Tuesday, January 22, 2013

SAFARI YA IRINE UWOYA NCHINI UINGEREZA YASHINDWA KUZAA MATUNDA


Actress mwenye makeke mengi na vituko vya kila aina Irine Uwoya amesema kuwa safari yake aliyoifanya nchini Uingereza mwishoni mwa mwaka jana bado haijazaa matunda ingawa bado wapo katika mazungumzo na wahusika, ila kwa sasa kitu wanachokizungumzia ni namna watakavyoandika story ingawa hakuweka wazi ni story ya namna gani wakati mtandao wa Dartalk ulipomuuliza.Uwoya amesema kuwa watu hao wameonyesha nia ya kufanya nae kazi ingawa malipo ya mzigo huo bado hayajawekwa wazi na lini watafanya hiyo kazi rasmi. uwoya pia alikataa kuwataja hao watu anaotaka kufanya nao kazi ingwawa baadhi ya mitandao na magazeti mwishoni mwa mwaka jana yalimtaja muigizaji wa Hollywood Hale Berry kuwa anaweza piga mzigo na muigizaji huyu wa swahiliwood. Uwoya alisema "Bado tunaendelea na mazungumzo najua watu wanasubiri kuona ukweli juu ya maneno yangu haya lakini ninachotaka kusema ni kwamba nilienda kwa ajili ya mazungumzo ila bado mambo hayajakaa sawa". Tunamtakia kila la kheri muigizaji wetu huyu katika safari yake ya kuanza kufanya kazi na watu nje ya nchi.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment