Friday, May 17, 2013

Movie aliyoigiza mama Kanumba kutoka leo


mama-steven-kanumba-without-a-daddy-movie-poster-pichaFilamu inayoitwa “Without Daddy” ambayo imekua ikipikwa kwa muda mrefu sasa, inatoka leo. Filamu hiyo ina upekee fulani sababu itakua ni filamu ya kwanza ambayo Mama yake marehemu Steven kanumba ameigiza.

Watu wengi wana hamu kuangalia movie hii kwa sababu mbalimbali. Wengine wanataka wapime kipaji chake, wengine ku-show support kwa mama wa msanii kipenzi chao wanayem-miss… Steven Kanumba.

Utabiri wangu ni kwamba mama atakuwa mkali kwenye kuigiza. Sababu? Kwanza yuko comfortable mbele ya kamera kwa interview mbalimbali nilizomuona. Pili asilimia kubwa ya kina mama wana uwezo wa kuigiza sababu sehemu kubwa ya maisha yao ni kuigiza mbele ya watoto, kama vile wanapotumia ucheshi kuficha ugumu au ukubwa wa tatizo ili watoto wasi-panic. Tatu yeye ndiye aliyezaa kipaji, Steven Kanumba, hivyo kuna uwezekano mkubwa personality na ucheshi aliokua nao hayati Kanumba kwa kiasi fulani aliridhi kutoka kwa mama yake

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment