Friday, February 22, 2013

Jisajili Hapa Kwa wanaotaka kufanya mtihani wa kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) mwezi Novemba 2013 kama watahiniwa wa kujitegemea Kwa huraisi


T A N G A Z O   

Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu wote wanaotaka kufanya mtihani wa kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) mwezi Novemba 2013 kama watahiniwa wa kujitegemea kwamba kipindi cha usajili kitaanza rasmi tarehe 01/01/2013 kwa ada ya shilingi 35,000/= kwa CSEE na 20,000/= kwa QT. Kipindi cha malipo bila adhabu kinaishia tarehe 28 Februari 2013.

Kuanzia tarehe 01 Machi 2013 hadi tarehe 31 Machi 2013 waombaji watajisajili kwa ada ya shilingi 50,000/= kwa CSEE na 30,000/= kwa QT (ada pamoja na faini).

Waombaji wote watajisajili kwa njia ya mtandao kupitia tovuti: www.necta.go.tz. ya Baraza la Mitihani la Tanzania. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao, waombaji watapaswa kwenda kwenye vituo vya mitihani kuchukua namba rejea (reference number) watakazotumia kujisajili. Hakuna mtahiniwa atakayeweza kujisajili bila kupata namba rejea kutoka katika kituo anachokusudia kufanyia mtihani. Wakuu wote wa vituo nchini wamekabidhiwa namba rejea hizo tayari kwa kuzigawa kwa watahiniwa tarajali bila malipo.

Bofya Hapa Kujisajili
 
LIMETOLEWA NA:

KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA


Bofya Hapa Kujisajili

 Hakikisha wakati wa kufungua "account" unaandika anwani ya barua pepe (email) sahihi inayotumika. Ukishindwa kutoa anwani sahihi ya barua pepe, itakua vigumu kupatiwa huduma zifuatazo:
  1. Kupata password mpya na username iwapo utazisahau!

  2. Kukutumia taarifa mbalimbali za kukusaidia unapokwama kwenye zoezi la usajili.
Tunaomba ushirikiano wako katika kutekeleza tangazo hili ili tuweze kukuhudumia ipasavyo.

 
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Upinzani nchini Djibout kushiriki uchaguzi wa bunge leo baada ya kususia kwa miaka 10.



Uchaguzi wa bunge nchini Djibout unafanyika leo ambapo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 10 upinzani unashiriki.

Uchaguzi huu unafanyika miaka miwili baada ya rais Ismail Omar Guelleh kuchaguliwa kuongoza nchi hiyo kwa mhula wa tatu.

Chama chake cha PRP kimekuwa kikishinda uchaguzi tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mnamo mwaka 1977 kutoka mikononi mwa Ufaransa.

Upinzani umekuwa ukisusia uchaguzi kwa madai kuwa hakuna uwezekano wa kushinda katika mfumo wa vyama vya wafuasi wa mirengo tofauti serikalini chini ya rais Guelleh.

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Thursday, February 21, 2013

Jack wa Chuzi amdhalilisha Isabale Kuhusu wanaume anaotembea nao Isabela


WAKATI kukiwa na bifu la chini kwa chini kati ya wasanii wawili Jack wa Chuz na Isabela, hali imekuwa tofauti ambapo Jack ameamua kufunguka na kudai kuwa msanii huyo ni malaya na analala na wanaume walala hao, huku akijifanya matawi ya juu.

Kauli hiyo imekuja mara baada ya mwandishi wa
DarTalk, kuzungumza na Jack juu ya maneno ya chini chini yanayosambazwa na Isabela juu yake, yanayodai kuwa alisababisha kumuachananisha na bwana ake.

Jack
alidai kuwa kamwe hawezi kutembea na wanaume wanatoka na msanii huyo kwani hawana ubora huku wengi ni walala hoi wasiyojiweza hata kimaisha.

Alienda mbali zaidi kwa kudai kuwa kutokana na hali ya uchafu aliyonayo msanii huyo, hakuna mwanaume analiyewahi kutoka na yeye anayeweza kumtamani kwani ana mwili ambao hata mvuto hauna.


“Sijawahi kutembea na bwana wa Isabela sasa inakuwaje anazungumza mambo ya uongo tena ya chini kwa chini hana lolote nahisi anatafuta jina yeye wanaume zake wote walala hoi sasa itakuwaje watoke na mimi wakati hawana cha kunipa,”
alihoji Jack.

Hata hivyo kwa mujibu wa maneno ya
Isabela alidai kuwa Jack aliwahi kumfanya asielewane na mpenzi wake baada ya kumtaka kimapenzi huku akijua wazi kuwa anatokana na yeye miaka yote.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

HICHI NDO WALICHO SEMA WEMA NA AUNT EZEKIEL KUHUSU PICHA WALIZOPIGWA WAKIKATA 'MAUNO'



“Sisi tumecheza tumefurahi tu hawa waliofunga mtaa kututazama watakuwa wanataka kuona mavituzi yetu,” alisema Wema. 
 
Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wakikata mauno. 
Mpango mzima ulitokea hivi karibuni katika arobaini ya mtoto wa dada yake Wema iliyofanyika Sinza Kwa - Remmy, jijini Dar ambapo Aunt pamoja na baadhi ya wasanii walifika kusherehekea sherehe hiyo ya kumtoa mtoto.
 
 ...Warembo hao wakiwa katika pozi.
Awali, Wema alionekana akimtunza fedha pamoja na mikufu ya dhahabu yenye thamani kubwa na ilipoisha sherehe ya maulid ndipo mastaa hao waliwasha muziki na kuanza kulisakata rumba.
 
...Wakizidi kumwaga radhi.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Acheni kutibiwa kwa Waganga wa Jadi nendeni Hospitali: Mama Salma Kikwete



Mama Salma Kikwete
Na Anna Nkinda, Maelezo  Lindi

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Mama Salma Kikwete amewataka wakazi wa wilaya ya Lindi mjini  kujenga mazoea ya kwenda hospitali kupima afya zao mara kwa  mara na kuachana na tabia ya kwenda kutibiwa kwa waganga wa jadi na kushikana uchawi kutokana na maradhi yanayowasumbua.

Mama Kikwete ambaye pia ni Mke wa Rais alitoa rai hiyo  jana alipokuwa  akiongea kwa nyakati tofauti na wakazi wa kata za Matopeni na Wailesi zilizopo wilaya ya Lindi mjini wakati wa ziara yake ya kichama ya siku saba katika wilaya ya Lindi mjini ya kuwashukuru wanachama wa CCM kwa kumchagua kuwa mjumbe wa NEC.

Aliwasihi watu wenye tabia ya kutopenda kupima afya zao wakati wanaumwa na wale wenye tabia za kukimbilia kwa waganga wa jadi huku wakijua fika kuwa ni wagonjwa waache kwani wanaweza kupoteza maisha kwa magonjwa ambayo wangeweza kutibiwa katika vituo vya afya na kupona.

“Hakuna mtu asiyejua kuwa kuna Ugonjwa wa Ukimwi, muache suala la kushikana uchawi katika hili kwani ugonjwa huu haupatikani kwa kurogwa. Mtu mwenye virusi vya ukimwi  anapimwa  kinga za mwili za kupambana na magonjwa ( CD4) kama zipo chini atapewa dawa za kuongeza na akitumia dawa atakuwa na nguvu na kuweza kufanya kazi zake kama zamani jambo la muhimu asipitishe muda wa kuzitumia” , alisema Mama Kikwete.

Aidha Mjumbe huyo wa NEC alisema kuwa jamii nzima inahusika katika ulezi wa watoto lakini jambo la kusikitisha ni kuwa hivi sasa watu wamebadilisha mienendo ya maisha kila mtu anahangaika kulea mwanawe. Na kuwasihi wakazi wa Lindi kufuata maadili ya  zamani ya kuwalea watoto  kwani mtoto wa mwenzako ni wako .

“Ni jukumu la jamii nzima kuwalea watoto wao kwa kufuata  mila za kitanzania , wazazi ambao wakiambiwa kuwa watoto wao wanamienondo mibaya na kuja juu badala ya kuzifanyia kazi taarifa hizo waache tabia hiyo kwani watoto wakilelewa vizuri hata shuleni watakuwa na maadili mazuri na kuweza kufanya vizuri katika masomo yao”, alisema.

Kuhusu ufanyaji kazi kwa ushirikiano Mama Kikwete aliwataka wananchi hao kuachana na  mambo ya siasa kwani uchaguzi umeshapita hivyo basi wafanye kazi za maendeleo kwa na kujenga tabia ya kujitolea kufanya kazi.

Mama Kikwete alihoji,  “Hawa wazungu manaowaona wanakuja Lindi kufanya kazi wamekuja kujitolea ni jambo la muhimu kujitolea kufanya kazi za maendeleo, ukiambiwa kuna ujenzi wa shule, Zahanati wewe nenda ukajitolee usiseme ile si kazi ya Serikali sasa Serikali ni nani kama si wewe mwananchi?”.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi 2010 – 2015 Diwani wa kata ya Matopeni Suleiman Namkoma alisema kuwa idadi ya watoto wanaoanza darasa la kwanza imeongezeka kutoka 45 hadi 60, kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi wanaofanya mtihani wa darasa la saba kutoka 20 hadi 43, kuongezeka kwa barabara zinazopitika kipindi cha masika na kiangazi na kuimarika kwa miundombinu na barabara za mifereji.

