Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

Wednesday, September 7, 2016

MAFUTA YASHUKA BEI

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji na Mafuta (Ewura), imetangaza kushuka bei ya mafuta ya aina zote kwa jumla na rejareja.


Bei hizo mpya ya mafuta zimeshuka katika mikoa yote isipokuwa Mkoa wa Tanga, hasa kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa.



Taarifa ya Ewura jana ilisema bei hizo zimeshuka ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, mwaka huu.



Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi, alisema katika toleo hilo, bei ya rejareja kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa imepungua kwa viwango tofauti.



Alisema kwa petroli imeshuka kwa Sh 65, dizeli Sh 63 na mafuta ya taa Sh 86.



“Bei ya jumla imepungua ambako kwa petroli ni Sh 65.31, dizeli Sh 63.39 na mafuta ya taa Sh 85.93,” alisema.



Ngamlagosi alisema kushuka kwa bei ya petroli katika soko la dunia na kupungua kwa gharama za usafarishaji/uletaji wa mafuta hayo nchini, ndizo sababu kuu zilizochangia kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la ndani nchini.



“Bei ya jumla na rejareja kwa petroli na dizeli katika Mkoa wa Tanga imeongezeka kidogo ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, 2016.



“Katika toleo hili, bei ya rejareja kwa petroli na dizeli imeongezeka kwa viwango ambavyo petroli ni Sh 50 na dizeli Sh 19. Kwa kulinganisha na matoleo haya mawili, bei ya jumla imeongezeka.



“Petroli Sh 49.61 kwa lita sawa na asilimia 2.80 na dizeli Sh 18.57 kwa lita sawa na asilimia 1.1.



“Ongezeko hili la bei limechangiwa kwa kiasi kikubwa na kupokea mafuta mapya (petroli na dizeli) ndani ya Agosti 2016, ambayo yalitarajiwa kupokewa Julai 2016 na pia kutokupokea mafuta mapya kutoka katika meli ya MT. Nevaska Lady ndani ya Agosti mwaka huu,” alisema Ngamlagosi.



Hata hivyo, alisema mamlaka hiyo inawakumbusha wananchi kwamba bei kikomo ya mafuta kwa eneo husika, pia inapatikana kupitia simu zao za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kufuata maelekezo.



Alisema huduma hiyo hutolewa bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi nchini.

JPM atoa siku saba kwa wadaiwa sugu NHC

Siku chache baada ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) litoe nje vitu vya mmiliki wa Mbowe Hotels Limited, Freeman Mbowe kwa kile kilichoelezwa kushindwa kulipa kodi ya pango iliyofikia Sh bilioni 1.172 , Rais Dk. John Magufuli amempongeza Mkurugenzi wa Shirika hilo, Nehemia Mchechu kwa hatua hiyo.

Pamoja na hali hiyo ametoa siku saba kufukuzwa kwa wapangaji wote wa NHC watakaoshindwa kulipa kodi ya pango, zikiwemo wizara, taasisi za Serikali, watu binafsi na watumishi wa umma.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika mkutano wake na waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota, Rais Dk. Magufuli, alisema hatua zinazochukuliwa na Mchechu zitasaidia upatikanaji wa fedha za kuwekeza kwenye miradi mipya.


“Nakupongeza kwa hatua unazoendelea kuchukua. Wale wapangaji wote ni lazima walipe madeni yao, nimetoa maagizo leo (jana) wapangaji wote wa Serikali, Wizara ya Ujenzi, wizara gani kule ndani ya siku saba lazima wawe wameshalipa madeni yao,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:


“Wasipolipa endelea kuwatoa nje kama ulivyomtoa yule jamaa (Mbowe),” alisema na kusababisha watu kushangilia huku wakiangua vicheko.


“Endelea hivyo hivyo usiogope kumtoa nje mtu yeyote. Awe amepangishwa ni wa CCM mtoe nje, awe ni wa Ukawa mtoe nje, awe mtumishi wa Serikali mtoe nje, awe mtumishi huyo ni waziri mtoe nje, awe ni Rais mtoe nje,” alisema Rais Magufuli.


Alisema anashangaa kuona watumishi wa Serikali wakishindwa kulipa madeni ya kodi za pango wakati kila siku wanaomba safari za nje huku wakilipana posho.


“Ukipanga na ukashindwa kulipa kodi jiandae kuondoka. Nataka uendelee kuwatoa na nakueleza kweli Nehemia sitanii ‘take it from me and I am very serious’ (nisikilize mimi sifanyi mzaha) ” alisisitiza.


Alisema madeni hayo yangekusanywa yangelisaidia shirika hilo kuwekeza katika maeneo kama la Magomeni Kota ambalo limekaa kwa muda mrefu bila kuendelezwa.


“Inawezekana ungekuwa na hizo fedha ungeshajenga katika eneo hili kuliko kuanza kumtafuta mwekezaji kwa ujanjaujanja. Haiwezekani eneo kama hili (Magomeni Kota) la ekari 33 unazitoa hivi hivi na ni mali ya Serikali,


“Afadhali umtoe mke wako umpe mzaramo mtani wangu akae naye,” alisema Rais Magufuli huku wananchi wakiangua kicheko.

Alimsisitizia Mchechu kuharakisha kuzitoa wizara zinazodaiwa kwenye majengo yake ili ziharakishe kwenda kujenga Dodoma yaliko makao makuu ya nchi.


Awali Rais Magufuli, alisema alibaini ukweli kuhusu eneo hilo kwamba lilitaka kuuzwa kwa mwekezaji kinyemela na kuwaacha bila kitu wakazi hao.


VIA Mtanzania

Darasa la saba waanza mitihani leo


WATAHINIWA 795,761 wanatarajia kufanya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) unaofanyika leo na kesho nchini kote.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk Charles Msonde alisema wanafunzi 372,883 ambao ni sawa na asilimia 46.86 ni wavulana na wasichana ni 422,878 ambao ni asilimia 53.14.


Mwaka 2015 watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 775,729 huku 763,602 ndio waliofanya mtihani huo na wanafunzi 518,034 walifaulu.


Dk Msonde alisema watahiniwa 765,097 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili na watahiniwa 30,664 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiingereza ambayo wamekuwa wakiitumia katika kujifunzia. Masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa.


Alisema watahiniwa wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani ni 95 wakiwemo wavulana 57 na wasichana 38 wakati wale wenye uoni hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 810 ambao kati yao wavulana ni 402 na wasichana ni 408.


“Maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika kiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, fomu maalum za kujibia mtihani na nyaraka zote muhimu katika halmashauri na manispaa zote nchini,” alisema Dk Msonde.


Aidha, Dk Msonde alitoa mwito kwa kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha taratibu za mitihani ya Taifa zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mazingira ya vituo vya mitihani yanakuwa salama, tulivu na kuzuia mianya ya udanganyifu.


“Wasimamizi wanatakiwa kusimamia kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu. Nawaaasa kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani Baraza litachukua hatua kali kwa yeyote yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya Taifa,” alieleza.

Ujenzi nyumba za Magomeni Kota kukamilika mwakani

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 06 Septemba, 2016 amewatembelea Wakazi wa Magomeni Kota Jijini Dar es Salaam ambao nyumba walizokuwa wakiishi katika eneo hilo zilivunjwa mwaka 2012 kwa makubaliano ya kujengwa nyumba za kisasa na kuwaahidi kuwa Serikali itaanza kujenga nyumba hizo katika kipindi cha Miezi miwili kuanzia sasa.


Rais Magufuli amesema ujenzi wa nyumba hizo utakamilika katika kipindi cha mwaka mmoja na baada ya hapo Wakazi wote 644 walioondolewa kupisha ujenzi wa nyumba za kisasa watapatiwa nyumba za kuishi na kwamba wataishi katika nyumba hizo kwa muda wa miaka mitano bila kulipa pango na baada ya muda huo kuisha wataandaliwa utaratibu wa kila mmoja kuuziwa nyumba anayoishi.


"Nakwenda kutoa pesa Mwezi huu, ili Mkandarasi atakayeteuliwa aanze kujenga nyumba za wakazi wote 644, wakati wanapojenga hayo majengo ya wakazi 644, ujenzi utaendelea pia katika maeneo mengine, ili kusudi kama yanajengwa maduka makubwa (Shopping Malls) au zinajengwa nyumba zingine za wananchi wanaohangaika nao tuwalete hapa.


"Nataka katika miji yetu ya Tanzania tuanze kupambana na makazi ya wananchi, tuwe tunajenga nyumba ili hata hawa masikini wa Tanzania waweze kufaidi kukaa kwenye ghorofa" Amesema Rais Magufuli.


Aidha, Dkt. Magufuli ameelezea kusikitishwa kwake na namna tatizo la wakazi wa Magomeni Kota lilivyoshughulikiwa na amewaahidi kuwa Serikali yake itahakikisha wananchi hao hawasumbuliwi tena.


Pamoja na hatua alizochukua kwa wakazi wa Magomeni Kota ambao nyaraka zimeonesha walikuwa wakiishi katika Nyumba za Shirika la Nyumba (NHC), Rais Magufuli ameagiza maeneo yote katika mikoa 20 hapa nchini yenye nyumba za kuishi za NHC kama lilivyo eneo hilo yatwaliwe na Serikali na kwamba Serikali itatoa maelekezo ya namna yatakavyotumika ama kuendelezwa.


Pamoja na kumpongeza kwa kazi nzuri anazofanya, Rais Magufuli amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Shirika na Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Neemia Mchechu Kyando kuwaondoa wapangaji ambao ni wadaiwa sugu wa pango zikiwemo Taasisi za Serikali ambazo amezipa siku saba kuwa zimelipa madeni yao.


"Wale wapangaji wote lazima walipe madeni yao, nimetoa maagizo leo, wapangaji wote wa Serikali, Wizara ya Ujenzi, Wizara gani kule... ndani ya siku saba lazima wawe wameshalipa madeni yao wasipolipa endelea kuwatoa nje.


"Endelea hivyo hivyo usiogope kumtoa nje mtu yeyote, awe amepangishwa ni wa CCM mtoe nje, awe wa UKAWA mtoe nje, awe Serikali mtoe nje, awe Waziri Mtoe nje, mpangaji huyo awe ni Rais mtoe nje, ni lazima upate pesa zitakazowezesha kuendesha Shirika la Nyumba la Taifa" Amesisistiza Rais Magufuli.


Wakati huo huo, Rais Magufuli amekagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa kwa chuo hicho alipokwenda kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho tarehe 02 Juni, 2016.


Jumla ya majengo 20 yenye ghorofa nne kila moja yanajengwa katika eneo hilo la mashariki mwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na yatakapokamilika tarehe 31 Desemba, 2016 yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanachuo 3,840 kati ya wanachuo 7,000 wanaolazimika kupanga vyumba vya kuishi mitaani kutokana na kukosa nafasi katika mabweni ya chuo yaliyopo.


Akizungumza na wafanyakazi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na Vijana walioajiriwa katika kazi za ujenzi wa majengo hayo Rais Magufuli amepongeza moyo wa uzalendo waliouonesha kwa kufanya kazi usiku na mchana na amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TBA Elius Mwakalinga kuendelea kuwatumia vijana hao katika miradi mingine ambayo Serikali itaitekeleza kwa kutumia TBA.

TBA ikitumia wataalamu na Vijana wa Kitanzania itatumia Shilingi Bilioni 10 kukamilisha ujenzi huo ikilinganishwa na endapo ingetumia Wakandarasi ambao walitaka kulipwa kati ya Shilingi Bilioni 50 na Bilioni 100.


Rais Magufuli ameutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuacha kuingia mikataba mingine na wafanyabiashara wanaotumia maeneo ya chuo hicho kujenga majengo ya kibiashara na badala yake amesema Serikali itaendelea kutafuta namna ya kulimaliza tatizo la mabweni kwa wanafunzi wa chuo hicho na vyuo vingine hapa nchini. 

Tuesday, August 16, 2016

Jibu la Mwimbaji Emmanuel Mbasha kuhusu kurudiana na Flora Mbasha


Kama utakuwa unakumbuka mnamo September 21,2015 moja ya stori kubwa iliyogusa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania ni ishu ya Hukumu ya Kesi ya Mwimbaji wa Gospel Tanzania, Emmanuel Mbasha ambapo alikuwa anakabiliwa na Keshi ya kumbaka shemeji yake na kesi imekuwa Mahakamani tangu 2014.

Wengi tunafahamu kwamba mwimbaji huyo aliachiwa huru baada ya Mahakama kumkuta hana hatia kwenye Kesi hiyo, sasa leo kajibu swali kuhusu kurudiana na mkewe Flora Mbasha na kuyaongea haya>>

‘Mimi kurudiana na Flora Mbasha ni ngumu kwasababu yeye ndio aliniacha mimi na yeye ndio aliandaa mazingira yake ya kuniacha mimi mpaka ikafika wakati Familia yangu, viongozi mbalimbali wa Dini wakawa wanamshauri lakini akutaka kurudiana na mimi kwahiyo naweza sema ni ngumu kurudiana na Flora’




WANAFUNZI SHULE YA MSINGI MASANZA 1192 WASOMEA JUANI

Na, Shushu Joel,BUSEGA


Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Masanza katika Kijiji cha Mitindu Kata ya Kiloleli, Wilaya ya Busega, Mkoani Simiyu, wanalazimika kusomea kwenye mti kutokana na upungufu wa madarasa.

Aidha upungufu huo wa madarasa unawalazimu wanafunzi wengine kusomea juani katika madarasa mawili ambayo hayajapauliwa licha kufikia hatua hiyo miaka miwili iliyopita.

Shule hiyo ilianzishwa tangu mwaka 2006 lakini mpaka sasa haina hata nyumba moja ya walimu.

Wanafunzi wa shule ya msingi masanza wakiwa darasani

Akizungumza na NIPASHE mwalimu mkuu wa shule hiyo Vedasto Chibuga  amesema kutokana na uwepo wa changamoto hizo kunapelekea idadi kubwa ya wanafunzi kusomea kwenye darasa la vyumba viwili ambalo halijaezekwa, huku wengine wakisomea chini miti.
 
Chibuga aliongeza kuwa wanaosomea kwenye darasa hilo ni wanafunzi wa awali,darasa la sita na darasa la tatu, lakini ikifika majira ya saa tano asubuhi hulazimika kuthitisha vipindi kutokana na jua kali na kwenda kuwachanganya na wananfunzi madarasa mengine.

“Sera ya elimu inasema kuwa kila chumba wasome wanafunzi 45 lakini hapa kwangu mkondo mmoja wanasoma wanafunzi wasiopungua 100  kutokana na changamoto hizo za uhaba wa vyumba vya madara”.

Aidha Chibuka alisema kuwa serikali ndio ya kulaumiwa kwani wananchi wao walitimiza wajibu wao wa kuchangishana kwa ajili ya ujenzi wa boma hilo tangu mwaka 2013.

Kwa muji mwalimu mkuu huyo, hali inawafanya walimu kukata tamaa hali inayopelekea wanafunzi kutofanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa kutokana na mazingira magumu ya kufundishia.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi katika shule hiyo, Mikwanga Yona, alisema kuwa ni aibu kwa serikali kushindwa kupaua jengo hilo lililojengwa kwa nguvu za wananchi, na kwamba hali hiyo inaweza kufanya wananchi kukata tamaa kuchangia maendeleo katika maeneo yao kwa kukatishwa tamaa na serikali kwa kushindwa kuunga mkono jitihada zao.
Wanafunzi wakiwa darasani na mwalimu wao akiwafundisha

Ofisa Elimu Kata ya Kiloleli John Mayunga amethibitisha kuwepo kwa hali hiyo, na kwamba jambo hilo wamelifikisha katika kikao cha maendeleo ya kata ambacho mwenyekiti wake huwa diwani wa kata husika, na kuongeza kuwa pengine serikali inalifanyia hivyo kwa kuwa walishaliwasilisha katika ngazi ya halmashauri.


>>>>>>>>>>MWISHO>>>>>>

Monday, August 15, 2016

Video ya Original Komedi alivyoingia ukumbini kwenye Harusi ya Masanja

Ni August 14, 2016 ambapo mchekeshaji kutoka kwenye kundi la Original Komedi, Emmanuel Mgaya aka Msanja Mkandamizaji aliziandika headlines baada ya kufunga ndoa na mchumba wake Monica katika kanisa la Mito ya Baraka Dar es Salaam.

Miongoni mwa walitoa burudani kwenye sherehe hiyo wakiwemo wachekeshaji wenzake kutoka kundi la Original Komedi, tazama video uone jinsi walivyoingia ukumbini.



Download


Download
Download

Thursday, July 7, 2016

JPM ateua wakurugenzi halmashauri za majiji, wilaya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo July 07 2016 amefanya uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji 5, Manispaa 21, Miji 22 na Wilaya (DC) 137 za Tanzania Bara.
Uteuzi huo umetangazwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe ambapo kati ya wakurugenzi wote 185 walioteuliwa, 65 wameteuliwa kutoka orodha ya wakurugenzi wa zamani na 120 ni wakurugenzi wapya.
Orodha ya wakurugenzi walioteuliwa kulingana na mikoa yao ni kama ifuatavyo;

ARUSHA
⦁ Arusha Jiji – Athumani Juma Kihamia

⦁ Arusha DC – Dkt. Wilson Mahera Charles

⦁ Karatu DC – Banda Kamwande Sonoko

⦁ Longido DC – Jumaa Mohamed Mhiwapijei

⦁ Meru DC – Kazeri Christopher Japhet

⦁ Monduli DC – Stephen Anderson Ulaya

⦁ Ngorongoro DC – Raphael John Siumbu


DAR ES SALAAM
⦁ Dar es salaam Jiji – Siporah Jonathan Liana

⦁ Kinondoni Manispaa – Aron Titus Kagurumjuli

⦁ Temeke Manispaa – Nassibu Bakari Mmbaga

⦁ Ilala Manispaa – Msongela Nitu Palela

⦁ Kigamboni Manispaa – Stephen Edward Katemba

⦁ Ubungo Manispaa – Kayombo Lipesi John


DODOMA
⦁ Dodoma Manispaa – Dkt. Leonard M. Masale

⦁ Kondoa DC – Kibasa Falesy Mohamed

⦁ Kondoa Mji – Khalifa Kondo Mponda

⦁ Mpwapwa DC – Mohamed Ahamed Maje

⦁ Kongwa DC – Mhandisi Ngusa Laurent Izengo

⦁ Chemba DC – Semistatus Hussein Mashimba

⦁ Chamwino DC – Athuman Hamis Masasi

⦁ Bahi DC – Rachel Marcel Chuwa


GEITA
⦁ Bukombe DC – Dionis Maternus Nyinga

⦁ Chato DC – Mhandisi Joel Bahahari

⦁ Geita DC – Ally Abdallah Kidwaka

⦁ Geita Mji – Modest J. Apolinaly

⦁ Mbogwe DC – Mahwago Elias Kayandabila

⦁ Nyang’wale DC – Carlos K. Gwamagobe


IRINGA
⦁ Iringa Manispaa – William Donald Mafwele

⦁ Mafinga Mji – Saada S. Mwaruka

⦁ Mufindi DC – Riziki Salas Shemdoe

⦁ Iringa DC – Robert Mgendi Magunya

⦁ Kilolo DC – Aloyce Kwezi


KAGERA
⦁ Biharamulo DC – Wende Israel Ng’ahala

⦁ Bukoba DC – Abdulaaziz Jaad Hussein

⦁ Bukoba Manispaa – Makonda Kelvin Stephen

⦁ Karagwe DC – Godwin Moses Kitonka

⦁ Kyerwa DC – Shedrack M. Mhagama

⦁ Missenyi DC – Limbe Berbad Maurice

⦁ Muleba DC – Emmanuel Shelembi Luponya

⦁ Ngara DC – Aidan John Bahama


KATAVI
⦁ Mlele DC – Alex Revocatus Kagunze
⦁ Mpimbwe DC – Erasto Nehemia Kiwale

⦁ Mpanda DC – Ngalinda Hawamu Ahmada

⦁ Mpanda Manispaa – Michael Francis Nzyungu

⦁ Nsimbo DC – Joachim Jimmy Nchunda


KIGOMA
⦁ Buhigwe DC – Anosta Lazaro Nyamoga

⦁ Kakonko DC – Lusubilo Joel Mwakabibi

⦁ Kasulu DC – Godfrey Msongwe Masekenya

⦁ Kasulu Mji – Fatina Hussein Laay

⦁ Kigoma Ujiji – Manispaa – Judethadeus Joseph Mboya

⦁ Kigoma DC – Hanji Yusuf Godigodi

⦁ Kibondo DC – Shelembi Felician Manolo

⦁ Uvinza DC – Weja Lutobola Ng’olo


KILIMANJARO
⦁ Manispaa ya Moshi – Michael Nelson Mwandezi

⦁ Hai DC – Yohana Elia Sintoo

⦁ Siha DC – Valerian Mwargwe Juwal

⦁ Same DC – Shija Anaclaire

⦁ Mwanga DC – Golden A. Mgonzo

⦁ Rombo DC – Magreth Longino John

⦁ Moshi DC – Emalieza Sekwao Chilemeji


LINDI
⦁ Kilwa DC – Bugingo I. N. Zabron

⦁ Lindi DC – Samwel Warioba Gunzar

⦁ Lindi Manispaa – Jomaary Mrisho Satura

⦁ Liwale DC – Justine Joseph Monko

⦁ Nachingwea DC – Bakari Mohamed Bakari

⦁ Ruangwa DC – Andrea Godfrey Chezue


MANYARA
⦁ Babati Mji – Fortunatus Hilario Fwema

⦁ Hanang DC – Bryceson Paul Kibasa

⦁ Mbulu DC – Festi Fungameza Fwema

⦁ Mbulu Mji – Anna Philip Mbogo

⦁ Simanjiro DC – Yefred Edson Myezi

⦁ Kiteto DC – Tamim Kambona

⦁ Babati DC – Hamis Iddi Malinga


MARA
⦁ Manispaa ya Musoma – Fidelica Gabriel Myovela

⦁ Bunda DC – Amos Jeremiah Kusaja

⦁ Bunda Mji – Janeth Peter Mayanja

⦁ Butiama DC – Solomon Kamlule Ngiliule

⦁ Musoma DC – Flora Rajab Yongolo

⦁ Serengeti DC – Juma Hamsini Seph

⦁ Rorya DC – Charles Kitanuru Chacha

⦁ Tarime DC – Apoo Castro Tindwa

⦁ Tarime Mji – Hidaya Adam Usanga


MBEYA
⦁ Busokelo DC – Eston Paul Ngilangwa

⦁ Chunya DC – Sofia Kumbuli

⦁ Kyela DC – Mussa Joseph Mgata

⦁ Mbarali DC – Kivuma Hamis Msangi

⦁ Mbeya DC – Ameichiory Biyengo Josephat

⦁ Mbeya Jiji – Zacharia Nachoa Ntandu

⦁ Rungwe DC – Loema Isaya Peter


SONGWE
⦁ Momba DC – Adrian Jovin Jungu

⦁ Tunduma Mji – Valery Alberth Kwemba

⦁ Mbozi DC – Edna Amulike Mwaigomole

