Monday, January 21, 2013

FLORA MVUNGI: NI LAZIMA SHILOLE AJE KUNIPIGIA MAGOTI LA SIVYO.....


 
Muigizaji maarufu Swahiliwood Flora Mvungi amesema kuwa bifu lake na muigizaji mwenzake Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole haliwezi kuisha hivi hivi kama shilole hatamuomba msamaha na kwenda kukiri kwenye magazeti kwa alichokisema ambacho kilionekana kumkera sana Flora.Swahiliworldplanet lilimtafuta Flora na kumuuliza kama yeye na Shilole wakipatanishwa wanaweza kuondoa tofauti zao na kuwa mashostito walioshibana kama mwanzo, Flora alijibu "Mi sina tatizo but ili mambo yawe sawa ni lazima aniombe msamaha mimi na H.baba kwenye hayo hayo magazeti ambayo alienda kuongea upuuzi la sivyo hayawezi kuisha na sitaki kusuluhishwa kimya kimya, waandishi waitwe akiri alichofanya mambo yawe wazi na baada ya hapo yatakuwa yameisha". Shilole na Flora walikuwa mabest wakubwa huko nyuma lakini wakaja kuwa chui na paka, shilole anadaiwa kumponda Mvungi pamoja na mwandani wake H.Baba kuwa Flora hana maendeleo yoyote tangu aanze uhusiano wake na H.Baba amekuwa anamsikiliza sana huyo H.Baba kama mungu mtu kiasi cha kushindwa kujijengea maisha yake yeye mwenyewe kwasababu anamtegemea na kumsikiliza kwa kila kitu.kwa upande mwingine mastaa hawa wa filamu waliiingia kwenye mtifuano mkali baada ya Flora kudaiwa yeye ndiye alimpokea Shilole na kuishi wote nyumbani kwake miaka kadhaa nyuma wakati shilole anatoka kwao kuja mjini kutafuta maisha lakini Shilole amemgeuzia kibao Flora kuwa asijitape yeye ndio alimpokea Flora mjini na kuishi nae nyumbani kwake.Pia hivi karibuni Flora alikaririwa na gazeti moja akisema "Shilole ananuka wanaume". Hatukufanikiwa kumpata shilole ili kumuuliza kama yupo tayari kuyamaliza wakipatanishwa lakini bado tunamsaka atoe yaliyo moyoni mwake....


MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment