Wakati
gari hilo likiwa limeegeshwa dukani kwa mfanyabiashara huyo ili
kusubiri kupakia mzigo huo dereva alishuka kununua sigara maduka ya
jirani akamwacha utingo wake ndani ya gari peke yake ambaye anaitwa Juma
s/o Rashid 21-23, mwangaza wa Ngara ambaye ni familia ya mwenye
gari.(Pichani)
Baada ya muda mfupi kama dakika 15 hivi dereva alisikia mshindo mkubwa na alipokwenda kwenye gari alimkuta utingo wake ametupwa nje ya gari na akiwa amefariki mwili wake ukiwa na majeraha tumboni,mkono wa kushoto kiganja kimekatika,mkuu wa kulia kwenye paja ambalo limechimbika hadi kwenye mfupa, shingoni upande wa kushoto kuna shimo kubwa lililosababishwa na kitu chenye ncha kali. |
Pia
mfanyabiashara Donard s/o Nzugala Mwalimu ambaye ameumia mkono wa kulia
kwa kuchanwa chanwa na vipande vya chuma,amepelekwa hospitali ya mkoa
kwa matibabu zaidi.
|
Seni s/o Edward (25 ), msukuma mkulima wa Lubaga Kishapu amejeruhiwa bega la kushoto, majeruhi wote wametibiwa na kuruhusiwa.
No comments:
Post a Comment