Wednesday, October 10, 2012

UCHAGUZI UVCCM ARUSHA VURUGU TUPU CHATANDA ANUSURIKA KICHAPO.


Picha Juu na Chini ni Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa Uvccm mkoani Arusha kutoka wilayani Monduli wakiingia kwa mara ya pili  kupiga kura za kumchagua mwenyekiti wa umoja huo baada ya zoezi la awali kuvurugika katika ukumbi wa CCM mkoa.(picha na Mahmoud Ahmad-Arusha).
Mahmoud Ahmad Arusha
Hali ya tafrani imeibuka katika uchaguzi wa jumuiya ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi(Uvccm) mkoa wa Arusha baada ya katibu wa CCM mkoani hapa,Mary Chatanda kunusurika kipigo baada ya kutuhumiwa kuvuruga uchaguzi huo kwa lengo la kumpitisha chaguo lake ambaye alitajwa kuwa ni  ,Dk Harold Adamson.

Katika vurugu hizo  Chatanda alinusurika kipigo kutoka kwa wajumbe waliotoka wilayani ya Monduli baada ya kuamuru zoezi la uchaguzi huo lilirudiwe kwa madai kwamba wajumbe hao pamoja na wale wanaotoka wilayani Meru  idadi yao ilikuwa na kasoro.

Katika vurugu hizo makundi ya baadhi ya vigogo wa CCM hapa nchini yanyohusihswa na waziri mkuu mstaafu aliyejiuzulu,Edward Lowasa pamoja na Bernad Membe yalijidhihirisha waziwazi ambapo yalikuwa yakitambiana nje ya ukumbi wa mkutano.

Hatahivyo,katika hali isiyo ya kawaida polisi pamoja na maofisa wa usalama wa taifa waliwatimua waandishi wa habari waliokuwa nje ya ukumbi wa mkutano katika jengo la CCM mkoani hapa kwa amri ya katibu wa CCM wilaya kwa madai kwamba hawana mashati yenmye rangi ya kijani.
Zoezi la kupiga kura za uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti wa Uvccm mkoa lilianza majira ya saa 6;00 mchana ambapo upepo wa awali katika uchaguzi huo ulionyesha kwenda kwa mgombea,Robinson Meitenyiku anayetokea wilayani Arusha.

Vurugu hizo zilianza majira ya saa 9;00 mchana ambapo Chatanda alipoamuru wajumbe wa mkutano huo watoke nje ya ukumbi kwa madai kwamba kuna baadhi yao kutoka wilaya za Meru na Monduli walizidi.

Akitangaza uamuzi huo katibu huyo alisema kwamba wajumbe kutoka wilayani Monduli idadi yao haikuwa halali pamoja na ile ya wilayani Meru kwamba wajumbe watano walizidi kitendo kilichopingwa vikali.

Hatahivyo,mara baada ya wajumbe hao kutoka nje ya ukumbi wa uchaguzi walianza kupaza sauti kwamba katibu huyo analengo la kuvuruga uchaguzi huo kwa kuwa anataka kumpitisha mgombea wa nafasi hiyo,Dk Adamson.

Wakati vurugu hizo zikiendelea ndipo baadhi ya wajumbe kutoka wilayani Monduli walitishia kumchapa ndani ya ukumbi huo lakini juhudi zao zilizimwa na baadhi ya walinzi wakiwemo askari wa jeshi la polisi mkoani Arusha.

Mmoja wa wajumbe hao kutoka wilayani Monduli,Isaac Kadogoo alimwakia vikali Chatanda ndani ya ukumbi huo na kumtuhumu kwamba kitendo chake cha kukaa karibu na sanduku la kura kilikuwa na lengo la kutaka kuchakachua kura hizo.

“Mheshimiwa katibu rudi ukae meza kuu hata kama wewe ni msimamizi wa uchaguzi huu ondoka hapo kwenye sanduku la kura tuna wasiwasi na wewe”alisikika Kadogoo
Wakati hayo yakijiri nje ya ukumbi wa mkutano huo baadhi ya wajumbe walipinga kitendo cha Chatanda kuwatoa nje na kusema kwamba ana lengo la kuuvuruga uchaguzi huo ili chaguo lake lipite.

Hatahivyo,ilipotimu majira ya saa 9;15 mchana ndipo wajumbe hao walitangaziwa kurudi ndani ya ukumbi huo kwa lengo la kurudia zoezi la kupiga kura na ndipo walipojipanga kwa mistari na kuelekea katika ukumbi wa uchaguzi kupiga kura kwa mara nyingine.
Maofisa wa usalama wa taifa sanjari na askari wa jeshi la polisi mkoani Arusha walikuwa wakiranda randa nje na ndani ya  ukumbi wa mkutano kuimarisha ulinzi wakiwemo na baadhi ya maofisa wa Takukuru mkoani Arusha.

VIA: MO BLOG
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment