦁ Morogoro Manispaa – John Kulwa Magalula

⦁ Mvomero DC – Florent Laurent Kyombo

⦁ Ulanga DC – Audax Christian Rukonge

⦁ Malinyi DC – Marcelin Rafael Ndimbwa


MTWARA
⦁ Mtwara DC – Omari Juma Kipanga

⦁ Mtwara Mikindani Manispaa – Beatrice Dominic Kwai

⦁ Masasi Mji – Gimbana Emmanuel Ntayo

⦁ Masasi DC – Mkwazu M. Changwa

⦁ Nanyumbu DC – Hamis Hassan Dambaya

⦁ Newala DC – Mussa Mohamed Chimae

⦁ Newala Mji – Andrew Frank Mgaya

⦁ Tandahimba DC – Said Ally Msomoka

⦁ Nanyamba Mji – Oscar Anatory Ng’itu


MWANZA
⦁ Mwanza Jiji – Kiomoni Kibamba Kiburwa

⦁ Ilemela Manispaa – John Paul Wanga

⦁ Kwimba DC – Pendo Anangisye Malabeja

⦁ Magu DC – Lutengano George Mwalwiba

⦁ Misungwi DC – Eliud Leonard Mwaiteleke

⦁ Ukerewe DC – Tumaini Sekwa Shija

⦁ Buchosa DC – Crispian Methew Luanda

⦁ Sengerema DC – Magesa M. Boniphace


NJOMBE
⦁ Njombe Mji – Iluminata Leonald Mwenda

⦁ Makambako Mji – Paul Sostenes Malala

⦁ Makete DC – Francis Emmanuel Namaumbo

⦁ Njombe DC – Monica Peter Kwiluhya

⦁ Ludewa DC – Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija

⦁ Wanging’ombe DC – Amina Mohamed Kiwanuka


PWANI
⦁ Bagamoyo DC – Azimina A. Mbilinyi

⦁ Chalinze DC – Edes Philip Lukoa

⦁ Kibaha DC – Tatu Seleman Kikwete

⦁ Kibaha Mji – Jenifer Christian Omolo

⦁ Kisarawe DC – Mussa L. Gama

⦁ Mafia DC – Erick Mapunda

⦁ Mkuranga DC – Mshamu Ally Munde

⦁ Kibiti DC – Alvera Kigongo Ndabagoye

⦁ Rufiji DC – Salum Rashid Salum


RUKWA
⦁ Kalambo DC – Simon Ngagani Lyamubo

⦁ Sumbawanga DC – Nyangi John Msemakweli

⦁ Sumbawanga Manispaa – Hamid Ahmed Njovu

⦁ Nkasi DC – Julius M. Kaondo


RUVUMA
⦁ Mbinga DC – Gumbo Samanditu Gumbo

⦁ Mbinga Mji – Robert Kadaso Mageni

⦁ Namtumbo DC – Christopher Michael Kilungu

⦁ Nyasa DC – Oscar Albano Mbuzi

⦁ Songea DC – Simon Michael Bulenganija

⦁ Madaba DC – Shafi Kassim Mpenda

⦁ Tunduru DC – Abdallah Hussein Mussa

⦁ Songea Manispaa – Tina Emelye Sekambo


SHINYANGA
⦁ Kishapu DC – Stephen Murimi Magoiga

⦁ Msalala DC – Berege Sales Simon

⦁ Shinyanga DC – Mark Emmanuel Malembeka

⦁ Kahama Mji – Anderson David Msumba

⦁ Shinyanga Manispaa – Lewis Kweyemba Kalinjuna

⦁ Ushetu DC – Michael Augustino Matomola


SIMIYU
⦁ Bariadi DC – Abdallah Mohamed Malela

⦁ Bariadi Mji – Melkizedek Oscar Humbe

⦁ Itilima DC – Mariano Manyingu

⦁ Maswa DC – Fredrick Damas Sagamiko

⦁ Busega DC – Anderson Njiginya

⦁ Meatu DC – Said F. Manoza


SINGIDA
⦁ Ikungi DC – Rustika William Turuka

⦁ Iramba DC – Linno Pius Mwageni

⦁ Mkalama DC – Martin Msuha Mtanda

⦁ Manyoni DC – Charles Edward Fussi

⦁ Itigi DC – Luhende Pius Gerald

⦁ Singida DC – Rashid Mohamed Mandoa

⦁ Singida Manispaa – Kizito L. Brava


TABORA
⦁ Igunga DC – Revocatus Lubigili Kuuli

⦁ Kaliua DC – John Marco Pima

⦁ Nzega DC – Jacob James Mtalitinya

⦁ Nzega Mji – Phillimon Mwita Magesa

⦁ Sikonge DC – Simon Saulo Ngatunga

⦁ Tabora Manispaa – Bosco Addo Ndunguru

⦁ Urambo DC – Magreth Nakainga

⦁ Tabora -Uyui – Hadija Maulid Makuani


TANGA
⦁ Tanga Jiji – Daudi R. Mayeji

⦁ Korogwe DC – George John Nyaronga

⦁ Korogwe Mji – Jumanne Kiangoshauri

⦁ Muheza DC – Luiza Osmin Mlelwa

⦁ Handeni Mji – Keneth K. Haule

⦁ Handeni DC – William Methew Mafukwe

⦁ Pangani DC – Sabas Damian Chambasi

⦁ Mkinga DC – Mkumbo Emmanuel Barnabas