⦁ Ileje DC – Haji Mussa Mnasi

⦁ Songwe DC – Elias Philemon Nawela


MOROGORO
⦁ Gairo DC – Agnes Martin Mkandya

⦁ Kilombero DC – Dennis Lazaro Londo

⦁ Ifakara Mji – Francis Kumba Ndulane

⦁ Kilosa DC – Kessy Juma Mkambala

⦁ Morogoro DC – Sudi Mussa Mpili

⦁ Morogoro Manispaa – John Kulwa Magalula

⦁ Mvomero DC – Florent Laurent Kyombo

⦁ Ulanga DC – Audax Christian Rukonge

⦁ Malinyi DC – Marcelin Rafael Ndimbwa


MTWARA
⦁ Mtwara DC – Omari Juma Kipanga

⦁ Mtwara Mikindani Manispaa – Beatrice Dominic Kwai

⦁ Masasi Mji – Gimbana Emmanuel Ntayo

⦁ Masasi DC – Mkwazu M. Changwa

⦁ Nanyumbu DC – Hamis Hassan Dambaya

⦁ Newala DC – Mussa Mohamed Chimae

⦁ Newala Mji – Andrew Frank Mgaya

⦁ Tandahimba DC – Said Ally Msomoka

⦁ Nanyamba Mji – Oscar Anatory Ng’itu


MWANZA
⦁ Mwanza Jiji – Kiomoni Kibamba Kiburwa

⦁ Ilemela Manispaa – John Paul Wanga

⦁ Kwimba DC – Pendo Anangisye Malabeja

⦁ Magu DC – Lutengano George Mwalwiba

⦁ Misungwi DC – Eliud Leonard Mwaiteleke

⦁ Ukerewe DC – Tumaini Sekwa Shija

⦁ Buchosa DC – Crispian Methew Luanda

⦁ Sengerema DC – Magesa M. Boniphace


NJOMBE
⦁ Njombe Mji – Iluminata Leonald Mwenda

⦁ Makambako Mji – Paul Sostenes Malala

⦁ Makete DC – Francis Emmanuel Namaumbo

⦁ Njombe DC – Monica Peter Kwiluhya

⦁ Ludewa DC – Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija

⦁ Wanging’ombe DC – Amina Mohamed Kiwanuka


PWANI
⦁ Bagamoyo DC – Azimina A. Mbilinyi

⦁ Chalinze DC – Edes Philip Lukoa

⦁ Kibaha DC – Tatu Seleman Kikwete

⦁ Kibaha Mji – Jenifer Christian Omolo

⦁ Kisarawe DC – Mussa L. Gama

⦁ Mafia DC – Erick Mapunda

⦁ Mkuranga DC – Mshamu Ally Munde

⦁ Kibiti DC – Alvera Kigongo Ndabagoye

⦁ Rufiji DC – Salum Rashid Salum


RUKWA
⦁ Kalambo DC – Simon Ngagani Lyamubo

⦁ Sumbawanga DC – Nyangi John Msemakweli

⦁ Sumbawanga Manispaa – Hamid Ahmed Njovu

⦁ Nkasi DC – Julius M. Kaondo


RUVUMA
⦁ Mbinga DC – Gumbo Samanditu Gumbo

⦁ Mbinga Mji – Robert Kadaso Mageni

⦁ Namtumbo DC – Christopher Michael Kilungu

⦁ Nyasa DC – Oscar Albano Mbuzi

⦁ Songea DC – Simon Michael Bulenganija

⦁ Madaba DC – Shafi Kassim Mpenda

⦁ Tunduru DC – Abdallah Hussein Mussa

⦁ Songea Manispaa – Tina Emelye Sekambo


SHINYANGA
⦁ Kishapu DC – Stephen Murimi Magoiga

⦁ Msalala DC – Berege Sales Simon

⦁ Shinyanga DC – Mark Emmanuel Malembeka

⦁ Kahama Mji – Anderson David Msumba

⦁ Shinyanga Manispaa – Lewis Kweyemba Kalinjuna

⦁ Ushetu DC – Michael Augustino Matomola


SIMIYU
⦁ Bariadi DC – Abdallah Mohamed Malela

⦁ Bariadi Mji – Melkizedek Oscar Humbe

⦁ Itilima DC – Mariano Manyingu

⦁ Maswa DC – Fredrick Damas Sagamiko

⦁ Busega DC – Anderson Njiginya

⦁ Meatu DC – Said F. Manoza


SINGIDA
⦁ Ikungi DC – Rustika William Turuka

⦁ Iramba DC – Linno Pius Mwageni

⦁ Mkalama DC – Martin Msuha Mtanda

⦁ Manyoni DC – Charles Edward Fussi

⦁ Itigi DC – Luhende Pius Gerald

⦁ Singida DC – Rashid Mohamed Mandoa

⦁ Singida Manispaa – Kizito L. Brava


TABORA
⦁ Igunga DC – Revocatus Lubigili Kuuli

⦁ Kaliua DC – John Marco Pima

⦁ Nzega DC – Jacob James Mtalitinya

⦁ Nzega Mji – Phillimon Mwita Magesa

⦁ Sikonge DC – Simon Saulo Ngatunga

⦁ Tabora Manispaa – Bosco Addo Ndunguru

⦁ Urambo DC – Magreth Nakainga

⦁ Tabora -Uyui – Hadija Maulid Makuani


TANGA
⦁ Tanga Jiji – Daudi R. Mayeji

⦁ Korogwe DC – George John Nyaronga

⦁ Korogwe Mji – Jumanne Kiangoshauri

⦁ Muheza DC – Luiza Osmin Mlelwa

⦁ Handeni Mji – Keneth K. Haule

⦁ Handeni DC – William Methew Mafukwe

⦁ Pangani DC – Sabas Damian Chambasi

⦁ Mkinga DC – Mkumbo Emmanuel Barnabas

⦁ Bumbuli DC – Peter Isaiah Nyalali

⦁ Kilindi DC – Clemence Andagile Mwakasenda

⦁ Lushoto DC – Kazimbaya Makwega Adeladius


Wakurugenzi wote walioteuliwa wametakiwa kufika Ikulu Jijini Dar es salaam siku ya Jumanne July 12 2016 saa tatu asubuhi kwa ajili ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

Tuesday, July 5, 2016

Uganda na Tanzania wajadili bomba la mafuta



 

Baada ya tangazo la marais wa Uganda na Tanzania sasa maafisa wameanza vikao vya utekelezaji mradi wa bomba la mafuta
Uganda na Tanzania zimeanza upya mazungumzo utekelezaji wa makubaliano baina ya viongozi wa mataifa hayo mawili kupitisha mradi wa bomba la mafuta kupitia Hoima Tanga badala ya Hoima - Lamu Kenya.
Ujumbe wa Uganda unaongozwa na waziri wa kawi Irene Muloni huku Tanzania wakiongozwa na Prof Sospeter Muhongo.


Wengine wanaohudhuria mazungumzo hayo huko Hoima ni wawakilishi wa kampuni ya kuchimba mafuta yenye asili yake nchini Uingereza Tullow, mjumbe wa kampuni ya kuuza mafuta ya Total yenye asili yake nchini Ufaransa na kisha
kampuni ya kichina ya CNOOC inayotekeleza mradi wenyewe wa kuchimba na kuweka bomba la mafuta Kuanzia Hoima hadi bandari ya Tanga.

 
Bomba hilo la mafuta litakwenda kilomita 1,400km kuanzia Hoima, hadi kwenye bandari ya Tanga.
Mada kuu ya mazungumzo hayo huko Hoima ni utekelezaji wa miradi kwa kuzungumzia hali halisia.
Kwa mfano maswala ya ardhi itakayotumika kwa mradi huo itamilikiwa na nani na itatwaliwa vipi kutoka kwa uma, pia kuna swala la ukubwa wa ardhi yenyewe, wanadani wanasema kuwa mradi huo ulikuwa umependekezwa utekelezwe kwenye ardhi ya takriban mita 20 ,sasa hilo linaonekana kupata upinzani na hivyo kunahoja mbadala ukubwa huo upunguzwe katika mradi huo utakaotekelezwa kwa umbali wa kilomita 1403
Uganda yavunja mkataba na kampuni ya Urusi
Uganda kupitishia mafuta yake Tanzania

Kenya iliamua kujenga bomba la mafuta kutoka Turkana hadi Lamu

Aidha swala la ujenzi wa mtambo wa kusafishia mafuta wenye thamani ya dola bilioni 2.5 uliopata pigo baada ya Serikali ya Uganda kukatiza mazungumzo na kampuni moja ya Urusi pia utajadiliwa.
Uganda imeanza mazungumzo mbadala na kampuni moja ya ujenzi kutoka Korea Kusini.
Uganda ilikuwa imependekeza kujenga bomba la mafuta safi mkabala na bomba la mafuta la Hoima -Tanga.
Mkurugenzi wa usafirishaji wa mafuta nchini Uganda Robert Kasande akizungumza na wanahabari alisema kuwa tayari wajumbe wamekubaliana mambo mengi kati ya maswala makuu yaliyohitaji kujadiliwa.

Rais Magufuli atengua na kufanya uteuzi mwingine leo July 05 2016




Taarifa niliyoipokea kutokea ikulu inasema kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act) Sura 1, leo tarehe 5 Julai, 2016 ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB Prof. William Lyakurwa.

Kufuatia hatua hiyo, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (2) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act) Sura 257, Rais Magufuli amemteua Prof. Palamagamba J. A. M. Kabudi kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kufuatia mabadiliko hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act) Sura 1, ametengua uteuzi wa Wajumbe Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB. 

Aidha, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (1) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act, Sura 257) Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango ameteua wajumbe wapya wa Bodi wafuatao kwa kipindi cha miaka mitatu

⦁ Brig. Gen (Rtd) Mabula Mashauri
⦁ Dkt. Razack B. Lokina

⦁ Bi. Rose Aiko

⦁ Prof. Joseph Bwechweshaija

⦁ Bw. Said Seif Mzee

⦁ Dkt. Arnold M. Kihaule

⦁ Bw. Maduka Paul Kessy

⦁ Bw. Charles Singili

Uteuzi wa Mwenyekiti na Wajumbe wapya wa Bodi unaanza tarehe leo July 5 2016.

Baada ya ajali mfululizo zilizohusisha mabasi, polisi wamekuja na hii taarifa


Ni takribani wiki moja yametokea matukio makubwa matatu ya ajali za barabarani mfululizo ambayo yamehusisha mabasi yanayofanya safari zake mikoani, taarifa ya polisi imesema ajali hizo zimesababisha jumla ya vifo vya watu 46 na majeruhi 73.

Matukio hayo yanahusisha ajali iliyotokea June 28 2016 Misungwi Mwanza  ambapo basi la kampuni ya Super Samy likitokea Shinyanga kwenda Mwanza lilipata ajali kwa kuacha njia na kupinduka hivyo kusababisha vifo wa watu 5 na majeruhi 13.

Tukio lingine ni mnamo July 01 2016  VETA Dakawa katika barabara ya Morogoro/Dodoma malori mawili yaligongana na kuwaka moto na kusababisha vifo vya watu 5 na  na baadae katika eneo hilohilo siku July 02 2016 usiku gari la kampuni ya OTA lilipata ajali kwa kuyagonga mabaki ya malori yaliyopata ajali na kubaki eneo la tukio na kusababisha vifo  vya watu 6 na majeruhi 6

Halikadhalika mnamo July 04 2016 maeneo ya Maweni-Kintiku Singida mabasi mawili ya kampuni ya City Boys yaligongana na kusababisha vifo wa 30 na majeruhi 54 ambapo hadi leo wamebaki majeruhi 33 wakiendelea na matibabu. Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi, kikosi cha usalama barabarani, Mohamed Mpinga amesema
>>>’kwa ajali iliyotokea Maweni Singida siyo ajali ya kawaida bali ni tukio la kufanya mauaji bila kukusudia, hivyo polisi imedhamiria kuwafikisha mahakamani madereva waliohusika na ajali hiyo kwa mashtaka ya mauaji bila kukusudia kutokana na taarifa za awali za chanzo cha kutokea kwa ajali hiyo kwamba madereva wa mabasi hayo walikuwa wakifanya mzaha wakati wa kupishana.

>>>Aidha tumewasiliana na wenzetu wa SUMATRA, kampuni ya mabasi ya City Boys na makampuni mengine yaliyohusika katika ajali yafungiwe kutoa huduma za usafirishaji katika njia zote hapa nchini

Zamaradi kuhusu mahojiano na mwanaume anayejihusisha mapenzi ya jinsia moja

Kama utakuwa unakumbuka hivi karibuni mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi aliingia kwenye headlines za kufanya mahojiano na mwanaume anayejihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Sasa leo July 5, 2016 amezungumza na Ayo TV kueleza kile ambacho alikuwa akitarajia baada ya kurusha mahojiano hayo na kusema….‘Nilitarajia kwamba kuna watu watakuwa hawanielewi kwa kile nilichokuwa nakifanya na yule mtu, kwahiyo nilijua kwamba kuna aina ya watu ambao ni vigumu sana na kama utakuwa unakumbuka kabla ya kuanza kipindi nilisema najua kuna watu watanikosoa kwa kile ninachokirusha kwahiyo impact imekuwa kubwa’- Zamaradi

PICHA 15: DC Gondwe rasmi ofisini kwake Handeni Tanga!

Mtangazaji mkongwe Godwin Gondwe ni miongoni mwa wakuu wa Wilaya wapya walioteuliwa na Rais Magufuli ambaye mwishoni mwa wiki alikuwa ni miongoni mwa wakuu wa wilaya wapya nane wa wilaya za mkoa wa Tanga walioapishwa na mkuu wa mkoa huo, Martin Shigela, kushika wadhifa huo.
Gondwe ameteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Handeni na hapa rasmi ameanza kutekeleza majukumu yake
13495301_1026842670733760_2749475014848608034_n
.
13516149_1026842207400473_6121894779098771318_n
.
13435456_1026841477400546_1374006405219847851_n
13528754_1026843010733726_2728326069503132052_n
13557670_1026841917400502_1946866140714881756_n
.
13557676_1026841860733841_3504302852576707063_n
13567067_1026842744067086_7480311689404712173_n
.
13567480_1026843117400382_5163859454991466912_n
.
13567293_1026843074067053_2688152585902801072_n
.
13590228_1026842850733742_2155676313116316571_n
.

13590398_1026842484067112_1792617471443967264_n
.
13590504_1026842294067131_3447681663306351623_n
.
13599852_1026841610733866_1859383303269268075_n
.
13620253_1026841664067194_2102052997560850740_n
DC Gondwe akipokea mchango wa madawati kutoka kwa mwakilishi wa A to Z Company .







13620932_1026841570733870_5882275500979903394_n