Namkoma alisema, “Tunakabiliwa na changamoto za uchache wa wataalam wa kada mbalimbali ngazi ya kata na jamii kukosa wataaluma wa huduma stahiki, ukosefu wa uwajibikaji kwa baadhi ya watumishi wa ngazi ya kata, ukosefu wa huduma ya maji safi na salama, kuchelewa kwa ruzuku ya Serikali kuu na makusanyo madogo ya Halmashauri na upungufu wa walimu wa shule ya msingi”.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mikumbi Zahara Suleiman alisema kuwa katika kata hiyo kuna vikundi vingi vya maendeleo lakini kwa mwaka 2010/2013 hakuna vikundi vilivyokopeshwa na Seambavyo ni  Ayayoli na Mafundi Seremali.

Suleiman alisema, “Tunawashukuru wafadhili waliovikopeshwa baadhi ya vikundi vyetu vya maendeleo kwani  kikundi cha Mwambao Fishing Group kilipewa na Mama Salma Kikwete boti na vifaa vya kuvulia vyenye thamani ya shilini milioni 57  na kikundi cha Uganda kilipewa pesa kutoka MACEP shilingi milioni 15”.

Katika mkutano wa kata ya Mikumbi   Mjumbe huyo wa NEC aliwapokea vijana 18  waliokuwa wanachama wa CUF na kujiunga  na CCM. Akiwa katika kata za Matopeni, Wailesi  na Mikumbi alikabidhi  kadi  kwa wanachama  wapya wa CCM 43 , Umoja wa vijana 60, Umoja wa Wanawake  22 na Jumuia ya Wazazi  59.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Kampuni ya Deloitte yafanya Utafiti wa Teknolojia na Mawasiliano kwa Miezi 18-24 Ijayo.



Mkurugenzi wa Kampuni ya Deloitte nchini Kenya, Bw. Nikhil Hira akiongea katika mkutano na wadau wa teknolojia na mawasiliano leo ambapo alisema kuwa kwa utafiti mdogo ambao wameuanza unaonyesha kuwa watu wengi wamekuwa wakitizama TV kwa kutumia komputa. Mkutano huo ulifanyika  hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Deloitte nchini Uholanzi, Bw. Jean Diop akisisitiza jambo katika mkutano na wadau wa teknolojia na mawasiliano leo hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Wadau wa teknolojia na mawasilianowaliohuduria katika mkutano huo.
Mmoja ya wadau wa teknolojia na mawasiliano akiuliza swali.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

RAIS WA KENYA AZINDUA BARABARA YA MWAI KIBAKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO



   Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Mwai Kibaki wa Kenya wakiongozwa na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph  Mwenda kutembea hatua chache kabla ya kuzindua rasmi jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.


 Rais Mwai Kibaki wa Kenya akikata utepe, akishuhudiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda kuzindua rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 201
 Rais Mwai Kibaki wa Kenya akifunua pazia, akishuhudiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda akizindua rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.



  Madiwani wa kinondoni
 Bendi ya Vijana Jazz ikitumbuiza wakati wa uzinduzi rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013. 
 MC Ephraim Kibonde akiwa kazini katika uzinduzi  rasmi wa  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.
 Sehemu ya barabara iliyopewa  rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.
  Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda akimkaribisha Rais Mwai kibaka na Mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika uzinduzi  rasmi wa  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013. 
    Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda akimkabidhi zawadi ya kasha la Zanzibar Rais Mwai kibaka huku  Mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia katika uzinduzi  rasmi wa  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013. PICHA NA IKULU.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

PICHA ZA NGONO ZA RAYUU ZA SAMBAA MTANDAONI




MTANDAO wetu, umezinasa picha kadhaa za msanii Rayuu zinazomuonesha akiwa kwenye tendo la ndoa na mwanaume ambaye hajajulikana mara moja, ambazo kati ya hizo nyingine hazifai kuonekana machoni mwa watu kutokana na uvunjaji wa maadili.


Picha hizo zimeonekana kwenye mtandao mmoja maarufu wa nje zikiwa kwenye utata mkubwa huku mwanaume anayeonekana akiwa ni raia wa Tanzania, kutokana na utata wa wa mtandao huo ambao unahusika zaidi na picha za ngono. Mtandao huu baada ya kuzipata picha hizo, ulifanya uchunguzi kwa kumtafuta muhusika ili kuzungumza naye, ambapo hata hivyo mwenyewe alionekana kushutuka kwa madai kuwa hajui picha hizo zimetoka wapi.


Rayuu alidai kuwepo kwa picha hizo kwenye mitandao ya ngono anahisi wasi kuna baadhi ya watu wanataka kumchafua kwani hajawahi kushiriki kwenye picha yoyote ya ngono kama picha hizo zinavyomuonesha.
“Jamani mbona naonewa sana hizo picha mimi sijui zimetoka wapi, kwanza kama nimefanya mapenzi mimi watu kiwanawahusu nini acha wazitazame sina muda nao napenda kufanya mambo yangu siku zote,” aliongeza.
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Wednesday, February 20, 2013

Hiki ndio alichosema Dr.Cheni Kuhusu Kurudi kwa Lulu Shule Rasmi



BAADA ya kupata dhamana msanii wa filamu Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu ajipanga kujiendeleza na masomo ili aweza kupambana na changamoto za maisha.

Akizungumza na Maisha msanii wa filamu ambaye pia amekuwa ni mtu wa karibu  familia ya Lulu Mahfudh Hussein 'Dkt. Cheni' amebainisha kuwa Lulu yupo kwenye mchakato wa kurudi shule ili aweze kuendelea na masomo yake

Alisema kuwa ingawa familia ina mikakati hiyo suala kubwa linalokwamisha kwa sasa ni kipato kwani familia yake haina uwezo wa kumlipia msanii huyo na badala yake anatakiwa Lulu kuanza kufanya kazi ili aweze kujikwamua kwa hilo

Dkt. Cheni aliweka wazi kuwa kutokana na kipato cha familia ya msanii huyo hivyo anatakiwa kwa sasa aweze kufanya kazi ya filamu ili aweze kujimudu kama ilivyokuwa mwanzo na maisha yaendele

"Hapo awali alikuwa na uwezo wa kuidumia familia yake kwa njia ya kazi zake alikuwa anamsomesha mdogo wake wa mwisho pamoja na kulipa kodi ya nyumba alikuwa akifanya mambo mengi hivyo na swala la kusoma lijukumu lake pia" alisema

Mbali na hayo msanii Cheni alieleza kuwa Lulu yupo tayari kurudi shule ili aweze kujikwamua kielimu aweze kupambana na maisha hivyo jambo la msingi ni yeye kufikisha malengo yake aliyojipangia kwani umri wake bado ni mdogo na ananafasi kubwa ya kubadilisha maisha yake

Akizungumzia kwa upande wa kazi Dkt. Cheni aliweka wazi kuwa endapo Lulu akimuomba amsimamie kazi zake atafanya hivyo kwani yote ni katika nia njema ya kumfikisha msanii huyo katika malengo aliyojipangia
MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.

Tuesday, February 19, 2013

HALI ILIVYO KUWA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JANA KATIKA KESI YA SHEKH PONDA



 
 
Kesi ya Uchochezi na Uharibifu wa mali inayo mkabili Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake leo imeendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam huku Polisi wakiwa katika doria kali ya kuimarisha ulinzi katika viunga jirani na Mahakama hiyo ambayo imejizolea umaarufu mkubwa jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla kwa jinsi inavyo endesha kesi na watu wa aina mbalimbali kufikishwa katika mahakma hiyo kabla ya baade kesi zao kuhamia Mahakama Kuu kwa hatua zaidi za kisheria.

Father Kidevu Blog ilikuwepo kufuatilia matukio ya hapa na pale na zifuatazo ni picha mbali mbali za tukio hilo na pia kesi hiyo inataraji kuendelea tena Mahakamani hapo kesho.
 Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa katika basi la Magereza tayari kwa kurejeshwa Mahabusu.

 Msafara ukianza kutoka Mahakama ya Kisutu
 Wafuasi waliokuwa nje wakiimba wakati gari likitoka
 Wafuasi wa Sheikh Ponda Issa Pondawakilifuatilia gari lililombeba kiongozi wao wakati akitoka Mahakama ya Kisutu.
Mkazi wa jiji akipita kando ya kundi la Askari nje ya Mahakama ya Hakimu Mkzi Kisutu wakati Askari hao walipo imarisha Ulinzi nbje ya Mahakama hiyo.
 Ustaadh huyu alitishiwa na Mbwa akataka kutoka baruti
 Wengine zaidi wakitoka Mahakama ya Kisutu
Wakiwapokea na kuwapongeza wenzao wanao tuhumiwa pamoja na Ponda
 Kundi la Wafuasi likiwa limejikusanya karibu na Jengo la Sophia House huku Polisi wakiwa kando yao.
 Doria barabarani nayo ilikamilika
 Ulinzi ulikuwa ni wa Uhakika
 Mbwa maalum wa Polisi nao walikuwa kazini hapa wakikata kiu kutokana na jua kali.
 Hapa ni Fanya Fujo Uone  kilicho mfanya Kanga akose Manyoya shingoni
Kikosi maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKM) nacho kilikuwepo

MWARICK JAPHET TEKELE MUJUNGU Web Developer

ASANTE KWA KUTEMBELEA KING SELE BLOG KWA MSAADA ZAIDI WASILIANA NASI: E-mail.: mwarickit@gmail.com.