Monday, June 4, 2012

Habari kwa Kiswahili: FBI Kuzima Kompyuta 350,000 Zilizoambukizwa na Virusi.


Mmoja kati ya watengeneza virusi aliyewekwa chini ya ulinzi na watu wa usalama FBI kutokana uhalifu wake. Hivi sasa FBI iko katika maandalizi ya kuzima kompyuta 350,000 duniani kote kutokana kuambukizwa na kirusi aina ya Trojan aliyetengenezwa na kundi la Kiestoni ambalo ni la wahalifu. Pia FBI wamefanikiwa kukamata kifaa aina DNS changer ambacho hutumika kutengenezea Vurusi hao. Walinzi wa kimarekani ambao wanashughulika na uhalifu huo wanafahamu kompyuta na Macs zote zilizoambukizwa na hicho kirusi aina ya Trojan , hivyo basi hitimisho la wamiliki endapo watachukua hatua ya kutatua tatizo, njia ni moja ya kuviondoa vifaa hivyo katika mtandao (Internet). Kifaa hicho cha kutengeneza virusi DNS changer, kilitengeneza na kuachia virusi hao kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2007. Kiliweza kuhasiri watumiaji, kwani kompyuta ilitenda kazi kinyume na inavyoweza. Na tatizo kubwa kwa watumiaji ilikuwa kompyuta kufanya kazi kwa taratibu sana katika mtandao. Pia virusi hivyo viliweza kulemaza antivirus programu na maelekezo ya kompyuta kuwa ya udanganyifu. Virusi hivyo viliachiwa na kundi la wahalifu wa Kiestoni na kuaminika kuwa, idadi ya virusi vilivyoachiwa katika mtandao ni dola milioni 16. Baada ya kashfa hiyo kugundulika, FBI walizima kifaa hicho kilichotumiwa na wahalifu cha kutoa mawasiliano ya mtandao (server) na mmoja wao kuchua nafasi hiyo, lakini Bureau alitaka kifaa hicho (server) kizimwe kabisa kwa sababu kinagharamia makumi ya maelfu ya dola kukiendesha. Bureau iliweka kifaa maalumu cha kutoa mawasiliano ya mtandao (Server) kwa maombi ya DNS kutoka kwa kompyuta zilizoambukizwa, kwani bila kifaa hicho (server) kompyuta hizo zilizoambukizwa zisingeweza kuunganishwa na mtandao. Jinsi ya kuunganishwa na mtandao Amri ya mahakama iliruhusu kifaa cha kotoa mawasiliano ya mtandao (Sever) cha FBI kupitisha anwani ya IP ya wale walioambukizwa na muda wake kumalizika Julai 9, wakati kompyuta hizo zitakapokuwa zimeondolewa katika mtandao (offline). hatua hiyo, kompyuta zote zilizoambukizwa na virusi aina ta Trojan hazitaweza kuunganishwa katika mtandao. Kuepukana na kompyuta yako kuzimwa na mtandao wa kuhakiki kompyuta zilizoambukiza "DNS ya FBI. ambao unaruhusu kwa sasa watumiaji kuangalia kama wana virusi na kuviondoa mapema. Kwani inasemekana kuwa tayari kuna baadhi ya kompyuta 150,000 zimesafishwa virusi hao. Lakini baadhi ya wakosoaji wanaonya hii, kuwa haitoshi hivyo ni bora kutangaza na uhamasishaji unahitajika. Ni lazima kuelewa kwamba kirusi aina ya Trojan kimeambatana na kirusi aina ya root kit ambacho ni kigumu kukiondoa katika kompyuta, hivyo kusababisha mtumiaji kufuta mpangilio na kuhifadhi upya. Hata hivyo makampuni ya usalama wa mipangilio ya kompyuta ambayo ni Norton, Kaspersky, Trend Micro, Microsoft, McAfee na wengine, husaidia kukiondoa kirusi aina rootkit bila kufuta mipangilio ya kompyuta yako. Kifaa hicho cha kutengeza virusi DNS Changer kimekuwa katika habari tangu Novemba 8, 2011, wakati botnet kubwa ya kusambaza virusi chini ya jina la kampuni ya Rove Digital, iliwekwa chini ya ulinzi na muungano wa msako ambao ni FBI pamoja na kundi la Kiestoni wahalifu. Na kutokea kukamatwa kwa wanaume sita. HABARI TOKA http://cheraboy.blogspot.com
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

No comments:

Post a Comment