Thursday, February 18, 2016

MATOKEO KIDATO CHA NNE YATANGAZWA ANGALIA HAPA



NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2015 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES 


Baraza la mitihani nchini(NECTA) leo Februari 18, 2016 limetoa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne iiyofanyika mwishoni mwa mwaka 2015.

Ufaulu umeshuka kwa 1.85% toka 69.75% mwaka 2014 hadi 67.91% mwaka 2015.

BOFYA HAPA KUANGALIA CSEE 2015

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Wednesday, February 10, 2016

SHULE YA MSINGI LUPEMBA ILIYOKO MAGU YAKABILIWA NA UHABA WA MAJENGO NA MADAWATI


Moja ya madarasa wanayotumia wanafunzi wa shule ya msingi lupemba iliyoko wilayani magu 
NA Shushu Joel,Magu
TUMEZOEA kusikia shule zilizoko vijijini ndani ndani ndizo zinakabiliwa na tatizo la madawati na majengo,lakini kumbe hata zile za karibu na mijini bado ni shida kwani shule ya msingi Lupemba iliyoko wilayani magu mkoani mwanza inakabiliwa na matatizo hayo
Shule hiyo iliyoko karibu kabisha na ofisi za mji mdogo wa halmashauri ya magu,inapungukiwa madawati zaidi ya 400 na majengo ya madarasa yasiyopungua 5, licha ya kuwa karibu na ofisi hizo, lakini cha kushangaza zaidi hakuna kiongozi wa aina yeyote ile ambaye amefikilia chochote kile juu ya kutatua tatizo hilo linalowakabili wanafunzi hao wanaosomea kwenye mahema na matofali.
Lupemba shule ya msingi iliyoko wilayani magu wakipata masomo


Shule hii ya Lupemba ilifunguliwa rasmi miaka michache tu iliyopita,pamoja na upungufu wa madawati na majengo bado pia inakumbwa na tatizo la upungufu wa walimu kwani waliopo ni walimu 8 tu wanawake ni 5 na 3 ni wanaume huku shule ikiwa na jumla ya wanafunzi 620.
Hayo ni baadhi tu ya matatizo yanayoikabili shule hiyo ya msingi Lupemba ambayo idadi kubwa ya wanafunzi wanaishia kukaa chini na kusomea kwenye mahema na huku wakiendelea na shughuli zao zingine za darasani kama ilivyozoeleka kwa wanafunzi wetu.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Daniel Matemi anathibitisha uwepo wa tatizo hilo katika shule yake na kusema kuwa suala hili hata yeye amelikuta katika shule hiyo ingawa amekwisha lifikisha katika sehemu husika ila mpaka sasa bado hakuna lolote lililofanyika.
Shule ya Msingi Lupemba Wilayani Magu Inasikitisha

“Tumewabana sana wazazi wa wanafunzi wetu katika michango mbalimbali japo tuweze kuinusuru shule hii lakini suala hili linakuwa ngumu kwa upande wa wazazi hao nah ii ni kutokana na siasa chafu zilizopo katika kijiji hiki na hili ni kutofautiana kwa vyama kati ya mwenyekiti wa shule na mwenyekiti wa kijiji ndio changamoto kubwa inayochangia kuwaumiza wanafunzi hao.
Mkuu huyo aliongeza kuwa kilichobaki kwa sasa ni kuwaomba wafadhili walio na moyo ili wajitokeze kuweza kuifadhili shule hii na kuweza kuinusuru katika janga hili kwani kipindi hiki cha mvua sijui itakuwaje kwa wale wa darasa la 5,6 na 3 ambao wanasomea kwenye mahema,kwa kusema ukweli watoto hawa wanapata taabu sana.
“Ndugu mwandishi kama unavyojua sisi wenyewe hatuna cha kuwasaidia,kama unavyofahamu kuwa mwanafunzi anayekaa chini unamkosesha mambo mengi sana” alisema mkuu huyo wa shule.
Lupemba shule ya msingi iliyoko wilayani magu wakipata masomo

Kwa ujumla hali hii inawafanya wanafunzi hao kupunguza uwezo wao wa kufanya vizuri darasani.
Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi wilaya ya magu Yesse Kanyuma alipohojiwa juu ya shule hiyo alisema kuwa yeye si msemaje juu ya hilo na wala ajui lolote kuhusu shule hiyo ya lupemba.
N kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Ntinika  Paul alipopigiwa simu yake ili kuthibitisha kwa habari ya shule hii simu yake iliiita bila kupokelewa.
 
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Lupemba Wakiwa Darasani Wakiendelea na Masomo yao Wilayani Magu Mkoani Mwanza
MWISHO
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.