⦁ Bumbuli DC – Peter Isaiah Nyalali

⦁ Kilindi DC – Clemence Andagile Mwakasenda

⦁ Lushoto DC – Kazimbaya Makwega Adeladius


Wakurugenzi wote walioteuliwa wametakiwa kufika Ikulu Jijini Dar es salaam siku ya Jumanne July 12 2016 saa tatu asubuhi kwa ajili ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, July 5, 2016

Confirmed:Sikukuu ya Eid Jumatano July 06.........


Taarifa ambayo imetolewa na Mufti Mkuu wa Tanzania Zubeir Bin Ally muda mfupi uliopita ni uthibitisho wa sikukuu ya Eid ul Fitr ambapo Waislam wote walikua wakisubiri kuandama kwa mwezi, Kwenye taarifa yake Muft Zubeir amesema Mwezi huo umeonekana sehemu mbalimbali za nchi yetu ya Tanzania.



Amewaomba pia waislam kujitokeza kwenye misikiti mbalimbali kwa ajili ya ibada ya Eid ul Fitr.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

DOWNLOAD VIDEO: HARMONIZE - MATATIZO (Official Video )


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Maneno Ya 20% Baada ya Kurudi Tena Ndani ya ‘Kombinenga’


Mkali wa Bongo Fleva, 20%  siku ya jana alisaini mkataba chini la Label ya Kombinenga inayomilikiwa na mtayarishaji wa muziki Man Water kutoka katika studio za Combination Sound, 20% aliweza kusaini mkataba wa miaka mitano kufanya kazi chini ya Label hiyo, ambayo itakuwa ikimsimamia katika kazi zake.

“Kwa upande wake 20% alisema kuwa sasa amerudi rasmi kuja kuwachinja tena na kusema amerudisha sauti ya gharama kwa jamii na mashabiki wake, sauti yenye kuburudisha, sauti yenye kufunza na kutoa burudani kwa watu wake” alisema 20%
Kwa upande wake Man Water amedai kuwa sasa 20% amerudi rasmi mwaka 2016 chini ya Kombinenga na kuwataka mashabiki wake mkao wa kula kupokea kazi nzuri zenye ujumbe mzito na wakusisimua kutoka kwa msani huyo

“Twenty Percent is back. …2016

Kaa mkao wakula ngoma zenye jumbe nzito na za kusisimua…kila kitu kiko sawa sasa…new page” aliandika Man Water.

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Mtoto wa Idi Amin akosoa sherehe za Entebbe


 
Bw Netanyahu amehimiza kuimarishwa kwa uhusiano baina ya Afrika na Isra


Mwanawe aliyekuwa kiongozi wa Uganda Idi Amin Dada amepinga sherehe za maadhimisho ya miaka 40 tangu kutekelezwa kwa operesheni ya makomando wa Israel uwanja wa ndege wa Entebbe.

Makomando hao walifika kuwaokoa mateka Wayahudi waliokuwa wanazuiliwa na wanamgambo wa Palestina waliokuwa wameteka ndege ya shirika la Air France.

Bw Hussein Lumumba Amin amesema ni makosa kwa serikali ya Uganda na nchi jirani za Afrika kushiriki sherehe hizo pamoja na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.

Kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari, Bw Amin, anasema baada ya kutekelezwa kwa shambulio hilo 1976, Umoja wa Afrika ulilaani kitendo hicho.

Aidha, amesema si haki kwa babake, Idi Amin, kuoneshwa kama mhusika katika utekaji nyara wa ndege hiyo.

Anasema babake alikuwa anatekeleza wajibu wa mpatanishi na kwamba hata aliwafaa mateka waliokuwa wanazuiliwa.

Aidha, alikuwa anatetea haki za Wapalestina.
 
Mnara wa walinzi na waelekezi wa ndege uwanja wa Entebbe
“Kama Amin angekuwa anapendelea upande mmoja wakati huo, mateka hao huenda labda wangezuiliwa gereza kuu la Luzira au afisi iliyoogopwa sana ya makachero wa serikali ambapo hawangeweza kutoroka,” Bw Lumumba anasema.

