Tuesday, July 5, 2016

Maneno Ya 20% Baada ya Kurudi Tena Ndani ya ‘Kombinenga’


Mkali wa Bongo Fleva, 20%  siku ya jana alisaini mkataba chini la Label ya Kombinenga inayomilikiwa na mtayarishaji wa muziki Man Water kutoka katika studio za Combination Sound, 20% aliweza kusaini mkataba wa miaka mitano kufanya kazi chini ya Label hiyo, ambayo itakuwa ikimsimamia katika kazi zake.

“Kwa upande wake 20% alisema kuwa sasa amerudi rasmi kuja kuwachinja tena na kusema amerudisha sauti ya gharama kwa jamii na mashabiki wake, sauti yenye kuburudisha, sauti yenye kufunza na kutoa burudani kwa watu wake” alisema 20%
Kwa upande wake Man Water amedai kuwa sasa 20% amerudi rasmi mwaka 2016 chini ya Kombinenga na kuwataka mashabiki wake mkao wa kula kupokea kazi nzuri zenye ujumbe mzito na wakusisimua kutoka kwa msani huyo

“Twenty Percent is back. …2016

Kaa mkao wakula ngoma zenye jumbe nzito na za kusisimua…kila kitu kiko sawa sasa…new page” aliandika Man Water.

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment