Tuesday, April 23, 2013

PREZZO AUMBUKA BAADA YA PICHA YAKE YA UTUPU KUVUJA, ICHEKI PICHA HIYO HAPA


Jackson Makini a.k.a. Prezzo is in trouble…..on Saturday after the release of his new and controversial track Liqher,  his n*ked photos enjoying some private time with two lasses were leaked to the internet.


Check out the first PHOTO>>>
Source:Daily post

PICHA 6 ZA RIHANA AKIWA KATIKA SWIMING POOL NA BEST FRIEND WAKE! ZICHEKI HAPA







HIVI NDIVYO WALINZI WA CHADEMA WANAVYO MLINDA MWENYEKITI WAO MH. MBOWE

Walinzi wa Chadema wakiwa wameninginia kwenye gari la Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe wakati wakielekea kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika Uwanja wa Wajenzi, mjini Dodoma, Jumamosi iliyopita.

ALICHOKISEMA DIAMOND, KUHUSU KUMREKODI WEMA NA KUSAMBAZA CLIP HIYO MTANDAONI, HIKI HAPA



Skendo iliyokuwa ikiendelea mtaani kuhusu msanii Diamond na tuhuma za kumrekodi aliyekuwa mpenzi wake wa zamani mwanadada Wema Sepetu, msanii huyo amekir kuwa ni kweli alifanya tuhuma hizo kwaajili ya kulinda penzi lake.

“Hivi karibuni Wema amekuwa akinipakazia mbovu kwa mpenzi wangu Penny akiwa na leno la kutaka kuni haribia juu ya mimi na mpenzi wangu, nilichukia sana kwahiyo siku alivyoamua kunipigia simu ndipo niliamua kumrekodi ili kumsikilizisha Penny ambaye alikuwa haniamoni kabisa” Alifunguka Diamond.

Sauti hiyo ambayo ilitoka kwa Wema Sepetu ikiwa inambembeleza Diamond waweze kurudiana pamoja kwakuwa bado anampenda, Diamond amekiri kuirekodi hiyo sauti lakini amekana kuisambaza mitaani na hajui nani kafanya hivyo.

“Lengo langu kubwa ilikuwa ni kurekodi sauti hiyo na kumsikilizisha Penny, sasa ambaye aliichukua na kuisambaza mitaani sijui ni nani, lakini hata mi sikujisikia vizuri nilipoisikia mitaani maana sikupenda hali iwe hivyo lakini ndo sina jinsi” aliongeza Diamond.

Baada ya kukiri kujutia, Diamond aliambiwa aombe msamaha Live ili Wema asikie ila alikataa na kusema hawezi kumuomba msamaha maana haoni kosa lake.

Monday, April 22, 2013

ROSE NDAUKA ANASWA KIMAHABA HADHARANI


Staa anayefanya poa katika sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka amenaswa akiwa kimahaba akifanya mambo ya chumbani hadharani na mchumba’ke, Malick Bandawe, Ijumaa Wikienda limewapiga chabo.Tukio hilo lililoshuhudiwa na mwanahabari wetu, lilijiri wikiendi katika Ukumbi wa Hazina Lounge uliopo Coco Beach, Dar ambapo kulikuwa na sherehe ya ‘bethidei’ ya mdogo wake Rose, Recho Ndauka.Baada ya kukolea kwa ‘maji’, Rose na mwandani wake walianza kugandana kama ruba huku wakifanyiana vitendo vya  kimalavidavi.Wakati burudani zikiendelea ukumbini hapo, wawili hao walijitenga pembeni na kuanza kumwagiana mabusu mfululizo huku kila mmoja akijitahidi kuzionesha hisia za upendo alizonazo kwa mwenzake, jambo lililowashangaza baadhi ya wageni waalikwa.


“Makubwa haya! Sijawahi kumuona Rose akiwa kimalovee hivi yaani leo ndiyo mara ya kwanza ila kwa upande mwingine wanaendana na wanapendeza sema tu hawataki kufunga hiyo ndoa jamani tuione,” alisikika dada mmoja akijadili na mwenzake.  Pamoja na hayo, sherehe hiyo ya mdogo wake ilitawaliwa na vituko kibao baada ya wageni waalikwa kukolea ‘maji’ kwani kulikuwa na pombe kali tu huku wasichana wakiwa wamevalia vimini vilivyoacha wazi sehemu kubwa za maungo nyeti hasa wakati wakiserebuka hivyo kuwatoa udenda wanaume wakware.


Kwa hisani ya GLP

BREAKING NEWS:MAHAKAMA YA RUFAA YATUPILIA MBALI RUFAA YA KUPINGA USHINDI WA MBUNGE WA ARUSHA.


 Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema. Godbless Lema
--
Ombi la kwanza la waleta rufani la kutaka review ya uamuzi uliotolewa na mahakama ya rufaa juu ya kesi ya Mh.Lema na kutaka isikilizwe na jopo la majaji 7 limetupiliwa mbali leo katika mahakama ya rufaa na sasa ni majaji walewale waliotoa hukumu wamepitia ,Mahakama imetupilia mbali madai ya kwanza kwa kuwa hayapo based on merits Kesi hii ilifunguliwa tena baada ya Mh.Lema kushinda rufaa tarehe 21 desemba 2012,Warufani safari hii walitaka mahakama ipitie upya uamuzi uliotolewa na jopo la majaji watatu na wametaka kuwe na majaji saba.

Mahakama imetupilia mbali mashtaka yao na mahakama imewaamuru tena wakata rufaa walipe gharama zote za kesi.
 
CHANZO JUMA MTANDA

WANAWAKE WAUNGANA KUSUSIA BIDHAA NA MAONYESHO YA MWANAMUZIKI DIAMOND


Kwa Kumdhalilisha Bi.Wema Sepetu kwa kumrekodi katika simu na kusambaza mazungumzo nyeti !
Kitendo cha Mwanamuziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul Juma maarufu kama Diamond,cha kurekodi mazungumzo yake na star wa Bongo Move Bi.Wema Sepetu,
na kuyatuma mazungumzo yao ya mapenzi katika mitandao ni kitendo cha "Udhalilishaji wa Mwanamke" . kwa kuwa wanamuziki na wasanii wote wanatakiwa wawe ni mfamo na kioo cha jamii katika kuielekeza jamii kuishi 
kwa kufuata na kuheshimu maadili ,lakini mwanamuziki Diamond ameonekana kuwa ni  kiongozi wa "Udhalilishaji wa Mwanamke" kufuatia kitendo chake cha
kurekodi na kusambaza mazungumzo yao ya simu  ya kimapaenzi kati yake na
Bi.Wema Sepetu na mpenzi wake wa sasa Bi.Penny,kitendo hiki ni cha "kuwadhalilisha wanawake wa kitanzania"Tunaowaomba akinamama
na kinadada na wanawake wote kwa ujumla kususia kununua video,vcd,cd
pia kugomea kuhudhuria onyesho lolote lile litakalofanywa na mwamuziki
Nasibu Abdul Juma aka Diamond hadi pale atakapo waomba radhi wanawake wote
wa kitanzania popote pale walipo.
Wanawake wote wanatakiwa kugomea maonyesho ya mwanamuziki huyo na
na kutonunua bidhaa za mwanamuziki huyo Diamond ili kukomesha kabisa tabia hizi chafu za "Udhalilishaji wa Mwanamke" 
Wanawake wote ambao wamempa like au ad katika mitandao kama facebook kujiondoa mara moja na kogemea kununua jarida au gazeti lolote  litakalo mpamba mwanamuziki huyo.

HACKERS WAINGILIA TOVUTI YA MAKAMU WA RAIS WAANDIKA MATUSI NA KUWEKA NYIMBO ZA MATUSI


   
 
Katika hali isiyo kuwa ya kawaida hacker waendele kusumbua sasa ni zamu ya tovuti ya serikali ya makamu wa rais  kilicho andikwa nimatusi  kwa maandishi na kuna muziki wa hiphop wa mitusi.. Kuna mtu anajiita Govt Attacker. Mr. Spam ..! Eti ni Mmoroco. Home - uone. Je hii inamaanisha nini kwa systems zetu za mawasiliano kuwa rahisi kufanyiwa uhuni kama hivyi mpaka lini. 
Hata hivyo wahusika wa tovuti hiyo wamefanikiwa kuondoa tatizo hilo kwa sasa
SOURCE BONGOCLANTZ

Mkuu wa wilaya ya Singida adai wanafunzi 118 wameacha shule mwaka jana kutokana na utoro.


Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi, akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa ilani cha uchaguzi ya CCM kwa mkuu wa mkoa wa Singida (aliyeketi) Dk.Parseko Kone.Dk.Kone alifanya ziara  ya kiazi katika manispaa ya Singida.(Picha na Nathaniel Limu).

Na  Nathaniel Limu.
Jumla ya wanafunzi 139 wa shule za msingi katika halmashauri ya manispaa ya Singida waliacha shule mwaka jana kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya utoro.

Akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM kwa mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone aliyefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika manispaa ya Singida, Mkuu  wa wilaya ya Singida Queen Mlozi amesema jumla ya wanafunzi 118 kati yao wavulana 76 na wasichana 42,waliacha shule kutokana na utoro.

Amesema wengine 11 waliacha shule kutokana na kukosa mahitaji muhimu na wawili walifariki dunia katika kipindi hicho cha mwaka jana.

Akifafanua zaidi, amesema kuwa utoro wa wanafunzi katika baadhi ya shule, umeendelea kuwa tatizo kubwa hali inasababishwa na wanafunzi kujihusisha na biashara ndogo ndogo, kuajiriwa na pia wazazi kutowapatia mahitaji muhimu.

Aidha, Mlozi aitaja baadhi ya mikakati ya kudhibiti utoro wa wanafunzi kuwa ni pamoja na kuhamasisha na kuhimiza shule na jamii kuongeza vivutio shuleni ikiwemo kuimarisha bendi za shule, michezo, kwaya na ngoma.

Mkuu huyo wa wilaya, ametaja mikakati mingine kuwa ni kuhamasisha jamii kuwapa watoto chakula cha mchana wawapo shuleni na orodha za watoro kupelekwa kwa maafisa watendaji wa kata ili sheria zichukuliwe.

Wakati huo huo, Mlozi amesema manispaa ya Singida inakabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 274, nyumba za walimu 793, matundu ya vyoo 870 na maktaba 43.

AVRIL KUZINDUA SINGLE YAKE NA OMMY DIMPOZ TAREHE 30 APRIL


Siku ya mkesha wa kuamkia sikukuu ya wafanyakazi "mei mosi", Msanii kutoka Kenya Avril anatarajia kuzindua single yake aliyomshirikisha Ommy Dimpoz huku perfomace za wasanii kutoka Kenya na Bongo zikitawala 


LULU AINGIA LOCATION TENA KUANZA KUFANYA VITU VYAKE.


Actress Elizabeth Michael(Lulu) anaonekana tayari yupo location akifanya films baada ya kimya cha muda mrefu kutokana na misukosuko ya hapa na pale iliyomkumba. Kupitia instagram Lulu ameweka picha akiwa location na Hashim Kambi na kuandika maneno haya "take 1 action, mic location, me doing ma thing". Ujio wa Lulu unasubiriwa kwa hamu sana because she is hot on screen and she has been missed alot by her fans. Hata hivyo haijajulikana bado jina la film hiyo ni lipi.

JACKLINE WOLPER: MIMI NA RAMMY GALIS SIYO WAPENZI BALI TUNAFANYA FILAMU YA KIISLAMU PAMOJA.


Tangu juzi baadhi ya blogs zimeandika kuwa Jackline Wolper na muigizaji mwenzake Rammy Galis wanaonekana kuwa wapenzi wapya kwa picha za wawili hao kuonekana katika mitandao ya kijamii huku zikiambata na maneno ya my baby. Juzi Swahiliworldplanet ilipoona tu picha za wawili hao ilimuuliza Wolper na kudai kuwa wao si wapenzi bali wanafanya filamu ya kiislamu, tukamuuliza tena filamu inaitwaje but Wolper hakujibu kwa wakati akionekana kuwa busy kidogo na mambo flani. Ila baada ya kuona news zinasambaa sana kuwa wawili hao wanakula bata kisirisiri SWP ilimuuliza tena Wolper kuhusu madai hayo na kusema si kweli ila wanafanya filamu kama alivyosema mwanzo na filamu hiyo akasema inaitwa Kanzu na Hijabu Zaficha Maovu. Wolper alisema "bata gani si tunafanya filamu ya kiislamu, inaitwa Kanzu na Hijabu Zaficha Maovu". Hayo ndiyo majibu ya Wolper kama kweli ni wapenzi kama wengine wanavyodai itakuja kubainika tu maana wahenga wanasema penzi ni kikohozi hivyo huwezi kukizuia. Rammy Galis anaonekana katika films kama Malaika akiwa na Seth Bosco na Rose Ndauka. Hatukufanikiwa kumpata haraka Rammy ili kutoa maoni yake kuhusu issue hiyo lakini tukimpta utasikia from his side too.

                                                                        Rammy Galis
                                                              Jackline Wolper

HII NDIO AC FAKE YA LULU INAYOTUMIWA NA WATU WASIOJULIKANA ONA HAPA.


oo


Kwa upande wa Elizabeth Lulu ambaye bado anakabilliwa na kesi mahakamani, watu wanachulia advantage na kufungua account mpya ya twitter ambako ndipo Lulu ana-spend sana time zaidi ya facebook siku hizi. Kupitia Instagram Lulu aliandika “Haya lulu mwngne huyo on twitter…..!am tired jaman…nyie ma lulu nioneeni huruma basi…..!!!nimechoka kusikia case’z zenu!!!!NIMECHOKA JAMANI“. Accouunt hiyo fake inatumia jina la @Lulu_actress wakati account halisi ya lulu ni @Hotlulumichael. Kitu pekee ambacho kinaweza kuwatofautisha lulu fake na wengine ni alama ya Verified ambayo twitter hutoa kwa watu maarufu.

MPENZI WA ZAMANI WA CHRIS BROWN ACHIA PICHA ZA UTUPU ZIONE HAPA.










Sunday, April 21, 2013

Wakati Maduro akiapishwa kuwa rais mpya wa Venezuela avamiwa na kunyang’anywa kipaza sauti na mtu asiejulikana.



Mwanasiasa Nicolas Maduro ameapishwa rasmi kuwa rais wa Venezuela na kuchukua nafasi ya Hugo Chavez.
 Akizungumza baada ya kuapishwa  Maduro ametoa wito wa kufanyika mazungumzo na upinzani ili kuijenga nchi yao iwe bora zaidi.

Maduro mwenye umri wa miaka 50 amesema anataka kuanza kipindi chake cha urais kwa kuwataka watu wa Venezuela kuijenga nchi hiyo iwe ya amani.

Hata hivyo, wakati akihutubia mbele ya marais, mawaziri wakuu na viongozi wengine, hotuba hiyo ilivurugwa baada ya mtu mmoja kuvamia jukwaa na kumpokonya kipaza sauti.

Akizungumza baada ya tukio hilo lililoleta mkanganyiko, Maduro ameisema vikosi vya usalama vimeshindwa kazi, kwani angeweza kuuawa.

Maduro ameapishwa saa chache baada ya tume ya uchaguzi ya Venezuela kusema itahesabu tena kura zilizosalia za uchaguzi wa Jumapili iliyopita kufuatia mpinzani wake Henrique Capriles, kudai kura zihesabiwe upya.

JUMBA LA LWAKATALE LAZIDI LETA UTATA BUNGENI




       WABUNGE wamemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Terezya Huvisa kuzivunja nyumba mbili zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam zilizojengwa katika fukwe ya bahari ya Hindi ikiwemo ya mbunge licha ya kwamba kuna zuio la Mahakama.

Bila kutaja majina ya wamiliki hao, wabunge hao walitaka hatua hizo zichukuliwe kwa haraka kwa nyumba hizo zilizojengwa kwenye fukwe kinyume cha sheria zivunjwe kwa maelezo kuwa hazina ofa wala hati.
Sambamba na hilo wametaka watendaji wa Serikali waliohusika kutoa vibali kuruhusu ujenzi huo kwa maelezo kuwa walichukua rushwa wachukuliwe hatua.

Mbunge wa kwanza kuanza kuzungumzia hilo ni wa Viti Maalumu, Esther Bulaya (CCM) aliyetaja viwanja viwili vyenye namba 2019 na 2020 kikiwemo cha mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani waliojenga nyumba zivunjwe licha ya kuwepo zuio la Mahakama.


“Mwaka jana Waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka alivunja nyumba za kawaida licha ya zuio la Mahakama, lakini nyumba zilizo kwenye viwanja namba 2019 na 2020 hazikuvunjwa kwa sababu ya zuio la Mahakama hii ni double standard (ndumilakuwili) hatuwezi kuvumilia.

“Wengine wenye nyumba ni viongozi tupo nao humu tena wa kiimani, lakini kwa nini viongozi tunafanya hivi wakati tunatakiwa tuwe wa mfano na tunawafanya viongozi wenzetu washindwe kufanya kazi zao?… hakuna haja ya kuogopa Waziri Huvisa (Mazingira) vunja nyumba, haiwezekani kuwa na nguvu ya fedha.

“Wabunge wenzangu tuazimie Manispaa ya Kinondoni na NEMC (Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira), wakavunje nyumba hizo ndani ya wiki moja , naomba kutoa hoja,” alisema.
Hata hivyo, Spika Anne Makinda alimweleza; “Haiwezekani kutoa hoja kwa kuingilia vyombo vingine”.

Mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani mwenye nyumba katika eneo hilo la Mbezi Beach aliyejenga katika fukwe ya bahari kwa kuondoa mikoko na kuweka kifusi na kujenga nyumba ni Mbunge wa Viti Maalumu, Mchungaji Dk Getrude Lwakatare (CCM). Hata hivyo wakati wa michango hiyo mbunge huyo hakuwa ndani ya Bunge.


Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Grace Kiwelu (Chadema) akichangia bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, alisema Kamati yake ya Ardhi na Mazingira ilitembelea eneo hilo la Mbezi Beach na kukuta aliyejenga katika kiwanja 2019 hakuwa na ofa wala hati.
“Ametumia pesa kuwarubuni watendaji akaondoa mikoko, akaweka kifusi na akajenga nyumba naomba Wizara ya Ardhi na ya Mazingira wawachukulie hatua watendaji hao,” alisema.

Akijibu hoja ya Bulaya, kuwa kwanini nyumba ya Mchungaji Lwakatare haikuvunjwa wakati nyingine zilivunjwa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema alisema: “Sisi ni wajibu wetu twende mahakamani kusema watu hao wamevunja sheria kujenga hapo.



Wao wanaruhusiwa na Katiba na Mahakama itafuata sheria. “Nashauri Bulaya usitoe Shilingi kuzuia Bajeti ya Waziri, uje tuone huyo kigogo itakuwaje.” Hata hivyo, Huvisa alisema: “Nyumba tulizovunja hazikuwa na kesi na hii tuliyoiacha ilikuwa na kesi.”

Jumba la kifahari linalodaiwa kuwa la Mchungaji Lwakatare ambalo lilizinduliwa mwaka jana, limekuwa likitajwa kuwa lina thamani ya takribani Sh bilioni 1.5.

MAKAHABA WAWAVALIA NJUGA POLISI


http://1.bp.blogspot.com/--rWzm9iVdsE/UIc-gPL6IMI/AAAAAAAABT0/uW-W06MAnKU/s1600/MALAYA+WA+DAR.jpg
Jeshi la Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni, limelalamikiwa kwa vitendo vya baadhi ya askari wake kuvamia vyumba vinavyodaiwa kupangwa na watu wanaodaiwa kuwa makahaba (madanguro) na kuwapora fedha, simu na vitu vingine vya thamani nyakati za usiku.

Aidha, askari hao wamedaiwa kuwageuza wanawake hao mashine za kutolea fedha (Atm) ambapo hufika katika vyumba vyao kila baada ya wiki moja na kuwadai fedha kati ya Sh.30,000 na 50,000 kila mmoja kama hongo ili wasiwafikishe polisi.


Malalamiko hayo yametolewa na baadhi ya akina mama wanaoishi eneo la Mwananyamala walipozungumza na NIPASHE baada ya askari hao kukamata wanawake zaidi ya 87.

Kiongozi wa wanawake hao, Judith Rugamwa alidai kuwa, askari hao kutoka vituo vya Oysterbay na Mabatini wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwapiga, jambo ambalo ni kinyume cha haki zao binadamu.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjzoX4tkEBNSr8B6lU77Y4dKjBPy91OgoX6WkX_evvwJYa226dcny37NZYaIDKS0pOrrwCmk0f0a2pGrxYTdQ-PoS4iRXB_tFWLtVHy8BcX0f6sj6dOGOigaBfj57Zp7Bvzxf6LC1ys55E/s1600/African.jpg

"Wakitukamata huwa wanasema kosa letu ni kufanya ukahaba, lakini tukifikishwa kortini kosa linabadilika na kuwa uzembe na uzururaji, wakati wametukamata vyumbani kwetu ," alisema Judith.

Alisema wamechoka kunyanyaswa kama wakimbizi na kuonya kuwa sasa wanajiandaa kupambana na kila askari atakayefika hasa nyakati za usiku na kuwavunjia milango ya vyumba vyao ili kuwamata na kuwalazimisha wawape fedha huku wakimtaja afande Swai na Emma kuwa ndiyo wanaoongoza uovu huo.


Akizungumzia tuhuma hizo, afande Swai alijitetea kuwa yeye binafsi hajawahi kushiriki katika kuomba fedha wala kupora simu za wanawake hao licha ya kukiri kuwa ndiye anayeongoza misako yote Kinondoni.

"Kuhusu madai ya kuomba fedha, siwezi kukataa kwa sababu mimi huwa siingii vyumbani kukamata wanawake hao, badala yake askari wangu ndiyo wanaohusika moja kwa moja kabla ya kuwaleta katika gari ambayo huwa nawasubiri, lakini kama wanafanyiwa hivyo naomba wawataje kwa majina askari hao," alisema.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUReGLC7b1GIOVWKcyWLbkal6ySfN84xr3UeyYE6DMgX87s7kqwF3sI4FC-5vFnFD61sFiKpcQh1pGc-A3NZr_U6V5sesI1zOHsb8du66Vy0_t56XqmaqM_inSplpjhjLOPG3hDwKBVZHr/s1600/MALAYA.jpg


Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoani wa Kinondoni (RPC), Charles Kenyela, alisema amri ya kuwasaka na kuwakamata makahaba hao huwa inatolewa na ofisi yake na kwamba madai ya polisi wake kuchukua fedha na simu za watuhumiwa ni uongo mkubwa.


"Kama kuna mtu amewahi kufanyiwa hivyo aje ofisi kwangu na ushahidi ili ofisi yangu ichukue hatua kali za kinidhamu kwa sababu anayeshawishi, anayetoa na kupokea rushwa wote wanafanya makosa, waache kulalamika waje niwasilikize," alisema Kenyela.

NATURE AKERWA NA KIPINDI CHA TELEVISHENI WAMTOA NA KUKATIZA INTERVIEW KISA KAVAA NDALA NA KAWOSH


Msanii mkongwe na maarufu nchini, Juma Kassin Kiroboto, aka Nature, ameonyesha kukerwa na kile kilichoendelea jana usiku katika kipindi cha burudani cha  televishen inayotizamwa africa ya mashariki alipokuwa akifanya nao interview. Nature alionekana akiwa amevaa kawosh na ndala na mara baada ya mahojiano mafupi ya mwanzo ambapo mtangazaji alisema watarejea baada ya mapumziko mafupi Nature hakuonekana tena. Kilichotokea  kwa mujibu wa Nature mwenyewe, ni wakati wa mapumziko hayo, mtangazaji wa kipindi hicho alimfata na kumuambia kuwa hataendelea na interview tena kwasababu ya mavazi aliyokuwa kavaa ambayo ni ndala na kawosh. kuonyesha kukerwa kwake na ishu hiyo Nature aliamua kuandika kupitia ukurasa wake wa facebook....

hivi kwa mfano angekuwepo mzungu pale na kavaa ndala wangesitisha mahojiano na kuvaa kaoshi ni tatizo,kunywa nimekunywa bt kuna baya nimeliongea na hivi kama kweri we nimuandishi wa habari unaruhusiwa kuvaa vile kisheria kama yule mtangazaji nimeboreka kinoma na ikiwezekana nasitisha kuanzia ssa kupeleka ngoma zangu pale siitaji interview

Saturday, April 20, 2013

TAARIFA KUHUSU WALIOMALIZA DARASA LA SABA KUANZA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU

.
.
http://www.mwananchi.co.tz wameripoti leo kwamba Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu kwa kutumia uzoefu wao ambapo udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.

Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B ambapo Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia Mwananchi kwamba baada ya kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha mitihani hiyo maalumu.

Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama ‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine, Sifa zinazotakiwa ili kujiunga…. mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba,  atakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma, awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni”

Mkurugenzi amekaririwa akisema “Kuna watu wameishia darasa la saba, lakini wamefanya kazi katika eneo moja, mfano karani wa mahakama, mwandishi wa habari kwa muda mrefu, mfumo huu utawawezesha kuendelea na masomo bila tatizo, kutakuwa na mitihani ya masomo matatu ambayo mtahiniwa ili apate nafasi ya kuendelea na masomo ni lazima afaulu kwa wastani wa daraja B, daraja la kwanza linaloanza na alama A ni 75-100, daraja B+ ni 60-75, B ni 50-59, C ni 40-49, D ni 35-39 na daraja E ni 0-34.

Wednesday, April 17, 2013

BREAKING NEWS: Bi.Kidude AFARIKI DUNIA

 
Msanii nguli wa Muziki wa Taarab asili kutokea visiwa vya Zanzibar nchini Tanzania, Fatuma binti Baraka maarufu kama Bi. Kidude amefariki dunia leo huko Zanzibar.
  
 
Endelea kusikiliza East Africa Radio na kutazama East Africa Television (EATV) kwa habari zaidi.
chanzo EATV