Anasema Bw Amin aliwaokoa mateka hao kwa kuhakikisha ndege hiyo, baada ya kutekwa, iliweza kutua Libya na kuongezwa mafuta kabla ya kuendelea na safari hadi Uganda.
  • Netanyahu: Israeli inataka uhusiano na Afrika
Kabla ya hapo, anasema ndege hiyo ilikuwa inazunguka angani bahari ya Mediterranean na haikuwa na mafuta ya kutosha kufika Uganda.

Kiongozi huyo wa zamani, alimsihi kiongozi wa Libya wakati huo, Kanali Muamar Gaddafi, aruhusu ndege hiyo kuongezwa mafuta.

Wakati huo, Bw Lumumba anasema kwenye taarifa yake, serikali za nchi za Kiarabu zilikuwa zimekataa ndege hiyo itue nchi zao.

“Kuingilia kati kwake huenda kuliokoa mateka wote na wahudumu wa ndege kutoka kwa mkasa wa kuanguka baharini,” anasema Bw Lumumba.

Anaeleza kuwa uwanja wa ndege, Idi Amin, angewazuru mateka na alihakikisha walipewa chakula na malazi mema.
Mateka takriban 100 waliokolewa

“Habari zinazoenezwa kuhusu kisa hicho cha Entebbe zinafanya ionekane kana kwamba Amin mwenyewe alikuwa mtekaji nyara. Makusudi, wamekaa kimya kuhusu usaidizi wowote ambao huenda (Amin) alitoa kwa mateka hao wa Israeli wakati huo,” anasema Lumumba.

Nduguye Bw Netanyahu, Luteni Kanali Yonatan "Yoni" Netanyahu aliyeongoza makomando 29 wa Israeli ndiye pekee kutoka Israel aliyeuawa wakati wa operesheni hiyo.

Wanajeshi 20 wa Uganda waliuawa.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Uganda na Tanzania wajadili bomba la mafuta




 

Baada ya tangazo la marais wa Uganda na Tanzania sasa maafisa wameanza vikao vya utekelezaji mradi wa bomba la mafuta
Uganda na Tanzania zimeanza upya mazungumzo utekelezaji wa makubaliano baina ya viongozi wa mataifa hayo mawili kupitisha mradi wa bomba la mafuta kupitia Hoima Tanga badala ya Hoima - Lamu Kenya.
Ujumbe wa Uganda unaongozwa na waziri wa kawi Irene Muloni huku Tanzania wakiongozwa na Prof Sospeter Muhongo.


Wengine wanaohudhuria mazungumzo hayo huko Hoima ni wawakilishi wa kampuni ya kuchimba mafuta yenye asili yake nchini Uingereza Tullow, mjumbe wa kampuni ya kuuza mafuta ya Total yenye asili yake nchini Ufaransa na kisha
kampuni ya kichina ya CNOOC inayotekeleza mradi wenyewe wa kuchimba na kuweka bomba la mafuta Kuanzia Hoima hadi bandari ya Tanga.

 
Bomba hilo la mafuta litakwenda kilomita 1,400km kuanzia Hoima, hadi kwenye bandari ya Tanga.
Mada kuu ya mazungumzo hayo huko Hoima ni utekelezaji wa miradi kwa kuzungumzia hali halisia.
Kwa mfano maswala ya ardhi itakayotumika kwa mradi huo itamilikiwa na nani na itatwaliwa vipi kutoka kwa uma, pia kuna swala la ukubwa wa ardhi yenyewe, wanadani wanasema kuwa mradi huo ulikuwa umependekezwa utekelezwe kwenye ardhi ya takriban mita 20 ,sasa hilo linaonekana kupata upinzani na hivyo kunahoja mbadala ukubwa huo upunguzwe katika mradi huo utakaotekelezwa kwa umbali wa kilomita 1403
Uganda yavunja mkataba na kampuni ya Urusi
Uganda kupitishia mafuta yake Tanzania

Kenya iliamua kujenga bomba la mafuta kutoka Turkana hadi Lamu

Aidha swala la ujenzi wa mtambo wa kusafishia mafuta wenye thamani ya dola bilioni 2.5 uliopata pigo baada ya Serikali ya Uganda kukatiza mazungumzo na kampuni moja ya Urusi pia utajadiliwa.
Uganda imeanza mazungumzo mbadala na kampuni moja ya ujenzi kutoka Korea Kusini.
Uganda ilikuwa imependekeza kujenga bomba la mafuta safi mkabala na bomba la mafuta la Hoima -Tanga.
Mkurugenzi wa usafirishaji wa mafuta nchini Uganda Robert Kasande akizungumza na wanahabari alisema kuwa tayari wajumbe wamekubaliana mambo mengi kati ya maswala makuu yaliyohitaji kujadiliwa.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Rais Magufuli atengua na kufanya uteuzi mwingine leo July 05 2016





Taarifa niliyoipokea kutokea ikulu inasema kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act) Sura 1, leo tarehe 5 Julai, 2016 ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB Prof. William Lyakurwa.

Kufuatia hatua hiyo, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (2) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act) Sura 257, Rais Magufuli amemteua Prof. Palamagamba J. A. M. Kabudi kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kufuatia mabadiliko hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act) Sura 1, ametengua uteuzi wa Wajumbe Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB. 

Aidha, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (1) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act, Sura 257) Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango ameteua wajumbe wapya wa Bodi wafuatao kwa kipindi cha miaka mitatu

⦁ Brig. Gen (Rtd) Mabula Mashauri
⦁ Dkt. Razack B. Lokina

⦁ Bi. Rose Aiko

⦁ Prof. Joseph Bwechweshaija

⦁ Bw. Said Seif Mzee

⦁ Dkt. Arnold M. Kihaule

⦁ Bw. Maduka Paul Kessy

⦁ Bw. Charles Singili

Uteuzi wa Mwenyekiti na Wajumbe wapya wa Bodi unaanza tarehe leo July 5 2016.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Sababu za Diamond kuhusu picha ya Alikiba kwenye ofisi za WCB….





Perfect Crispin ni mtangazaji wa Clouds FM ambaye hapa anatusogezea stori zilizochukua headlines kutoka kwenye tasnia ya Bongo Fleva, ambapo leo July 5,2016 ametusogezea hizi stori tatu ikiwemo ya Diamond Platnumz kuzungumzia picha ya Alikiba iliyowekwa katika ofisi za WCB.

‘Unajua ofisi ya WCB sio ya Diamond Platnumz sio ya Harmonize sio ofisi ya wakina Tale ni ofisi ya Muziki wa Bongo Fleva ambayo imekuwepo kuleta maendeleo kwenye muziki wetu, kwahiyo nimeamua kuweka zile  picha za mastaa ikiwemo ya Alikiba  kwamba ndio wasanii wenye mchango kwenye muziki wetu’-Diamond Platnumz
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Baada ya ajali mfululizo zilizohusisha mabasi, polisi wamekuja na hii taarifa



Ni takribani wiki moja yametokea matukio makubwa matatu ya ajali za barabarani mfululizo ambayo yamehusisha mabasi yanayofanya safari zake mikoani, taarifa ya polisi imesema ajali hizo zimesababisha jumla ya vifo vya watu 46 na majeruhi 73.

Matukio hayo yanahusisha ajali iliyotokea June 28 2016 Misungwi Mwanza  ambapo basi la kampuni ya Super Samy likitokea Shinyanga kwenda Mwanza lilipata ajali kwa kuacha njia na kupinduka hivyo kusababisha vifo wa watu 5 na majeruhi 13.

Tukio lingine ni mnamo July 01 2016  VETA Dakawa katika barabara ya Morogoro/Dodoma malori mawili yaligongana na kuwaka moto na kusababisha vifo vya watu 5 na  na baadae katika eneo hilohilo siku July 02 2016 usiku gari la kampuni ya OTA lilipata ajali kwa kuyagonga mabaki ya malori yaliyopata ajali na kubaki eneo la tukio na kusababisha vifo  vya watu 6 na majeruhi 6

Halikadhalika mnamo July 04 2016 maeneo ya Maweni-Kintiku Singida mabasi mawili ya kampuni ya City Boys yaligongana na kusababisha vifo wa 30 na majeruhi 54 ambapo hadi leo wamebaki majeruhi 33 wakiendelea na matibabu. Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi, kikosi cha usalama barabarani, Mohamed Mpinga amesema
>>>’kwa ajali iliyotokea Maweni Singida siyo ajali ya kawaida bali ni tukio la kufanya mauaji bila kukusudia, hivyo polisi imedhamiria kuwafikisha mahakamani madereva waliohusika na ajali hiyo kwa mashtaka ya mauaji bila kukusudia kutokana na taarifa za awali za chanzo cha kutokea kwa ajali hiyo kwamba madereva wa mabasi hayo walikuwa wakifanya mzaha wakati wa kupishana.

>>>Aidha tumewasiliana na wenzetu wa SUMATRA, kampuni ya mabasi ya City Boys na makampuni mengine yaliyohusika katika ajali yafungiwe kutoa huduma za usafirishaji katika njia zote hapa nchini
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.